< Marko 10 >

1 Yesu alitoka hapo akaenda mkoani Yudea na hata ng'ambo ya mto Yordani. Umati wa watu ukamwendea tena, naye akawafundisha tena kama ilivyokuwa desturi yake.
耶稣从那里起身,来到犹太的境界并约旦河外。众人又聚集到他那里,他又照常教训他们。
2 Basi, Mafarisayo wakamwendea, na kwa kumjaribu wakamwuliza, “Je, ni halali mtu kumpa talaka mkewe?”
有法利赛人来问他说:“人休妻可以不可以?”意思要试探他。
3 Yesu akawajibu, “Mose aliwapa maagizo gani?”
耶稣回答说:“摩西吩咐你们的是什么?”
4 Nao wakasema, “Mose aliagiza mume kumpatia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
他们说:“摩西许人写了休书便可以休妻。”
5 Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia amri hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
耶稣说:“摩西因为你们的心硬,所以写这条例给你们;
6 Lakini tangu kuumbwa ulimwengu, Mungu aliumba mwanamume na mwanamke.
但从起初创造的时候, 神造人是造男造女。
7 Hivyo mwanamume atawaacha baba yake na mama yake, ataungana na mkewe,
因此,人要离开父母,与妻子连合,二人成为一体。
8 nao wawili watakuwa mwili mmoja. Kwa hiyo, wao si wawili tena bali mwili mmoja.
既然如此,夫妻不再是两个人,乃是一体的了。
9 Basi, alichounganisha Mungu, binadamu asitenganishe.”
所以, 神配合的,人不可分开。”
10 Walipoingia tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake walimwuliza juu ya jambo hilo.
到了屋里,门徒就问他这事。
11 Naye akawaambia, “Anayemwacha mkewe na kuoa mwingine, anazini dhidi ya mkewe.
耶稣对他们说:“凡休妻另娶的,就是犯奸淫,辜负他的妻子;
12 Na mwanamke anayemwacha mumewe na kuolewa na mwingine anazini.”
妻子若离弃丈夫另嫁,也是犯奸淫了。”
13 Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
有人带着小孩子来见耶稣,要耶稣摸他们,门徒便责备那些人。
14 Yesu alipoona hivyo, alikasirika akawaambia, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa.
耶稣看见就恼怒,对门徒说:“让小孩子到我这里来,不要禁止他们;因为在 神国的,正是这样的人。
15 Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia katika Ufalme huo.”
我实在告诉你们,凡要承受 神国的,若不像小孩子,断不能进去。”
16 Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki.
于是抱着小孩子,给他们按手,为他们祝福。
17 Yesu alipoanza tena safari yake, mtu mmoja alimjia mbio, akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu mwema, nifanyeje ili niupate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
耶稣出来行路的时候,有一个人跑来,跪在他面前,问他说:“良善的夫子,我当做什么事才可以承受永生?” (aiōnios g166)
18 Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
耶稣对他说:“你为什么称我是良善的?除了 神一位之外,再没有良善的。
19 Unazijua amri: Usizini; Usiue; Usiibe; Usitoe ushahidi wa uongo; Usidanganye; Waheshimu baba na mama yako.”
诫命你是晓得的:不可杀人;不可奸淫;不可偷盗;不可作假见证;不可亏负人;当孝敬父母。”
20 Naye akamjibu, “Mwalimu, hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
他对耶稣说:“夫子,这一切我从小都遵守了。”
21 Yesu akamtazama, akampenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja: nenda ukauze vitu ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.”
耶稣看着他,就爱他,对他说:“你还缺少一件:去变卖你所有的,分给穷人,就必有财宝在天上;你还要来跟从我。”
22 Aliposikia hayo, alisikitika, akaenda zake akiwa na huzuni, kwa maana alikuwa na mali nyingi.
他听见这话,脸上就变了色,忧忧愁愁地走了,因为他的产业很多。
23 Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Jinsi gani itakavyokuwa vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
耶稣周围一看,对门徒说:“有钱财的人进 神的国是何等地难哪!”
24 Wanafunzi walishangazwa na maneno yake. Yesu akawaambia tena, “Watoto wangu, ni vigumu sana kuingia katika Ufalme wa Mungu!
门徒希奇他的话。耶稣又对他们说:“小子,倚靠钱财的人进 神的国是何等地难哪!
25 Ni rahisi zaidi ngamia kupenya katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
骆驼穿过针的眼,比财主进 神的国还容易呢。”
26 Wanafunzi wake wakashangaa sana wakaulizana, “Ni nani basi, atakayeweza kuokoka?”
门徒就分外希奇,对他说:“这样谁能得救呢?”
27 Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini kwa Mungu si hivyo, maana kwa Mungu mambo yote huwezekana.”
耶稣看着他们,说:“在人是不能,在 神却不然,因为 神凡事都能。”
28 Petro akamwambia, “Na sisi je? Tumeacha yote, tukakufuata!”
彼得就对他说:“看哪,我们已经撇下所有的跟从你了。”
29 Yesu akasema, “Kweli nawaambieni, kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu, au dada, au mama, au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Habari Njema,
耶稣说:“我实在告诉你们,人为我和福音撇下房屋,或是弟兄、姊妹、父母、儿女、田地,
30 atapokea mara mia zaidi wakati huu wa sasa nyumba, ndugu, dada, mama, watoto na mashamba pamoja na mateso; na katika wakati ujao atapokea uzima wa milele. (aiōn g165, aiōnios g166)
没有不在今世得百倍的,就是房屋、弟兄、姊妹、母亲、儿女、田地,并且要受逼迫,在来世必得永生。 (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
然而,有许多在前的,将要在后,在后的,将要在前。”
32 Basi, walikuwa njiani kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa anawatangulia. Wanafunzi wake walijawa na hofu, na watu waliofuata waliogopa. Yesu akawachukua tena kando wale kumi na wawili, akaanza kuwaambia yale yatakayompata:
他们行路上耶路撒冷去。耶稣在前头走,门徒就希奇,跟从的人也害怕。耶稣又叫过十二个门徒来,把自己将要遭遇的事告诉他们说:
33 “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu, na huko Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa makuhani wakuu na walimu wa Sheria, nao watamhukumu auawe na kumkabidhi kwa watu wa mataifa.
“看哪,我们上耶路撒冷去,人子将要被交给祭司长和文士,他们要定他死罪,交给外邦人。
34 Nao watamdhihaki; watamtemea mate, watampiga mijeledi na kumwua. Na baada ya siku tatu atafufuka.”
他们要戏弄他,吐唾沫在他脸上,鞭打他,杀害他。过了三天,他要复活。”
35 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba.”
西庇太的儿子雅各、约翰进前来,对耶稣说:“夫子,我们无论求你什么,愿你给我们做。”
36 Yesu akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
耶稣说:“要我给你们做什么?”
37 Wakamjibu, “Uturuhusu tuketi mmoja upande wako wa kulia na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wa Ufalme wako.”
他们说:“赐我们在你的荣耀里,一个坐在你右边,一个坐在你左边。”
38 Yesu akawaambia, “Hamjui mnachoomba! Je, mnaweza kunywa kikombe nitakachokunywa, au kubatizwa kama nitakavyobatizwa?”
耶稣说:“你们不知道所求的是什么。我所喝的杯,你们能喝吗?我所受的洗,你们能受吗?”
39 Wakamjibu, “Tunaweza.” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokunywa mtakinywa kweli, na mtabatizwa kama nitakavyobatizwa.
他们说:“我们能。”耶稣说:“我所喝的杯,你们也要喝;我所受的洗,你们也要受;
40 Lakini ni nani atakayeketi kulia au kushoto kwangu si wajibu wangu kupanga, bali nafasi hizo watapewa wale waliotayarishiwa.”
只是坐在我的左右,不是我可以赐的,乃是为谁预备的,就赐给谁。”
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, walianza kuchukizwa na Yakobo na Yohane.
那十个门徒听见,就恼怒雅各、约翰。
42 Yesu akawaita, akawaambia, “Mnajua kwamba wale wanaofikiriwa kuwa watawala wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, na wakuu hao huwamiliki watu wao.
耶稣叫他们来,对他们说:“你们知道,外邦人有尊为君王的,治理他们,有大臣操权管束他们。
43 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila anayetaka kuwa mkuu kati yenu, sharti awe mtumishi wenu.
只是在你们中间,不是这样。你们中间,谁愿为大,就必作你们的用人;
44 Anayetaka kuwa wa kwanza, sharti awe mtumishi wa wote.
在你们中间,谁愿为首,就必作众人的仆人。
45 Maana Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, ila alikuja kutumikia, na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi.”
因为人子来,并不是要受人的服事,乃是要服事人,并且要舍命作多人的赎价。”
46 Basi, wakafika Yeriko, naye Yesu alipokuwa anatoka katika mji huo akiwa na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mwombaji aitwaye Bartimayo mwana wa Timayo alikuwa ameketi kando ya barabara.
到了耶利哥;耶稣同门徒并许多人出耶利哥的时候,有一个讨饭的瞎子,是底买的儿子巴底买,坐在路旁。
47 Aliposikia kwamba ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita mahali hapo, alianza kupaaza sauti, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
他听见是拿撒勒的耶稣,就喊着说:“大卫的子孙耶稣啊!可怜我吧!”
48 Watu wengi walimkemea ili anyamaze, lakini yeye akazidi kupaaza sauti, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
有许多人责备他,不许他作声。他却越发大声喊着说:“大卫的子孙哪,可怜我吧!”
49 Yesu alisimama, akasema, “Mwiteni.” Basi, wakamwita huyo kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Simama, anakuita.”
耶稣就站住,说:“叫过他来。”他们就叫那瞎子,对他说:“放心,起来!他叫你啦。”
50 Naye akatupilia mbali vazi lake, akaruka juu, akamwendea Yesu.
瞎子就丢下衣服,跳起来,走到耶稣那里。
51 Yesu akamwuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Huyo kipofu akamwambia, “Mwalimu, naomba nipate kuona.”
耶稣说:“要我为你做什么?”瞎子说:“拉波尼,我要能看见。”
52 Yesu akamwambia, “Nenda, imani yako imekuponya.” Mara huyo kipofu akaweza kuona, akamfuata Yesu njiani.
耶稣说:“你去吧!你的信救了你了。”瞎子立刻看见了,就在路上跟随耶稣。

< Marko 10 >