< Marko 1 >

1 Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
The beginning of the Gospel of Jesus Christ, the Son of God.
2 Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
As it has been written by the prophet Isaiah: “Behold, I send my Angel before your face, who shall prepare your way before you.
3 Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
The voice of one crying out in the desert: Prepare the way of the Lord; make straight his paths.”
4 Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
John was in the desert, baptizing and preaching a baptism of repentance, as a remission of sins.
5 Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
And there went out to him all the region of Judea and all those of Jerusalem, and they were baptized by him in the river Jordan, confessing their sins.
6 Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
And John was clothed with camel’s hair and with a leather belt around his waist. And he ate locusts and wild honey.
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
And he preached, saying: “One stronger than me comes after me. I am not worthy to reach down and loosen the laces of his shoes.
8 Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I have baptized you with water. Yet truly, he will baptize you with the Holy Spirit.”
9 Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
And it happened that, in those days, Jesus arrived from Nazareth of Galilee. And he was baptized by John in the Jordan.
10 Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
And immediately, upon ascending from the water, he saw the heavens opened and the Spirit, like a dove, descending, and remaining with him.
11 Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
And there was a voice from heaven: “You are my beloved Son; in you I am well pleased.”
12 Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
And immediately the Spirit prompted him into the desert.
13 akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
And he was in the desert for forty days and forty nights. And he was tempted by Satan. And he was with the wild animals, and the Angels ministered to him.
14 Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
Then, after John was handed over, Jesus went into Galilee, preaching the Gospel of the kingdom of God,
15 “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
and saying: “For the time has been fulfilled and the kingdom of God has drawn near. Repent and believe in the Gospel.”
16 Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
And passing by the shore of the Sea of Galilee, he saw Simon and his brother Andrew, casting nets into the sea, for they were fishermen.
17 Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
And Jesus said to them, “Come after me, and I will make you fishers of men.”
18 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
And at once abandoning their nets, they followed him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
And continuing on a little ways from there, he saw James of Zebedee and his brother John, and they were mending their nets in a boat.
20 Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
And immediately he called them. And leaving behind their father Zebedee in the boat with his hired hands, they followed him.
21 Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
And they entered into Capernaum. And entering into the synagogue promptly on the Sabbaths, he taught them.
22 Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
And they were astonished over his doctrine. For he was teaching them as one who has authority, and not like the scribes.
23 Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
And in their synagogue, there was a man with an unclean spirit; and he cried out,
24 akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
saying: “What are we to you, Jesus of Nazareth? Have you come to destroy us? I know who you are: the Holy One of God.”
25 Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
And Jesus admonished him, saying, “Be silent, and depart from the man.”
26 Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
And the unclean spirit, convulsing him and crying out with a loud voice, departed from him.
27 Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
And they were all so amazed that they inquired among themselves, saying: “What is this? And what is this new doctrine? For with authority he commands even the unclean spirits, and they obey him.”
28 Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
And his fame went out quickly, throughout the entire region of Galilee.
29 Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
And soon after departing from the synagogue, they went into the house of Simon and Andrew, with James and John.
30 Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
But the mother-in-law of Simon lay ill with a fever. And at once they told him about her.
31 Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
And drawing near to her, he raised her up, taking her by the hand. And immediately the fever left her, and she ministered to them.
32 Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
Then, when evening arrived, after the sun had set, they brought to him all who had maladies and those who had demons.
33 Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
And the entire city was gathered together at the door.
34 Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
And he healed many who were troubled with various illnesses. And he cast out many demons, but he would not permit them to speak, because they knew him.
35 Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
And rising up very early, departing, he went out to a deserted place, and there he prayed.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
And Simon, and those who were with him, followed after him.
37 Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
And when they had found him, they said to him, “For everyone is seeking you.”
38 Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
And he said to them: “Let us go into the neighboring towns and cities, so that I may preach there also. Indeed, it was for this reason that I came.”
39 Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
And he was preaching in their synagogues and throughout all of Galilee, and casting out demons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
And a leper came to him, begging him. And kneeling down, he said to him, “If you are willing, you are able to cleanse me.”
41 Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
Then Jesus, taking pity on him, reached out his hand. And touching him, he said to him: “I am willing. Be cleansed.”
42 Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
And after he had spoken, immediately the leprosy departed from him, and he was cleansed.
43 Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
And he admonished him, and he promptly sent him away.
44 “Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
And he said to him: “See to it that you tell no one. But go and show yourself to the high priest, and offer for your cleansing that which Moses instructed, as a testimony for them.”
45 Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.
But having departed, he began to preach and to disseminate the word, so that he was no longer able to openly enter a city, but had to remain outside, in deserted places. And they were gathered to him from every direction.

< Marko 1 >