< Luka 8 >

1 Baada ya hayo, Yesu alipitia katika miji na vijiji akitangaza Habari Njema za Ufalme wa Mungu. Wale kumi na wawili waliandamana naye.
Ensuite, Jésus allait de ville en ville et de village en village, prêchant et annonçant la bonne nouvelle du royaume de Dieu;
2 Pia wanawake kadhaa ambao Yesu alikuwa amewatoa pepo wabaya na kuwaponya magonjwa, waliandamana naye. Hao ndio akina Maria (aitwaye Magdalene), ambaye alitolewa pepo wabaya saba;
et les Douze étaient avec lui. Il y avait aussi avec eux quelques femmes, qui avaient été délivrées de malins esprits ou guéries de leurs maladies: Marie appelée Madeleine, de laquelle étaient sortis sept démons,
3 Yoana, mke wa Kuza, mfanyakazi mkuu wa Herode; Susana na wengine kadhaa. Hao wanawake walikuwa wakiwatumikia kwa mali yao wenyewe.
Jeanne, femme de Chuzas, intendant d'Hérode, Suzanne et plusieurs autres, qui les assistaient de leurs biens.
4 Kundi kubwa la watu lilikuwa linakusanyika, na watu walikuwa wanamjia Yesu kutoka kila mji. Naye akawaambia mfano huu:
Comme une grande foule s'était rassemblée, et qu'on venait à lui de toutes les villes, Jésus leur dit en parabole:
5 “Mpanzi alikwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akipanda zile mbegu, nyingine zilianguka njiani, na wapita njia wakazikanyaga, na ndege wakazila.
Le semeur sortit pour semer. Et comme il jetait sa semence, il en tomba une partie le long du chemin; elle fut foulée aux pieds, et les oiseaux du ciel la mangèrent toute.
6 Nyingine zilianguka penye mawe, na baada ya kuota zikanyauka kwa kukosa maji.
Une autre partie tomba sur un sol pierreux; quand elle fut levée, elle sécha, parce qu'elle n'avait point d'humidité.
7 Nyingine zilianguka kati ya miti ya miiba. Ile miti ya miiba ilipoota ikazisonga.
Une autre partie tomba parmi les épines; les épines poussèrent avec la semence et l'étouffèrent.
8 Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikaota na kuzaa asilimia mia.” Baada ya kusema hayo, akapaaza sauti, akasema, “Mwenye masikio na asikie!”
Une autre partie tomba dans la bonne terre; elle leva et produisit du fruit, cent pour un. En disant ces choses, il s'écriait: Que celui qui a des oreilles pour entendre, entende!
9 Wanafunzi wake wakamwuliza Yesu maana ya mfano huo.
Ses disciples lui demandèrent ce que signifiait cette parabole.
10 Naye akajibu, “Ninyi mmejaliwa kujua siri za Ufalme wa Mungu, lakini hao wengine sivyo; ila hao huambiwa kwa mifano, ili wakitazama wasiweze kuona, na wakisikia wasifahamu.
Il répondit: Il vous a été donné de connaître les mystères du royaume de Dieu; mais, aux autres, tout est présenté en forme de paraboles, de sorte qu'en voyant, ils ne voient pas, et qu'en entendant, ils ne comprennent point.
11 “Basi, maana ya mfano huu ni hii: mbegu ni neno la Mungu.
Voici donc ce que signifie cette parabole: La semence, c'est la parole de Dieu.
12 Zile zilizoanguka njiani zinaonyesha watu wale wanaosikia lile neno, halafu Ibilisi akaja na kuliondoa mioyoni mwao wasije wakaamini na hivyo wakaokoka.
Ceux qui la reçoivent le long du chemin, ce sont ceux qui l'ont entendue; mais ensuite vient le Diable qui enlève cette parole de leur coeur, de peur qu'ils ne croient et ne soient sauvés.
13 Zile zilizoanguka penye mawe zinaonyesha watu wale ambao wanaposikia juu ya lile neno hulipokea kwa furaha. Hata hivyo, kama zile mbegu, watu hao hawana mizizi maana husadiki kwa kitambo tu, na wanapojaribiwa hukata tamaa.
Ceux qui la reçoivent sur le sol pierreux, ce sont ceux qui, entendant la parole, la reçoivent avec joie; mais ils n'ont point de racine, ils ne croient que pour un temps; et, quand l'épreuve survient, ils se retirent.
14 Zile zilizoanguka kwenye miti ya miiba ni watu wale wanaosikia lile neno, lakini muda si muda, wanapokwenda zao, husongwa na wasiwasi, mali na anasa za maisha, na hawazai matunda yakakomaa.
Ce qui est tombé parmi les épines, ce sont ceux qui ont entendu la parole, mais qui s'en vont et la laissent étouffer par les soucis, les richesses et les plaisirs de cette vie, de sorte qu'ils ne portent pas de fruit qui vienne à maturité.
15 Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu wale wanaolisikia lile neno, wakalizingatia kwa moyo mwema na wa utii. Hao huvumilia mpaka wakazaa matunda.
Mais ce qui tombe dans la bonne terre, ce sont ceux qui, ayant entendu la parole avec un coeur honnête et bon, la retiennent et portent du fruit avec persévérance.
16 “Watu hawawashi taa na kuifunika kwa chombo au kuiweka mvunguni. Lakini huiweka juu ya kinara ili watu wanapoingia ndani wapate kuona mwanga.
Il n'est personne qui, après avoir allumé une lampe, la couvre d'un boisseau ou la mette sous un lit. Au contraire, on la place sur un support, afin que ceux qui entrent voient la lumière.
17 “Chochote kilichofichwa kitafichuliwa na siri yoyote itagunduliwa na kujulikana hadharani.
En effet, il n'y a rien de secret qui ne doive être manifesté, ni rien de caché qui ne doive être connu et mis en évidence.
18 “Kwa hiyo, jihadharini jinsi mnavyosikia; maana aliye na kitu ataongezewa, lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani kuwa anacho, kitachukuliwa.”
Prenez donc garde à la manière dont vous écoutez; car on donnera à celui qui a, mais à celui qui n'a pas, on ôtera même ce qu'il croit avoir.
19 Hapo mama na ndugu zake Yesu wakamjia, lakini hawakuweza kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu.
Sa mère et ses frères vinrent le trouver; mais ils ne pouvaient l'aborder à cause de la foule.
20 Yesu akapewa habari kwamba mama na ndugu zake walikuwa nje, wanataka kumwona.
On vint donc lui dire: Ta mère et tes frères sont là dehors, qui désirent te voir.
21 Lakini Yesu akawaambia watu wote, “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika.”
Mais il répondit: Ma mère et mes frères, ce sont ceux qui écoutent la parole de Dieu et qui la mettent en pratique!
22 Siku moja, Yesu alipanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, “Tuvuke ziwa twende mpaka ng'ambo.” Basi, wakaanza safari.
Un jour, il entra dans une barque avec ses disciples, et il leur dit: Passons de l'autre côté du lac; et ils partirent.
23 Walipokuwa wanasafiri kwa mashua, Yesu alishikwa na usingizi, akalala. Dhoruba kali ikaanza kuvuma, maji yakaanza kuingia ndani ya mashua, wakawa katika hatari.
Comme ils voguaient, Jésus s'endormit. Un tourbillon de vent vint s'abattre sur le lac; la barque se remplissait d'eau et ils étaient en danger.
24 Wale wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwamsha wakisema, “Bwana, Bwana! Tunaangamia!” Yesu akaamka, akaikemea dhoruba na mawimbi, navyo vikatulia, kukawa shwari.
Alors ils vinrent à lui, et le réveillèrent en lui disant: Maître, Maître, nous périssons! Mais lui, s'étant réveillé, imposa silence au vent et aux flots, qui s'apaisèrent, et il se fit un grand calme.
25 Kisha akawaambia, “Iko wapi imani yenu?” Lakini wao walishangaa na kuogopa huku wakiambiana, “Huyu ni nani basi, hata anaamuru dhoruba na mawimbi, navyo vinamtii?”
Il leur dit alors: Où est votre foi? Et, saisis de crainte et d'admiration, ils se disaient entre eux: Quel est donc celui-ci? Il commande même aux vents et aux flots, et ils lui obéissent!
26 Wakaendelea na safari, wakafika pwani ya nchi ya Wagerase inayokabiliana na Galilaya, ng'ambo ya ziwa.
Ils abordèrent ensuite au pays des Géraséniens, qui est vis-à-vis de la Galilée.
27 Alipokuwa anashuka pwani, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo alimjia kutoka mjini. Kwa muda mrefu mtu huyo, hakuwa anavaa nguo, wala hakuwa anaishi nyumbani bali makaburini.
Et quand Jésus fut descendu à terre, il vint au devant de lui un homme de la ville, qui était possédé de plusieurs démons. Depuis fort longtemps il ne portait pas de vêtement, et il ne demeurait pas dans une maison, mais dans les tombeaux.
28 Alipomwona Yesu, alipiga kelele na kujitupa chini mbele yake, na kusema kwa sauti kubwa “We, Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu una shauri gani nami? Ninakusihi usinitese!”
Dès qu'il vit Jésus, il poussa un grand cri, et, se jetant à ses pieds, il dit d'une voix forte: Qu'y a-t-il entre moi et toi, Jésus, Fils du Dieu très haut? Je t'en supplie ne me tourmente pas!
29 Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikwishamwambia huyo pepo mchafu amtoke mtu huyo. Pepo huyo mchafu alikuwa anamvamia mtu huyo mara nyingi, na ingawa watu walimweka ndani na kumfunga kwa minyororo na pingu, lakini kila mara alivivunja vifungo hivyo, akakimbizwa na pepo huyo mchafu hadi jangwani.
En effet, l'esprit impur venait de recevoir de Jésus l'ordre de sortir de cet homme, dont il s'était rendu maître depuis longtemps; et, bien qu'on gardât le malade, lié de chaînes et les fers aux pieds, il rompait ses liens et était emporté par le démon dans les déserts.
30 Basi, Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” Yeye akajibu, “Jina langu ni Jeshi” —kwa sababu pepo wengi walikuwa wamempagaa.
Jésus lui demanda: Quel est ton nom? Il répondit: Légion! Car plusieurs démons étaient entrés en lui.
31 Hao pepo wakamsihi asiwaamuru wamtoke na kwenda kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos g12)
Et ils suppliaient Jésus de ne pas leur commander d'aller dans l'abîme. (Abyssos g12)
32 Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha mlimani. Basi, hao pepo wakamsihi awaruhusu wawaingie. Naye Yesu akawapa ruhusa.
Or, il y avait là un grand troupeau de pourceaux qui paissaient dans la montagne. Les démons supplièrent Jésus de leur permettre d'entrer dans ces pourceaux; et il le leur permit.
33 Kwa hiyo pepo hao wakamtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nao wakaporomoka kwenye ule mteremko mkali, wakatumbukia ziwani, wakazama majini.
Etant donc sortis de cet homme ils entrèrent dans les pourceaux; le troupeau se précipita dans le lac, du haut de la falaise, et il s'y noya.
34 Wale wachungaji walipoona yote yaliyotokea walikimbia, wakaenda kuwapa watu habari, mjini na mashambani.
Ceux qui le faisaient paître, voyant ce qui était arrivé, s'enfuirent et répandirent la nouvelle dans la ville et dans la campagne.
35 Watu wakaja kuona yaliyotokea. Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mtu aliyetokwa na pepo ameketi karibu na Yesu, amevaa nguo, ana akili zake, wakaogopa.
Alors les gens sortirent pour voir ce qui s'était passé; et, quand ils furent arrivés auprès de Jésus, ils trouvèrent l'homme, de qui les démons étaient sortis, assis aux pieds de Jésus, habillé et dans son bon sens; et ils furent saisis de crainte.
36 Wale watu walioshuhudia tukio hilo waliwaeleza hao jinsi yule mtu alivyoponywa.
Les témoins de l'événement leur racontèrent comment le démoniaque avait été délivré.
37 Wakazi wa nchi ya Gerase walishikwa na hofu kubwa. Kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke, aende zake. Hivyo Yesu alipanda tena mashua, akaondoka.
Tous les habitants de la contrée des Géraséniens prièrent Jésus de se retirer de chez eux; car ils étaient saisis d'une grande frayeur. Il entra donc dans la barque pour s'en retourner.
38 Yule mtu aliyetokwa na wale pepo akamsihi aende pamoja naye. Lakini Yesu hakumruhusu, bali akamwambia,
Et l'homme, de qui les démons étaient sortis, lui demandait la permission de rester avec lui; mais Jésus le renvoya, en disant:
39 “Rudi nyumbani ukaeleze yote Mungu aliyokutendea.” Basi, yule mtu akaenda akitangaza kila mahali katika mji ule mambo yote Yesu aliyomtendea.
Retourne dans ta maison, et raconte tout ce que Dieu a fait pour toi. Il s'en alla donc, publiant par toute la ville tout ce que Jésus lui avait fait.
40 Yesu aliporudi upande mwingine wa ziwa, kundi la watu lilimkaribisha, kwa maana wote walikuwa wanamngojea.
A son retour, Jésus fut reçu par la foule; car tous l'attendaient.
41 Hapo akaja mtu mmoja aitwaye Yairo, ofisa wa sunagogi. Alijitupa miguuni pa Yesu, akamwomba aende nyumbani kwake,
Et il vint un homme appelé Jaïrus, qui était chef de la synagogue. Il se jeta aux pieds de Jésus, en le priant de venir dans sa maison,
42 kwa kuwa binti yake wa pekee, mwana wa pekee mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa mahututi. Yesu alipokuwa akienda, watu wakawa wanamsonga kila upande.
parce qu'il avait une fille unique, âgée de douze ans, qui se mourait. Pendant que Jésus s'y rendait, la foule le pressait de tous côtés.
43 Kulikuwa na mwanamke mmoja kati ya lile kundi la watu, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote kwa waganga, hakuna aliyefaulu kumponya.
Alors une femme, qui avait une perte de sang depuis douze ans et qui avait dépensé tout son bien en médecins, sans avoir pu être guérie par aucun,
44 Huyo mwanamke alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake. Papo hapo akaponywa ugonjwa wake wa kutokwa damu.
s'approcha de lui par derrière et toucha le bord de son vêtement; et à l'instant, sa perte de sang s'arrêta.
45 Yesu akasema, “Ni nani aliyenigusa?” Wote wakasema kwamba hapakuwa na mtu aliyemgusa. Naye Petro akasema, “Mwalimu, umati wa watu umekuzunguka na kukusonga!”
Alors Jésus dit: Qui m'a touché? Comme tous s'en défendaient, Pierre et ceux qui étaient avec lui, répondirent: Maître, la foule t'environne et te presse!
46 Lakini Yesu akasema, “Kuna mtu aliyenigusa, maana nimehisi nguvu imenitoka.”
Jésus reprit: Quelqu'un m'a touché; car j'ai senti qu'une force est sortie de moi.
47 Yule mwanamke alipoona kwamba hawezi kujificha, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa mbele ya Yesu. Hapo akaeleza mbele ya wote kisa cha kumgusa Yesu na jinsi alivyoponyeshwa mara moja.
La femme, voyant qu'elle n'avait pu rester cachée, vint toute tremblante se jeter à ses pieds; et elle expliqua, devant tout le peuple, pourquoi elle l'avait touché, et comment elle avait été immédiatement guérie.
48 Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani.”
Jésus lui dit: Ma fille, ta foi t'a sauvée; va en paix.
49 Alipokuwa bado akiongea, Yairo akaletewa habari kutoka nyumbani: “Binti yako ameshakufa, ya nini kumsumbua Mwalimu zaidi?”
Comme il parlait encore, quelqu'un vint de la maison du chef de la synagogue et dit à ce dernier: Ta fille est morte; n'importune plus le Maître.
50 Yesu aliposikia hayo akamwambia Yairo, “Usiogope; amini tu, naye atapona.”
Mais Jésus, l'ayant entendu, dit à Jaïrus: Ne crains point! Crois seulement, et elle sera sauvée.
51 Alipofika nyumbani hakumruhusu mtu kuingia ndani pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohane, Yakobo na wazazi wa huyo msichana.
Quand il fut arrivé à la maison, il ne laissa entrer avec lui que Pierre, Jacques et Jean, et le père et la mère de l'enfant.
52 Watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili yake. Lakini Yesu akawaambia, “Msilie, kwa maana mtoto hajafa, amelala tu!”
Tous pleuraient et se lamentaient sur elle. Alors Jésus dit: Ne pleurez pas; elle n'est pas morte, mais elle dort.
53 Nao wakamcheka kwa sababu walijua kwamba alikuwa amekufa.
Et ils se moquaient de lui, sachant qu'elle était morte.
54 Lakini Yesu akamshika mkono akasema, “Mtoto amka!”
Mais Jésus la prit par la main, et dit à haute voix: Mon enfant, lève-toi!
55 Roho yake ikamrudia, akaamka mara. Yesu akaamuru wampe chakula.
Alors l'esprit lui revint; elle se leva à l'instant, et il commanda de lui donner à manger.
56 Wazazi wake walishangaa, lakini Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote hayo yaliyotendeka.
Ses parents furent saisis d'étonnement; mais il leur défendit de dire à personne ce qui était arrivé.

< Luka 8 >