< Marko 1 >
1 Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
The beginning of the gospel of Jesus Christ, the Son of God;
2 Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
as it is written in Isaiah the prophet: Behold, I send my messenger before thy face, who shall prepare thy way.
3 Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
The voice of one crying in the wilderness, Make ready the way of the Lord, make his paths straight.
4 Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
John was immersing in the wilderness, and preaching the immersion of repentance in order to the remission of sins.
5 Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
And all the country of Judea and the inhabitants of Jerusalem went out to him, and were all immersed by him in the river Jordan, confessing their sins.
6 Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
And John was clothed with camel’s hair, and had a girdle of leather around his loins, and he ate locusts and wild honey:
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
and he preached, saying: There comes after me One mightier than I, the strap of whose sandals I am not worthy to stoop down and loose.
8 Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I immerse you in water; but he will immerse you in the Holy Spirit.
9 Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
And it came to pass in those days, that Jesus came from Nazareth of Galilee, and was immersed by John in the Jordan.
10 Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
And immediately on coming up from the water, he saw the heavens opened, and the Spirit like a dove descending upon him.
11 Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
And there was a voice from the heavens: Thou art my beloved Son, in whom I delight.
12 Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
And immediately the Spirit compelled him to go forth into the wilderness.
13 akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
And he was there in the wilderness forty days, to be tempted by Satan; and he was with the wild beasts; and the angels ministered to him.
14 Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
But after John was delivered up, Jesus came into Galilee, preaching the gospel of the kingdom of God,
15 “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
and saying: The time has fully come, and the kingdom of God is at hand; repent, and believe the gospel.
16 Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
And as he walked by the sea of Galilee, he saw Simon, and Andrew the brother of Simon, throwing a net about in the sea; for they were fishers.
17 Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
And Jesus said to them: Come after me, and I will make you fishers of men.
18 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
And immediately they left their nets, and followed him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
And when he had gone a little further thence, he saw James the son of Zebedee, and John his brother, who also were in the ship, mending their nets.
20 Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
And he immediately called them: and they left their father Zebedee in the ship with the hired servants, and went after him.
21 Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
And they went into Capernaum; and immediately, on the sabbath, he entered the synagogue, and taught.
22 Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
And they were astonished at his teaching; for he taught them as one that had authority, and not as the scribes.
23 Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
And there was in their synagogue a man who had an unclean spirit; and he cried out,
24 akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
saying: Let us alone; what have we to do with thee, Jesus, thou Nazarene? Hast thou come to destroy us? I know thee who thou art, the Holy One of God.
25 Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
And Jesus rebuked him, saying: Be silent, and come out of him.
26 Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
And the unclean spirit threw him into convulsions, and cried with a loud voice, and came out of him.
27 Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
And all were amazed, so that they questioned one another, saying: What means this? What new teaching is this, that with authority he commands even the unclean spirits, and they obey him?
28 Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
And his fame immediately went abroad into all the surrounding country of Galilee.
29 Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
And forthwith, having gone out of the synagogue, they went into the house of Simon and Andrew, with James and John.
30 Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
Now the mother-in-law of Simon lay sick of a fever. And at once they told him of her.
31 Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
And he went to her, and took her by the hand, and raised her up, and the fever left her instantly; and she ministered to them.
32 Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
And at evening, when the sun had gone down, they brought to him all that were sick, and those who were possessed with demons.
33 Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
And the whole city came together to the door.
34 Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
And he cured many that were sick of various diseases, and cast out many demons, and did not suffer the demons to speak, because they knew him.
35 Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
And very early in the morning, while it was yet dark, he arose and went out, and departed to a desert place, and there prayed.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
And Simon, and those who were with him, followed after him.
37 Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
And when they had found him, they said to him: All are seeking for thee.
38 Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
And he said to them: Let us go into the neighboring towns, that I may preach there also; for I have come forth for this purpose.
39 Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
And throughout the whole of Galilee he continued to preach in their synagogues, and to cast out demons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
And there came to him a leper, beseeching him, and kneeling down to him, and saying to him: If thou wilt, thou canst make me clean.
41 Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
And Jesus, moved with compassion, stretched forth his hand, and touched him, and said to him: I will; be clean.
42 Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
And when he had spoken, the leprosy immediately departed from him, and he was cleansed.
43 Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
And he strictly charged him, and forthwith sent him away,
44 “Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
and said to him: See that you tell no one; but go, show yourself to the priest, and offer for your cleansing the things which Moses commanded, for a testimony to them.
45 Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.
But he went out, and began to proclaim it much, and to publish the matter abroad, so that he was no longer able to enter a city openly, but was without in desert places: and they came to him from every quarter.