< Marko 10 >

1 Yesu alitoka hapo akaenda mkoani Yudea na hata ng'ambo ya mto Yordani. Umati wa watu ukamwendea tena, naye akawafundisha tena kama ilivyokuwa desturi yake.
On leaving that place, Jesus went into the district of Judea on the other side of the Jordan. Crowds gathered about him again; and again, as usual, he began teaching them.
2 Basi, Mafarisayo wakamwendea, na kwa kumjaribu wakamwuliza, “Je, ni halali mtu kumpa talaka mkewe?”
Presently some Pharisees came up and, to test him, asked: “Has a husband the right to divorce his wife?”
3 Yesu akawajibu, “Mose aliwapa maagizo gani?”
“What direction did Moses give you?” replied Jesus.
4 Nao wakasema, “Mose aliagiza mume kumpatia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
“Moses,” they said, “permitted a man to ‘draw up in writing a notice of separation and divorce his wife.’”
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia amri hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
“It was owing to the hardness of your hearts,” said Jesus, “that Moses gave you this direction;
6 Lakini tangu kuumbwa ulimwengu, Mungu aliumba mwanamume na mwanamke.
but, at the beginning of the Creation, God ‘made them male and female.’
7 Hivyo mwanamume atawaacha baba yake na mama yake, ataungana na mkewe,
‘For this reason a man shall leave his father and mother,
8 nao wawili watakuwa mwili mmoja. Kwa hiyo, wao si wawili tena bali mwili mmoja.
and the man and his wife shall become one;’ so that they are no longer two, but one.
9 Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asitenganishe.”
What God himself, then, has yoked together man must not separate.”
10 Walipoingia tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake walimwuliza juu ya jambo hilo.
When they were indoors, the disciples asked him again about this,
11 Naye akawaambia, “Anayemwacha mkewe na kuoa mwingine, anazini dhidi ya mkewe.
and he said: “Any one who divorces his wife and marries another woman is guilty of adultery against his wife;
12 Na mwanamke anayemwacha mumewe na kuolewa na mwingine anazini.”
and, if the woman divorces her husband and marries another man, she is guilty of adultery.”
13 Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
Some of the people were bringing little children to Jesus, for him to touch them; but the disciples found fault with those who had brought them.
14 Yesu alipoona hivyo, alikasirika akawaambia, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa.
When, however, Jesus saw this, he was indignant. “Let the little children come to me,” he said, “do not hinder them; for it is to the childlike that the Kingdom of God belongs.
15 Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia katika Ufalme huo.”
I tell you, unless a person receives the Kingdom of God like a child, they will not enter it at all.”
16 Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki.
Then he folded the children in his arms, and, placing his hands on them, gave them his blessing.
17 Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja alimjia mbio, akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanyeje ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
As Jesus was resuming his journey, a man came running up to him, and threw himself on his knees before him. “Good Teacher,” he asked, “what must I do to gain eternal life?” (aiōnios g166)
18 Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
“Why do you call me good?” answered Jesus. “No one is good but God.
19 Unazijua amri: Usizini; Usiue; Usiibe; Usitoe ushahidi wa uongo; Usidanganye; Waheshimu baba na mama yako.”
You know the commandments — ‘Do not kill. Do not commit adultery. Do not steal. Do not say what is false about others. Do not cheat. Honour thy father and thy mother.’”
20 Naye akamjibu, “Mwalimu, hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
“Teacher,” he replied, “I have observed all these from my childhood.”
21 Yesu akamtazama, akampenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja: nenda ukauze vitu ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.”
Jesus looked at the man, and his heart went out to him, and he said: “There is still one thing wanting in you; go and sell all that you have, and give to the poor, and you shall heave wealth in Heaven; then come and follow me.”
22 Aliposikia hayo, alisikitika, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.
But the man’s face clouded at these words, and he went away distressed, for he had great possessions.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Jinsi gani itakavyokuwa vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
Then Jesus looked round, and said to his disciples: “How hard it will be for men of wealth to enter the Kingdom of God!”
24 Wanafunzi walishangazwa na maneno yake. Yesu akawaambia tena, “Watoto wangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu!
The disciples were amazed at his words. But Jesus said again: “My children, how hard a thing it is to enter the Kingdom of God!
25 Ni rahisi zaidi ngamia kupenya katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
It is easier for a camel to get through a needle’s eye, than for a rich man to enter the Kingdom of God.”
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana wakaulizana, “Ni nani basi, atakayeweza kuokoka?”
“Then who can be saved?” they exclaimed in the greatest astonishment.
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo, maana kwa Mungu mambo yote huwezekana.”
Jesus looked at them, and answered: “With men it is impossible, but not with God; for everything is possible with God.”
28 Petro akamwambia, “Na sisi je? Tumeacha yote, tukakufuata!”
“But we,” began Peter, “we left everything and have followed you.”
29 Yesu akasema, “Kweli nawaambieni, kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au mama, au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema,
“I tell you,” said Jesus, “there is no one who has left house, or brothers, or sisters, or mother, or father, or children, or land, on my account and on account of the Good News,
30 atapokea mara mia zaidi wakati huu wa sasa nyumba, ndugu, dada, mama, watoto na mashamba pamoja na mateso; na katika wakati ujao atapokea uzima wa milele. (aiōn g165, aiōnios g166)
who will not receive a hundred times as much, even now in the present — houses, and brothers, and sisters, and mothers, and children, and land — though not without persecutions, and, in the age that is coming, Immortal Life. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
But many who are first now will then be last, and the last will be first.”
32 Basi, walikuwa njiani kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa anawatangulia. Wanafunzi wake walijawa na hofu, na watu waliofuata waliogopa. Yesu akawachukua tena kando wale kumi na wawili, akaanza kuwaambia yale yatakayompata:
One day, when they were on their way, going up to Jerusalem, Jesus was walking in front of the Apostles, who were filled with misgivings; while those who were following behind were alarmed. Gathering the Twelve round him once more, Jesus began to tell them what was about to happen to him.
33 “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe na kumkabidhi kwa watu wa mataifa.
“Listen!” he said. “We are going up to Jerusalem; and there the Son of Man will be betrayed to the Chief Priests and the Teachers of the Law, and they will condemn him to death, and they will give him up to the Gentiles,
34 Nao watamdhihaki; watamtemea mate, watampiga mijeledi na kumwua. Na baada ya siku tatu atafufuka.”
who will mock him, spit upon him, and scourge him, and put him to death; and after three days he will rise again.”
35 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba.”
James and John, the two sons of Zebediah, went to Jesus, and said: “Teacher, we want you to do for us whatever we ask.”
36 Yesu akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
“What do you want me to do for you?” he asked.
37 Wakamjibu, “Uturuhusu tuketi mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wa Ufalme wako.”
“Grant us this,” they answered, “to sit, one on your right, and the other on your left, when you come in glory.”
38 Yesu akawaambia, “Hamjui mnachoomba! Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa, au kubatizwa kama nitakavyobatizwa?”
“You do not know what you are asking,” Jesus said to them. “Can you drink the cup that I am to drink? or receive the baptism that I am to receive?”
39 Wakamjibu, “Tunaweza.” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokunywa mtakinywa kweli, na mtabatizwa kama nitakavyobatizwa.
“Yes,” they answered, “we can.” “You shall indeed drink the cup that I am to drink,” Jesus said, “and receive the baptism that I am to receive,
40 Lakini ni nani atakayeketi kulia au kushoto kwangu si wajibu wangu kupanga, bali nafasi hizo watapewa wale waliotayarishiwa.”
but as to a seat at my right or at my left — that is not mine to give, but it is for those for whom it has been prepared.”
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, walianza kuchukizwa na Yakobo na Yohane.
On hearing of this, the ten others were at first very indignant about James and John.
42 Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba wale wanaofikiriwa kuwa watawala wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, na wakuu hao huwamiliki watu wao.
But Jesus called the ten to him, and said: “Those who are regarded as ruling among the Gentiles lord it over them, as you know, and their great men oppress them.
43 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila anayetaka kuwa mkuu kati yenu, sharti awe mtumishi wenu.
But among you it is not so. No, whoever wants to become great among you must be your servant,
44 Anayetaka kuwa wa kwanza, sharti awe mtumishi wa wote.
and whoever wants to take the first place among you must be the servant of all;
45 Maana Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, ila alikuja kutumikia, na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
for even the Son of Man came, not be served, but to serve, and to give his life as a ransom for many.”
46 Basi, wakafika Yeriko, naye Yesu alipokuwa anatoka katika mji huo akiwa na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mwombaji aitwaye Bartimayo mwana wa Timayo alikuwa ameketi kando ya barabara.
They came to Jericho. When Jesus was going out of the town with his disciples and a large crowd, Bartimaeus, the son of Timaeus, a blind beggar, was sitting by the road-side.
47 Aliposikia kwamba ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita mahali hapo, alianza kupaaza sauti, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Hearing that it was Jesus of Nazareth, he began to call out: “Jesus, Son of David, take pity on me.”
48 Watu wengi walimkemea ili anyamaze, lakini yeye akazidi kupaaza sauti, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Many of the people kept telling him to be quiet; but the man continued to call out all the louder: “Son of David, take pity on me.”
49 Yesu alisimama, akasema, “Mwiteni.” Basi, wakamwita huyo kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Simama, anakuita.”
Then Jesus stopped. “Call him,” he said. So they called the blind man. “Courage!” they exclaimed. “Get up; he is calling you.”
50 Naye akatupilia mbali vazi lake, akaruka juu, akamwendea Yesu.
The man threw off his cloak, sprang up, and came to Jesus.
51 Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Huyo kipofu akamwambia, “Mwalimu, naomba nipate kuona.”
“What do you want me to do for you?” said Jesus, addressing him. “Rabboni,” the blind man answered, “I want to recover my sight.”
52 Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Mara huyo kipofu akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.
“You may go,” Jesus said; “your faith has delivered you.” Immediately he recovered his sight, and began to follow Jesus along the road.

< Marko 10 >