< Luka 1 >
1 Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
SINCE many have been disposed to write narratives of those events, of which we have full assurance,
2 Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
as they delivered them to us, who from the first were eye-witnesses and ministers of the word;
3 Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
it seemed proper for me also, as I had examined them all accurately, to write out the whole, methodically, for thee, excellent Theophilus:
4 ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
that thou mayest know the truth of the statements, which thou hast been taught.
5 Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
In the days of Herod the king of Judaea, there was a certain priest, whose name was Zachariah, of the ministration of the house of Abijah; and his wife was of the daughters of Aaron, and her name was Elisabeth.
6 Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
And they were both upright before God, and walked in all his commandments, and in the righteousness of the Lord, without reproach.
7 Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
But they had no child, because Elisabeth was barren: and they were both advanced in life.
8 Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
And it occurred, that as he performed the priestly functions in the order of his ministration before the Lord,
9 Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
according to the usage of the priesthood, it fell to him to offer the incense. And he went into the temple of the Lord,
10 Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
and the whole multitude of the people were praying without, at the time of incense.
11 Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
And the angel of the Lord appeared to Zachariah, standing on the right side of the altar of incense.
12 Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
And when Zachariah saw him, he was agitated, and fear fell upon him.
13 Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
And the angel said to him: Fear not, Zachariah; for thy prayer is heard, and thy wife Elisabeth will bear thee a son, and thou shalt call his name John.
14 Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
And thou wilt have joy and gladness: and many will rejoice at his birth.
15 Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
For he will be great before the Lord; and he will not drink wine nor strong drink, and will be filled with the Holy Spirit even from his mother's womb.
16 Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
And many of the children of Israel will he convert to the Lord their God.
17 Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
And he will go before him, in the spirit and power of Elijah the prophet, and will turn the heart of the fathers unto the children, and them that are disobedient to the knowledge of the righteous, and will prepare a perfect people for the Lord.
18 Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
And Zachariah said to the angel: How shall I know this? For I am old, and my wife is advanced in life.
19 Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
The angel answered, and said to him: I am Gabriel, who stand before God; and I am sent to converse with thee, and to tell thee these things.
20 Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
Henceforth thou wilt be dumb, and unable to speak, until the day when these things take place: because thou believedst not my words, which will be fulfilled in their time.
21 Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
And the people were standing and waiting for Zachariah; and they wondered at his tarrying so long in the temple.
22 Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
And when Zachariah came forth, he could not speak with them: and they understood that he had seen a vision in the temple: and he made many signs to them, and remained speechless.
23 Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
And when the days of his ministration were accomplished, he came to his house.
24 Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
And it was after those days, that Elisabeth his wife conceived. And she secluded herself five months; and she said:
25 “Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
These things hath the Lord done for me, in the days when he looked upon me to take away my reproach among men.
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
And in the sixth month, the angel Gabriel was sent by God into Galilee, to a city named Nazareth,
27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
to a virgin espoused to a man whose name was Joseph, of the house of David; and the virgin's name was Mary.
28 Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
And the angel entered the house, and said to her: Peace to thee, thou full of grace! The Lord is with thee: and blessed art thou among women.
29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
And when she saw him, she was agitated by his speech; and she pondered, what this salutation could mean.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
And the angel said to her: Fear not, Mary; for thou hast found favor with God.
31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
For lo, thou wilt conceive in thy womb, and wilt bear a son, and wilt call his name Jesus.
32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
He will be great, and will be called the Son of the Most High, and the Lord God will give him the throne of his father David.
33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
And he will reign over the house of Jacob for ever; and of his reign there will be no end. (aiōn )
34 Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
And Mary said to the angel: How can this be, as I have not known a man?
35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
The angel replied, and said to her: The Holy Spirit will come, and the power of the Most High will overshadow thee; therefore he that is born of thee is holy, and will be called the Son of God.
36 Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
And lo, Elisabeth thy kinswoman, even she too hath conceived a son in her old age; and this is the sixth month with her who is called barren.
37 Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
Because nothing is difficult for God.
38 Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
Mary said: Behold, I am the handmaid of the Lord; be it to me, according to thy word. And the angel departed from her.
39 Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
And Mary arose in those days, and went hastily to the mountain district, to a city of Judaea;
40 Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
and entered the house of Zachariah, and saluted Elisabeth.
41 Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
And it was so, that when Elisabeth heard the salutation of Mary, the child leaped in her womb, and she was filled with the Holy Spirit.
42 akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
And she cried out with a loud voice, and said to Mary: Blessed art thou among women; and blessed is the fruit of thy womb.
43 Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
And whence is this to me, that the mother of my Lord should come to me?
44 Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
For lo, as the voice of thy salutation fell upon my ears, with great joy the child leaped in my womb.
45 Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
And happy is she that believed; for there will be a fulfillment of those things that were told her by the Lord.
And Mary said: My soul doth magnify the Lord:
47 “Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
and my spirit rejoiceth in God the author of my life.
48 Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
For he hath looked upon the humble condition of his hand maid; and lo, henceforth all generations will ascribe blessedness to me.
49 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
And He that is mighty hath done for me great things; and holy is his name.
50 Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
And his mercy is on them that fear him, for generations and posterities.
51 Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
He hath wrought victory with his arm; and hath scattered the proud in the imagination of their heart.
52 amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
He hath cast down the mighty from their thrones, and hath exalted the lowly.
53 Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
The hungry hath he satisfied with good things, and the rich hath he sent away empty.
54 Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
He hath aided Israel his servant, and remembered his mercy,
55 Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn )
(as he spoke with the fathers, ) with Abraham and his seed, for ever. (aiōn )
56 Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
And Mary remained with Elisabeth about three months, and returned to her home.
57 Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
And Elisabeth's time of bringing forth arrived; and she bore a son.
58 Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
And her neighbors and relatives heard that the Lord had magnified his mercy to her, and they rejoiced with her.
59 Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
And it occurred, that on the eighth day they came to circumcise the child. And they called him by the name of his father, Zachariah.
60 Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
And his mother answered and said: Not so; but John, shall he be called.
61 Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
And they said to her: There is no one among thy kindred called by that name.
62 Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
And they made signs to his father, how he would have him named.
63 Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
And he asked for a tablet, and wrote, and said: John is his name. And every one was surprised.
64 Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
And immediately his mouth was opened, and his tongue; and he spoke, and praised God.
65 Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
And fear came upon all their neighbors; and these things were talked of in all the mountain district of Judaea.
66 Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
And all who heard, pondered them in their heart, and said: What will this child be? And the hand of the Lord was with him.
67 Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
And Zachariah his father was filled with the Holy Spirit, and prophesied, and said:
68 “Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
Blessed be the Lord God of Israel, who hath visited his people, and wrought redemption for them:
69 Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
And hath raised up a horn of redemption for us, in the house of David his servant:
70 Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn )
as he spake by the mouth of his holy prophets, who were of old, (aiōn )
71 kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
that he would redeem us from our enemies, and from the hand of all that hate us.
72 Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
And he hath exercised his mercy to our fathers, and hath remembered his holy covenants,
73 Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
and the oath that he sware to Abraham our father, that he would grant to us,
74 tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
to be redeemed from the hand of our enemies; and that we should worship before him, without fear,
75 kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
all our days, in rectitude and uprightness.
76 Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
And thou, child, wilt be called a prophet of the Most High; for thou wilt go before the face of the Lord, to prepare his way,
77 kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
that he may give the knowledge of life to his people, and forgiveness of their sins,
78 Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
through the compassion of the mercy of our God; whereby the day-spring from on high will visit us,
79 na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
to give light to them that sit in darkness, and in the shadow of death; and to guide our feet into the way of peace.
80 Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.
And the child grew, and was strengthened in spirit. And he was in the wilderness, until the day of his manifestation to Israel.