< Marko 10 >

1 Yesu alitoka hapo akaenda mkoani Yudea na hata ng'ambo ya mto Yordani. Umati wa watu ukamwendea tena, naye akawafundisha tena kama ilivyokuwa desturi yake.
Then He set out from there and came into the borders of Judea, by way of the other side of the Jordan. Again, crowds gathered to Him, and as was His custom, He began to teach them once more.
2 Basi, Mafarisayo wakamwendea, na kwa kumjaribu wakamwuliza, “Je, ni halali mtu kumpa talaka mkewe?”
Then some Pharisees approached to test Him and asked Him, “Is it lawful for a man to divorce a wife?”
3 Yesu akawajibu, “Mose aliwapa maagizo gani?”
So in answer He said to them, “What did Moses command you?”
4 Nao wakasema, “Mose aliagiza mume kumpatia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
They said, “Moses permitted one to write a certificate of divorce and to put away.”
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia amri hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
Jesus answered and said to them: “It was due to your hardness of heart that he wrote you this precept.
6 Lakini tangu kuumbwa ulimwengu, Mungu aliumba mwanamume na mwanamke.
But from the beginning of creation, God made them a male and a female.
7 Hivyo mwanamume atawaacha baba yake na mama yake, ataungana na mkewe,
‘For this reason a man shall leave his father and mother and be joined to his wife,
8 nao wawili watakuwa mwili mmoja. Kwa hiyo, wao si wawili tena bali mwili mmoja.
and the two will be turned into one flesh.’ So then, they are no longer two but one flesh.
9 Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asitenganishe.”
Therefore what God has joined together, let man not separate.”
10 Walipoingia tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake walimwuliza juu ya jambo hilo.
When they were in the house again, His disciples asked Him about the same subject.
11 Naye akawaambia, “Anayemwacha mkewe na kuoa mwingine, anazini dhidi ya mkewe.
So He said to them, “Whoever divorces his wife and marries another commits adultery against her;
12 Na mwanamke anayemwacha mumewe na kuolewa na mwingine anazini.”
and if a woman divorces her husband and gets married to another, she commits adultery.”
13 Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
People started bringing little children to Him, that He might touch them; so the disciples started rebuking those doing the bringing.
14 Yesu alipoona hivyo, alikasirika akawaambia, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa.
But when Jesus saw it He was indignant and said to them: “Let the little children come to me; do not hinder them, because the Kingdom of God is made up of such.
15 Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia katika Ufalme huo.”
I tell you assuredly, whoever does not receive the Kingdom of God like a little child does will certainly not enter it.”
16 Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki.
And taking them in His arms and laying His hands on them, He blessed them.
17 Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja alimjia mbio, akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanyeje ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
As Jesus set out on the road, someone came running up, knelt before Him and asked Him, “Good Teacher, what must I do that I may inherit eternal life?” (aiōnios g166)
18 Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
So Jesus said to Him: “Why do you call me ‘good’? No one is good except one—God.
19 Unazijua amri: Usizini; Usiue; Usiibe; Usitoe ushahidi wa uongo; Usidanganye; Waheshimu baba na mama yako.”
You know the commandments: ‘Do not commit adultery,’ ‘Do not murder,’ ‘Do not steal,’ ‘Do not give false testimony,’ ‘Do not defraud,’ ‘Honor your father and mother.’”
20 Naye akamjibu, “Mwalimu, hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
In answer he said to Him, “Teacher, I have kept all these since I was young.”
21 Yesu akamtazama, akampenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja: nenda ukauze vitu ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.”
Then Jesus, looking at him, loved him, and said to him: “One thing you lack; go, sell whatever you have and give to the poor, and you will have treasure in heaven. Then come, take up the cross, and follow me.”
22 Aliposikia hayo, alisikitika, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.
But he was dismayed at the suggestion and went away sorrowing, because he had many possessions.
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Jinsi gani itakavyokuwa vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
Then Jesus looked around and said to His disciples, “How hard it is for those who have riches to get into the Kingdom of God!”
24 Wanafunzi walishangazwa na maneno yake. Yesu akawaambia tena, “Watoto wangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu!
But the disciples were astounded at His words. So Jesus tried again and said to them: “Children, how hard it is for those who trust in riches to enter the Kingdom of God.
25 Ni rahisi zaidi ngamia kupenya katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
It is actually easier for a camel to go through a needle's eye than for a rich man to enter the Kingdom of God.”
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana wakaulizana, “Ni nani basi, atakayeweza kuokoka?”
Then they were totally astonished, saying to each other, “Who then can be saved?”
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo, maana kwa Mungu mambo yote huwezekana.”
But Jesus looked at them and said, “With men it is impossible, but not with God; because all things are possible with God.”
28 Petro akamwambia, “Na sisi je? Tumeacha yote, tukakufuata!”
Then Peter began to say to Him, “So, we have left all and followed you.”
29 Yesu akasema, “Kweli nawaambieni, kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au mama, au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema,
In answer Jesus said: “I tell you assuredly, there is no one who has left house or brothers or sisters or father or mother or wife or children or fields, for my sake and for that of the Gospel,
30 atapokea mara mia zaidi wakati huu wa sasa nyumba, ndugu, dada, mama, watoto na mashamba pamoja na mateso; na katika wakati ujao atapokea uzima wa milele. (aiōn g165, aiōnios g166)
who will not receive a hundred times more, now in this time—houses and brothers and sisters and father and mother and children and fields (with persecutions)—and in the age to come, eternal life. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
But many first will be last, and last first.”
32 Basi, walikuwa njiani kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa anawatangulia. Wanafunzi wake walijawa na hofu, na watu waliofuata waliogopa. Yesu akawachukua tena kando wale kumi na wawili, akaanza kuwaambia yale yatakayompata:
Now they were on the road going up to Jerusalem, and Jesus was going ahead of them; this surprised them, and as they followed they started to be afraid. Then He took the twelve aside again and began to tell them the things that were about to happen to Him:
33 “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe na kumkabidhi kwa watu wa mataifa.
“Take note, we are going up to Jerusalem, and the Son of the Man will be betrayed to the chief priests and the scribes; and they will condemn Him to death and deliver Him over to the Gentiles;
34 Nao watamdhihaki; watamtemea mate, watampiga mijeledi na kumwua. Na baada ya siku tatu atafufuka.”
and they will mock Him, and scourge Him, and spit on Him, and kill Him. And on the third day He will rise again.”
35 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba.”
Then James and John, the sons of Zebedee, approached Him and said, “Teacher, we want you to do for us whatever we may ask.”
36 Yesu akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
So He said to them, “What do you want me to do for you?”
37 Wakamjibu, “Uturuhusu tuketi mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wa Ufalme wako.”
They said to Him, “Grant to us that we may sit, one at your right and one at your left, in your glory.”
38 Yesu akawaambia, “Hamjui mnachoomba! Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa, au kubatizwa kama nitakavyobatizwa?”
But Jesus said to them: “You do not know what you are asking. Are you able to drink the cup that I drink, and to be baptized with the baptism that I am baptized with?”
39 Wakamjibu, “Tunaweza.” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokunywa mtakinywa kweli, na mtabatizwa kama nitakavyobatizwa.
They said to Him, “We are able.” So Jesus said to them: “You will indeed drink the cup that I drink, and you will be baptized with the baptism that I am baptized with;
40 Lakini ni nani atakayeketi kulia au kushoto kwangu si wajibu wangu kupanga, bali nafasi hizo watapewa wale waliotayarishiwa.”
but to sit at my right and at my left is not mine to grant, but is for whom it has been prepared.”
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, walianza kuchukizwa na Yakobo na Yohane.
Well when the ten heard it they began to be indignant with James and John.
42 Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba wale wanaofikiriwa kuwa watawala wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, na wakuu hao huwamiliki watu wao.
But Jesus summoned them and said to them: “You know that those who are regarded as rulers of the Gentiles lord it over them, and their great ones exercise authority over them.
43 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila anayetaka kuwa mkuu kati yenu, sharti awe mtumishi wenu.
But it must not be so among you, but whoever desires to become great among you must be your servant,
44 Anayetaka kuwa wa kwanza, sharti awe mtumishi wa wote.
and whoever desires to be your number one must be slave of all.
45 Maana Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, ila alikuja kutumikia, na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
For even the Son of the Man did not come to be served, but to serve, and to give His life a ransom for many.”
46 Basi, wakafika Yeriko, naye Yesu alipokuwa anatoka katika mji huo akiwa na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mwombaji aitwaye Bartimayo mwana wa Timayo alikuwa ameketi kando ya barabara.
They came to Jericho. Then as He was going out from Jericho, with His disciples and a large crowd, the blind Bartimaeus (son of Timaeus) was sitting by the roadside begging.
47 Aliposikia kwamba ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita mahali hapo, alianza kupaaza sauti, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
And when he heard that it was Jesus the Natsorean, he began to call out and say, “O Son of David, Jesus, have mercy on me!”
48 Watu wengi walimkemea ili anyamaze, lakini yeye akazidi kupaaza sauti, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
Many started telling him to shut up, but he started calling out even louder, “Son of David, have mercy on me!”
49 Yesu alisimama, akasema, “Mwiteni.” Basi, wakamwita huyo kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Simama, anakuita.”
So Jesus stood still and said to call him. Then they called the blind man, saying to him: “Courage! Get up! He's calling you!”
50 Naye akatupilia mbali vazi lake, akaruka juu, akamwendea Yesu.
Tossing off his cloak, he got up and went to Jesus.
51 Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Huyo kipofu akamwambia, “Mwalimu, naomba nipate kuona.”
Jesus reacted by saying to him, “What do you want me to do for you?” The blind man said to Him, “Rabouni, that I may see again!”
52 Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Mara huyo kipofu akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.
So Jesus said to him, “Go; your faith has healed you.” And immediately he could see, and followed Jesus on the road.

< Marko 10 >