< Marko 10 >
1 Yesu alitoka hapo akaenda mkoani Yudea na hata ng'ambo ya mto Yordani. Umati wa watu ukamwendea tena, naye akawafundisha tena kama ilivyokuwa desturi yake.
And having risen thence, he doth come to the coasts of Judea, through the other side of the Jordan, and again do multitudes come together unto him, and, as he had been accustomed, again he was teaching them.
2 Basi, Mafarisayo wakamwendea, na kwa kumjaribu wakamwuliza, “Je, ni halali mtu kumpa talaka mkewe?”
And the Pharisees, having come near, questioned him, if it is lawful for a husband to put away a wife, tempting him,
3 Yesu akawajibu, “Mose aliwapa maagizo gani?”
and he answering said to them, 'What did Moses command you?'
4 Nao wakasema, “Mose aliagiza mume kumpatia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
and they said, 'Moses suffered to write a bill of divorce, and to put away.'
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia amri hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
And Jesus answering said to them, 'For the stiffness of your heart he wrote you this command,
6 Lakini tangu kuumbwa ulimwengu, Mungu aliumba mwanamume na mwanamke.
but from the beginning of the creation, a male and a female God did make them;
7 Hivyo mwanamume atawaacha baba yake na mama yake, ataungana na mkewe,
on this account shall a man leave his father and mother, and shall cleave unto his wife,
8 nao wawili watakuwa mwili mmoja. Kwa hiyo, wao si wawili tena bali mwili mmoja.
and they shall be — the two — for one flesh; so that they are no more two, but one flesh;
9 Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asitenganishe.”
what therefore God did join together, let not man put asunder.'
10 Walipoingia tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake walimwuliza juu ya jambo hilo.
And in the house again his disciples of the same thing questioned him,
11 Naye akawaambia, “Anayemwacha mkewe na kuoa mwingine, anazini dhidi ya mkewe.
and he saith to them, 'Whoever may put away his wife, and may marry another, doth commit adultery against her;
12 Na mwanamke anayemwacha mumewe na kuolewa na mwingine anazini.”
and if a woman may put away her husband, and is married to another, she committeth adultery.'
13 Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
And they were bringing to him children, that he might touch them, and the disciples were rebuking those bringing them,
14 Yesu alipoona hivyo, alikasirika akawaambia, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa.
and Jesus having seen, was much displeased, and he said to them, 'Suffer the children to come unto me, and forbid them not, for of such is the reign of God;
15 Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia katika Ufalme huo.”
verily I say to you, whoever may not receive the reign of God, as a child — he may not enter into it;'
16 Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki.
and having taken them in his arms, having put [his] hands upon them, he was blessing them.
17 Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja alimjia mbio, akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanyeje ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios )
And as he is going forth into the way, one having run and having kneeled to him, was questioning him, 'Good teacher, what may I do, that life age-during I may inherit?' (aiōnios )
18 Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
And Jesus said to him, 'Why me dost thou call good? no one [is] good except One — God;
19 Unazijua amri: Usizini; Usiue; Usiibe; Usitoe ushahidi wa uongo; Usidanganye; Waheshimu baba na mama yako.”
the commands thou hast known: Thou mayest not commit adultery, Thou mayest do no murder, Thou mayest not steal, Thou mayest not bear false witness, Thou mayest not defraud, Honour thy father and mother.'
20 Naye akamjibu, “Mwalimu, hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
And he answering said to him, 'Teacher, all these did I keep from my youth.'
21 Yesu akamtazama, akampenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja: nenda ukauze vitu ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.”
And Jesus having looked upon him, did love him, and said to him, 'One thing thou dost lack; go away, whatever thou hast — sell, and give to the poor, and thou shalt have treasure in heaven, and come, be following me, having taken up the cross.'
22 Aliposikia hayo, alisikitika, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.
And he — gloomy at the word — went away sorrowing, for he was having many possessions.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Jinsi gani itakavyokuwa vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
And Jesus having looked round, saith to his disciples, 'How hardly shall they who have riches enter into the reign of God!'
24 Wanafunzi walishangazwa na maneno yake. Yesu akawaambia tena, “Watoto wangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu!
And the disciples were astonished at his words, and Jesus again answering saith to them, 'Children, how hard is it to those trusting on the riches to enter into the reign of God!
25 Ni rahisi zaidi ngamia kupenya katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
It is easier for a camel through the eye of the needle to enter, than for a rich man to enter into the reign of God.'
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana wakaulizana, “Ni nani basi, atakayeweza kuokoka?”
And they were astonished beyond measure, saying unto themselves, 'And who is able to be saved?'
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo, maana kwa Mungu mambo yote huwezekana.”
And Jesus, having looked upon them, saith, 'With men it is impossible, but not with God; for all things are possible with God.'
28 Petro akamwambia, “Na sisi je? Tumeacha yote, tukakufuata!”
And Peter began to say to him, 'Lo, we left all, and we followed thee.'
29 Yesu akasema, “Kweli nawaambieni, kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au mama, au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema,
And Jesus answering said, 'Verily I say to you, there is no one who left house, or brothers, or sisters, or father, or mother, or wife, or children, or fields, for my sake, and for the good news',
30 atapokea mara mia zaidi wakati huu wa sasa nyumba, ndugu, dada, mama, watoto na mashamba pamoja na mateso; na katika wakati ujao atapokea uzima wa milele. (aiōn , aiōnios )
who may not receive an hundredfold now in this time, houses, and brothers, and sisters, and mothers, and children, and fields, with persecutions, and in the age that is coming, life age-during; (aiōn , aiōnios )
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
and many first shall be last, and the last first.'
32 Basi, walikuwa njiani kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa anawatangulia. Wanafunzi wake walijawa na hofu, na watu waliofuata waliogopa. Yesu akawachukua tena kando wale kumi na wawili, akaanza kuwaambia yale yatakayompata:
And they were in the way going up to Jerusalem, and Jesus was going before them, and they were amazed, and following they were afraid. And having again taken the twelve, he began to tell them the things about to happen to him,
33 “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe na kumkabidhi kwa watu wa mataifa.
— 'Lo, we go up to Jerusalem, and the Son of Man shall be delivered to the chief priests, and to the scribes, and they shall condemn him to death, and shall deliver him to the nations,
34 Nao watamdhihaki; watamtemea mate, watampiga mijeledi na kumwua. Na baada ya siku tatu atafufuka.”
and they shall mock him, and scourge him, and spit on him, and kill him, and the third day he shall rise again.'
35 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba.”
And there come near to him James and John, the sons of Zebedee, saying, 'Teacher, we wish that whatever we may ask for ourselves, thou mayest do for us;'
36 Yesu akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
and he said to them, 'What do ye wish me to do for you?'
37 Wakamjibu, “Uturuhusu tuketi mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wa Ufalme wako.”
and they said to him, 'Grant to us that, one on thy right hand and one on thy left, we may sit in thy glory;'
38 Yesu akawaambia, “Hamjui mnachoomba! Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa, au kubatizwa kama nitakavyobatizwa?”
and Jesus said to them, 'Ye have not known what ye ask; are ye able to drink of the cup that I drink of, and with the baptism that I am baptized with — to be baptized?'
39 Wakamjibu, “Tunaweza.” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokunywa mtakinywa kweli, na mtabatizwa kama nitakavyobatizwa.
And they said to him, 'We are able;' and Jesus said to them, 'Of the cup indeed that I drink of, ye shall drink, and with the baptism that I am baptized with, ye shall be baptized;
40 Lakini ni nani atakayeketi kulia au kushoto kwangu si wajibu wangu kupanga, bali nafasi hizo watapewa wale waliotayarishiwa.”
but to sit on my right and on my left, is not mine to give, but — to those for whom it hath been prepared.'
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, walianza kuchukizwa na Yakobo na Yohane.
And the ten having heard, began to be much displeased at James and John,
42 Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba wale wanaofikiriwa kuwa watawala wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, na wakuu hao huwamiliki watu wao.
but Jesus having called them near, saith to them, 'Ye have known that they who are considered to rule the nations do exercise lordship over them, and their great ones do exercise authority upon them;
43 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila anayetaka kuwa mkuu kati yenu, sharti awe mtumishi wenu.
but not so shall it be among you; but whoever may will to become great among you, he shall be your minister,
44 Anayetaka kuwa wa kwanza, sharti awe mtumishi wa wote.
and whoever of you may will to become first, he shall be servant of all;
45 Maana Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, ila alikuja kutumikia, na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
for even the Son of Man came not to be ministered to, but to minister, and to give his life a ransom for many.'
46 Basi, wakafika Yeriko, naye Yesu alipokuwa anatoka katika mji huo akiwa na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mwombaji aitwaye Bartimayo mwana wa Timayo alikuwa ameketi kando ya barabara.
And they come to Jericho, and as he is going forth from Jericho, with his disciples and a great multitude, a son of Timaeus — Bartimaeus the blind — was sitting beside the way begging,
47 Aliposikia kwamba ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita mahali hapo, alianza kupaaza sauti, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
and having heard that it is Jesus the Nazarene, he began to cry out, and to say, 'The Son of David — Jesus! deal kindly with me;'
48 Watu wengi walimkemea ili anyamaze, lakini yeye akazidi kupaaza sauti, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
and many were rebuking him, that he might keep silent, but the more abundantly he cried out, 'Son of David, deal kindly with me.'
49 Yesu alisimama, akasema, “Mwiteni.” Basi, wakamwita huyo kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Simama, anakuita.”
And Jesus having stood, he commanded him to be called, and they call the blind man, saying to him, 'Take courage, rise, he doth call thee;'
50 Naye akatupilia mbali vazi lake, akaruka juu, akamwendea Yesu.
and he, having cast away his garment, having risen, did come unto Jesus.
51 Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Huyo kipofu akamwambia, “Mwalimu, naomba nipate kuona.”
And answering, Jesus saith to him, 'What wilt thou I may do to thee?' and the blind man said to him, 'Rabboni, that I may see again;'
52 Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Mara huyo kipofu akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.
and Jesus said to him, 'Go, thy faith hath saved thee:' and immediately he saw again, and was following Jesus in the way.