< Marko 1 >
1 Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
This is the beginning of the gospel of Jesus Christ, the Son of God.
2 Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
As it is written in Isaiah the prophet: “Behold, I will send My messenger ahead of You, who will prepare Your way.”
3 Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
“A voice of one calling in the wilderness, ‘Prepare the way for the Lord, make straight paths for Him.’”
4 Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
John the Baptist appeared in the wilderness, preaching a baptism of repentance for the forgiveness of sins.
5 Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
People went out to him from all of Jerusalem and the countryside of Judea. Confessing their sins, they were baptized by him in the Jordan River.
6 Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
John was clothed in camel’s hair, with a leather belt around his waist. His food was locusts and wild honey.
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
And he began to proclaim: “After me will come One more powerful than I, the straps of whose sandals I am not worthy to stoop down and untie.
8 Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I baptize you with water, but He will baptize you with the Holy Spirit.”
9 Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
In those days Jesus came from Nazareth in Galilee and was baptized by John in the Jordan.
10 Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
As soon as Jesus came up out of the water, He saw the heavens breaking open and the Spirit descending on Him like a dove.
11 Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
And a voice came from heaven: “You are My beloved Son; in You I am well pleased.”
12 Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
At once the Spirit drove Jesus into the wilderness,
13 akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
and He was there for forty days, being tempted by Satan. He was with the wild animals, and the angels ministered to Him.
14 Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
After the arrest of John, Jesus went into Galilee and proclaimed the gospel of God.
15 “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
“The time is fulfilled,” He said, “and the kingdom of God is near. Repent and believe in the gospel!”
16 Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
As Jesus was walking beside the Sea of Galilee, He saw Simon and his brother Andrew. They were casting a net into the sea, for they were fishermen.
17 Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
“Come, follow Me,” Jesus said, “and I will make you fishers of men.”
18 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
And at once they left their nets and followed Him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
Going on a little farther, He saw James son of Zebedee and his brother John. They were in a boat, mending their nets.
20 Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
Immediately Jesus called them, and they left their father Zebedee in the boat with the hired men and followed Him.
21 Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
Then Jesus and His companions went to Capernaum, and right away Jesus entered the synagogue on the Sabbath and began to teach.
22 Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
The people were astonished at His teaching, because He taught as one who had authority, and not as the scribes.
23 Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
Suddenly a man with an unclean spirit cried out in the synagogue:
24 akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
“What do You want with us, Jesus of Nazareth? Have You come to destroy us? I know who You are—the Holy One of God!”
25 Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
But Jesus rebuked the spirit. “Be silent!” He said. “Come out of him!”
26 Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
At this, the unclean spirit threw the man into convulsions and came out with a loud shriek.
27 Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
All the people were amazed and began to ask one another, “What is this? A new teaching with authority! He commands even the unclean spirits, and they obey Him!”
28 Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
And the news about Jesus spread quickly through the whole region of Galilee.
29 Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
As soon as Jesus and His companions had left the synagogue, they went with James and John to the home of Simon and Andrew.
30 Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
Simon’s mother-in-law was sick in bed with a fever, and they promptly told Jesus about her.
31 Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
So He went to her, took her by the hand, and helped her up. The fever left her, and she began to serve them.
32 Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
That evening, after sunset, people brought to Jesus all who were sick and demon-possessed,
33 Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
and the whole town gathered at the door.
34 Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
And He healed many who were ill with various diseases and drove out many demons. But He would not allow the demons to speak, because they knew who He was.
35 Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
Early in the morning, while it was still dark, Jesus got up and slipped out to a solitary place to pray.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
Simon and his companions went to look for Him,
37 Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
and when they found Him, they said, “Everyone is looking for You!”
38 Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
But Jesus answered, “Let us go on to the neighboring towns so I can preach there as well, for that is why I have come.”
39 Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
So He went throughout Galilee, preaching in their synagogues and driving out demons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
Then a leper came to Jesus, begging on his knees: “If You are willing, You can make me clean.”
41 Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
Moved with compassion, Jesus reached out His hand and touched the man. “I am willing,” He said. “Be clean!”
42 Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
And immediately the leprosy left him, and the man was cleansed.
43 Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
Jesus promptly sent him away with a stern warning:
44 “Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
“See that you don’t tell anyone. But go, show yourself to the priest and present the offering Moses prescribed for your cleansing, as a testimony to them.”
45 Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.
But the man went out and openly began to proclaim and spread the news. Consequently, Jesus could no longer enter a town in plain view, but He stayed out in solitary places. Yet people came to Him from every quarter.