< Marko 10 >
1 Yesu alitoka hapo akaenda mkoani Yudea na hata ng'ambo ya mto Yordani. Umati wa watu ukamwendea tena, naye akawafundisha tena kama ilivyokuwa desturi yake.
On leaving that place Jesus came into the borders of Judea, on the other side of the Jordan, Once more the people flocked about him, and again, as usual, he began teaching them.
2 Basi, Mafarisayo wakamwendea, na kwa kumjaribu wakamwuliza, “Je, ni halali mtu kumpa talaka mkewe?”
Presently some Pharisees came up and tested him, by asking if it was lawful for a man to divorce his wife.
3 Yesu akawajibu, “Mose aliwapa maagizo gani?”
"What did Moses command you?" he replied,
4 Nao wakasema, “Mose aliagiza mume kumpatia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
"Moses," said they, "permitted a man to draw up a bill of separation and divorce her."
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia amri hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
But Jesus said to them. "Moses gave you that command because of the hardness of your hearts;
6 Lakini tangu kuumbwa ulimwengu, Mungu aliumba mwanamume na mwanamke.
but from the beginning of the creation God made them male and female.
7 Hivyo mwanamume atawaacha baba yake na mama yake, ataungana na mkewe,
"For this cause a man shall leave his father and his mother, and shall cleave to his wife; and the two shall become one flesh;
8 nao wawili watakuwa mwili mmoja. Kwa hiyo, wao si wawili tena bali mwili mmoja.
so that they are no more two, but one flesh.
9 Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asitenganishe.”
What therefore God has joined together, let not man put asunder."
10 Walipoingia tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake walimwuliza juu ya jambo hilo.
When indoors the disciples began to question Jesus again about this, and he said.
11 Naye akawaambia, “Anayemwacha mkewe na kuoa mwingine, anazini dhidi ya mkewe.
"Any man who divorces his wife and marries another woman commits adultery against her;
12 Na mwanamke anayemwacha mumewe na kuolewa na mwingine anazini.”
and if she divorces her husband and marries another man, she commits adultery."
13 Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
Now people were bringing little children to Jesus for him to touch them; but the disciples rebuked them.
14 Yesu alipoona hivyo, alikasirika akawaambia, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa.
Jesus was indignant when he saw it, and said. "Let the little children come to me. Do not hinder them; for the kingdom of God belongs to such.
15 Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia katika Ufalme huo.”
I tell you true that unless a man receives the kingdom of God as a little child, he shall not even enter it."
16 Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki.
Then he took them in his arms, and laid his hand upon them in blessing.
17 Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja alimjia mbio, akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanyeje ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios )
As he started to go forth into the road, a man came running up to him, and knelt down before him. "Good Teacher," he asked, "what must I do to inherit eternal life?" (aiōnios )
18 Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
Jesus said to him. "Why do you call me ‘good’? No one is good save one, God himself.
19 Unazijua amri: Usizini; Usiue; Usiibe; Usitoe ushahidi wa uongo; Usidanganye; Waheshimu baba na mama yako.”
You know the commandments. Do not murder, do not commit adultery, do not steal, do not bear false witness, do not cheat, honor your father and mother."
20 Naye akamjibu, “Mwalimu, hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
"Teacher," he answered, "I have observed all these from my youth."
21 Yesu akamtazama, akampenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja: nenda ukauze vitu ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.”
Jesus loved him as he looked at him, and said. "One thing you lack. Go, sell all you have and give to the poor; and you shall have wealth in heaven; and come, follow me."
22 Aliposikia hayo, alisikitika, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.
But his face fell at these words, and he went away saddened, for he was one who had great wealth.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Jinsi gani itakavyokuwa vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
Then Jesus looked round on his disciples and said, "How hard it is for those who have wealth to enter into the kingdom of God!"
24 Wanafunzi walishangazwa na maneno yake. Yesu akawaambia tena, “Watoto wangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu!
The disciples were amazed at his words. Jesus looked around and said again to them.
25 Ni rahisi zaidi ngamia kupenya katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
"My sons, how hard it is for those who trust in money to enter the kingdom of God. It is easier for a camel to get through the eye of a needle, than for a rich man to enter the kingdom of heaven."
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana wakaulizana, “Ni nani basi, atakayeweza kuokoka?”
"Then who can be saved?" they said to themselves astonished beyond measure.
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo, maana kwa Mungu mambo yote huwezekana.”
When he had looked at them, Jesus said, "With men it is impossible, but not with God, for all things are possible with God."
28 Petro akamwambia, “Na sisi je? Tumeacha yote, tukakufuata!”
"But we," Peter began to say, "we have left our all and have followed you."
29 Yesu akasema, “Kweli nawaambieni, kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au mama, au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema,
"I tell you solemnly," said Jesus, "that there is no man who has left house, or brothers, or sisters, or mother, or father, or children, or lands, for my sake and the gospel’s,
30 atapokea mara mia zaidi wakati huu wa sasa nyumba, ndugu, dada, mama, watoto na mashamba pamoja na mateso; na katika wakati ujao atapokea uzima wa milele. (aiōn , aiōnios )
but shall receive a hundred times as much, now in this present world, houses, brothers, sisters, mothers, children, lands-and persecutions with them - and in the world to come eternal life. (aiōn , aiōnios )
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
But many who are first shall be last, and the last, first."
32 Basi, walikuwa njiani kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa anawatangulia. Wanafunzi wake walijawa na hofu, na watu waliofuata waliogopa. Yesu akawachukua tena kando wale kumi na wawili, akaanza kuwaambia yale yatakayompata:
They were still on the road going up to Jerusalem, and Jesus led the way; and they were amazed, and some, although they followed, were afraid. Then once more he took the Twelve, and began to tell them what was about to befall him.
33 “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe na kumkabidhi kwa watu wa mataifa.
"See," said he, "we are going up to Jerusalem and the Son of man will be betrayed to the high priests and the Scribes. They will condemn him to death, and will hand him over to the Gentiles,
34 Nao watamdhihaki; watamtemea mate, watampiga mijeledi na kumwua. Na baada ya siku tatu atafufuka.”
who will mock him, spit upon him, flog him, and put him to death; and after three days he will rise again."
35 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba.”
Presently there came up to him Jamesand John, the sons of Zebedee, and said, "Teacher, we wish you would do for us whatever we ask you."
36 Yesu akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
"What is it you want me to do for you?" said he.
37 Wakamjibu, “Uturuhusu tuketi mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wa Ufalme wako.”
They answered, "Allow us to sit, one at your right hand, and the other at your left hand, in your glory."
38 Yesu akawaambia, “Hamjui mnachoomba! Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa, au kubatizwa kama nitakavyobatizwa?”
"You know not what you are asking," said Jesus. "Can you drink the cup that I drink, or be baptized with the baptism that I am baptized with?"
39 Wakamjibu, “Tunaweza.” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokunywa mtakinywa kweli, na mtabatizwa kama nitakavyobatizwa.
They answered him, "We can." "You shall indeed drink the cup that I drink, and with the baptism that I am baptized with shall you be baptized,
40 Lakini ni nani atakayeketi kulia au kushoto kwangu si wajibu wangu kupanga, bali nafasi hizo watapewa wale waliotayarishiwa.”
but a seat upon my right hand or my left is not mine to grant, but it is for those for whom it has been reserved."
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, walianza kuchukizwa na Yakobo na Yohane.
When they heard this the ten began to be indignant at Jamesand John, so Jesus called them to him and said.
42 Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba wale wanaofikiriwa kuwa watawala wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, na wakuu hao huwamiliki watu wao.
"You know that those who are regarded as rulers among the Gentiles lord it over them, and their great ones make them feel their authority.
43 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila anayetaka kuwa mkuu kati yenu, sharti awe mtumishi wenu.
Not so shall it be among you. On the contrary whoever would become great among you shall be your servant;
44 Anayetaka kuwa wa kwanza, sharti awe mtumishi wa wote.
and whoever among you would be first, shall be slave of all,
45 Maana Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, ila alikuja kutumikia, na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
and justly, for even the Son of man came not to be served, but to serve, and to give his life, a ransom for many."
46 Basi, wakafika Yeriko, naye Yesu alipokuwa anatoka katika mji huo akiwa na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mwombaji aitwaye Bartimayo mwana wa Timayo alikuwa ameketi kando ya barabara.
Then they reached Jericho; and as he was leaving Jericho with his disciples and a great crowd, Bartimeus, the son of Timaeus, a blind beggar, was sitting beside the road.
47 Aliposikia kwamba ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita mahali hapo, alianza kupaaza sauti, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Hearing that it was Jesus of Nazareth, he began shouting and saying, "Jesus, thou son of David, have mercy on me!"
48 Watu wengi walimkemea ili anyamaze, lakini yeye akazidi kupaaza sauti, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
and many kept rebuking him and telling him to be quiet, but he only shouted much louder, "Son of David, have mercy on me!"
49 Yesu alisimama, akasema, “Mwiteni.” Basi, wakamwita huyo kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Simama, anakuita.”
Then Jesus stood still, saying, "Call him." So they called the blind man, and said, "Courage, rise, he is calling you."
50 Naye akatupilia mbali vazi lake, akaruka juu, akamwendea Yesu.
The man threw off his cloak, sprang to his feet, and came to Jesus.
51 Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Huyo kipofu akamwambia, “Mwalimu, naomba nipate kuona.”
"What do you want me to do?" said Jesus, addressing him. And the blind man answered, "O Rabboni, that I might receive my sight!"
52 Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Mara huyo kipofu akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.
"Go," said Jesus, "your own faith has saved you," and immediately he received his sight, and began to follow Jesus along the road.