< Marko 1 >

1 Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
天主子耶穌基督福音的開始,
2 Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, namtuma mjumbe wangu akutangulie; yeye atakutayarishia njia yako.
正如先知依撒意亞書上記載的:「看,我派遣我的使者在你面前,預備你的道路。
3 Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni mapito yake.”
曠野中有呼號者的聲音:你們當預備上主的道路,修直他的途徑。」
4 Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba ni lazima watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao.
洗者若翰便在曠野裏出現,宣講悔改的洗禮,為得罪之赦。
5 Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.
猶太全地和耶路撒冷的群眾都出來,到他那裏,承認自己的罪過,在約但河裏受他的洗。
6 Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.
若翰穿的是駱駝毛的衣服,腰間束的是皮帶,吃的是蝗蟲與野蜜。
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake.
他宣告說:「那比我更有力量的,要在我以後來,我連俯身解他的鞋帶也不配。
8 Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
我以水洗你們,他卻要以聖神洗你們。」
9 Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani.
在那些日子裏,耶穌加利肋亞納匝肋來,在約旦河裏受了若翰的洗。
10 Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa.
他剛從水裏上來,就看見天裂開了,聖神有如鴿子降在他上面;
11 Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
又有聲音從天上說:「你是我的愛子,我因你而喜悅。
12 Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani,
聖神立刻催他到曠野裏去。
13 akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamtumikia.
他在曠野裏,四十天之久,受撒殫的試探,與一起,並有天使服侍他。
14 Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema,
若翰被監禁後,耶穌來到加利肋亞,宣講天主的福音,
15 “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
說:「時期已滿,天主的國臨近了,你們悔改,信從福音罷!」
16 Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu.
當耶穌沿著加里肋亞海行走時,看見西滿和西滿的兄弟安德肋在海裏撒網,他們原是漁夫。
17 Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu.”
耶穌向他們說:「來跟隨我,我要使你們成為漁人的漁夫。」
18 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.
他們便立刻拋下了網,跟隨了他。
19 Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
耶穌向前行了不遠,看見載伯德的兒子雅各伯和他的弟弟若望,正在船上修網。
20 Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
耶穌遂立即召叫他們;他們就把自己的父親載伯德和傭工們留在船上,跟隨他去了。
21 Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika Sunagogi, akaanza kufundisha.
他們進了葛法翁;一到安息日,耶穌就進入會堂教訓人。
22 Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama walimu wao wa Sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.
人都驚奇他的教訓,因為他教訓他們正像有權威似的,不像經師們一樣。
23 Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu,
當時,在他們的會堂裏,正有一個附邪魔的人,他喊叫
24 akapaaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: wewe ni Mtakatifu wa Mungu!”
說:「納匝肋人耶穌! 我們與你有什麼相干﹖你竟來毀滅我們! 我佑道你是誰,你是天主的聖者。」
25 Yesu akamkemea, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”
耶穌叱責他說:「不要作聲! 從他身上出去!」
26 Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.
邪魔使那人拘攣了一陣,大喊一聲,就從他身上出去了。
27 Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
眾人大為驚愕,以致彼此詢問說:「這是怎麼一回事﹖這是新的教訓,並具有權威;他連給邪魔出命,邪魔也聽從他。」
28 Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika wilaya ya Galilaya.
他的聲譽遂即傳遍了加里肋亞附近各處。
29 Wakatoka katika sunagogi, wakaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea; Yakobo na Yohane walikwenda pamoja nao.
他一出會堂,就同雅各伯和若望來到了西滿和安德肋的家裏。
30 Basi, mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa kitandani ana homa kali. Wakamwarifu Yesu mara alipowasili.
那時,西滿的岳母正躺著發燒;有人就向耶穌提起她來,
31 Yesu akamwendea huyo mama, akamshika mkono, akamwinua. Na ile homa ikamwacha, akaanza kuwatumikia.
耶穌上前去,握住她的手,扶起她來,熱症隨即離開了她;她就伺候他們。
32 Jioni, jua lilipokwisha tua, wakamletea Yesu wagonjwa wote na watu waliopagawa na pepo.
到了晚上,日落之後,人把所有患病的和附魔的,都帶到他跟前,
33 Watu wote wa mji ule wakakusanyika nje ya mlango.
閤城的人都聚在門前。
34 Naye Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa mbalimbali; aliwafukuza pepo wengi, lakini hakuwaruhusu kusema kitu maana walikuwa wanamjua yeye ni nani.
耶穌治好了許多患各種病症的人,驅逐了許多魔鬼,並且不許魔鬼說話,因為魔鬼認識他。
35 Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
清晨,天還很黑,耶穌就起身出去,到荒野的地方在那裏祈禱。
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta.
西滿和同他在一起的人都去追尋他,
37 Walipomwona wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta.”
找到了他,就向他說:「眾人都找你呢! 」
38 Yesu akawaambia, “Twendeni katika miji mingine ya jirani nikahubiri huko pia, maana nimekuja kwa sababu hiyo.”
耶穌對他們說:「讓我們到別處去,到鄰近的村鎮去罷! 叫我也在那裏宣講,因為我是為這事出來的。」
39 Basi, akaenda kila mahali Galilaya akihubiri katika masunagogi na kufukuza pepo.
他遂到加里肋亞各地,在他們的會堂裏宣講,並驅逐魔鬼。
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimwendea Yesu, akapiga magoti, akamwomba, “Ukitaka, waweza kunitakasa!”
有一個癩病人來到耶穌跟前,跪下求他說:「你若願意,就能潔淨我。」
41 Yesu akamwonea huruma, akanyosha mkono wake, akamgusa na kumwambia, “Nataka, takasika!”
耶穌動了憐憫的心,就伸手撫摸他,向他說:「我願意,你潔淨了罷!」
42 Mara ukoma ukamwacha mtu huyo, akatakasika.
癩病立時脫離了他,他就潔淨了。
43 Kisha Yesu akamwambia aende zake upesi na kumwonya vikali,
然後耶穌嚴厲警告他,立即催他走,
44 “Usimwambie mtu yeyote jambo hili, ila nenda ukajionyeshe kwa kuhani; kisha utoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama alivyoamuru Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
並向他說:「當心! 什麼也不可告訴人,但去叫司祭檢驗你,並為你的潔淨,奉獻梅瑟所規定的,給他們當作證據。」
45 Lakini huyo mtu akaenda, akaanza kueneza habari hiyo kila mahali na kusema mambo mengi hata Yesu hakuweza tena kuingia katika mji wowote waziwazi; ikamlazimu kukaa nje, mahali pa faragha. Hata hivyo, watu wakamwendea kutoka kila upande.
但那人一出去,便開始極力宣揚,把這事傳揚開了,以致耶穌不能再公然進城,只好留在外邊荒野的地方;但人們卻從各處到他跟前來。

< Marko 1 >