< Luka 6 >
1 Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
有一個安息日,耶穌經過麥田時,祂的門徒掐著麥穗,用手搓著吃。
2 Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
有幾個法利賽人說:「為什麼你們做安息日不准做的呢? 」
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
耶穌回答說:「你們沒有讀過:達味和同他在一起的人,在飢餓時所做的嗎?
4 Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
怎麼進了天主的殿,拿起供餅來吃了,又給了同他在一起的人吃。這餅原不准他人吃,而只准司祭吃。
5 Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
耶穌又向他們說:「人子是安息日的主。」
6 Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
另一個安息日,祂進了會堂施教。在那裡有一個人,他的右手乾枯了。
7 Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
經師和法利賽人窺察祂是否在安息日治病,好尋隙好控告祂。
8 Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
祂看透了他們的心思,就對那枯了手的人說:「起來,站在中間。」他遂站了起來。
9 Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
耶穌對他們說:「我問你們:安息日是許行善呢? 還是許作惡呢? 是救命呢? 還是喪命呢?
10 Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
祂環視眾人一週,就對那人說:「伸出你的手來! 那人照樣一做,他的手便復了原。
11 Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
他們竟狂怒填胸,彼此商議,要怎樣來對付耶穌。
12 Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
在這幾天,耶穌出去,上山祈禱。
13 Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
天一亮,祂把們徒叫來,由他們人揀選了十二人,並稱他們為宗徒:
14 Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
即西滿,耶穌又給他起名叫伯多祿,和他的兄弟安德肋、雅各伯、若望、斐理伯、巴爾多祿茂、
15 Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
瑪竇、多默、阿耳斐的兒子雅各伯、號稱「熱誠者」的西滿、
16 Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
雅各伯的兄弟猶達和猶達依斯加略,他成了負賣者。
17 Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
耶穌同他們下山,站在一塊平地上,有祂的一大群們徒和很多從猶太、耶路撒冷及提洛和漆冬海邊來的群眾,
18 Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
他們來是為聽祂講道,並為治好自己的病症;那些疲邪魔纏擾的人都被治好了
19 Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
群眾都設法觸摸祂,因為有一種能力從祂身上出來,治好眾人。
20 Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
耶穌舉目望自己的們徒說:「你們貧窮的是有福的,因為天主的國是你們的。
21 Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
你們現今飢餓的是有福的,因為你們將得飽飫。你們現今哭泣的是有福的,因為你們將要歡笑。
22 “Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
幾時,為了人子的緣故,人惱恨你們,並棄絕你們,並以的名字為可惡的,而加以辱罵詛咒,你們才是有福的。
23 Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
在那一天,歡喜踴躍吧! 看,你們的賞報在天上是豐厚的,因為他們的祖先也同樣對待了先知。
24 Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
但是你們富有的是禍的,因為你們已經獲得了你們的安慰。
25 Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
你們現今飽飫的是禍的,因為你們將要飢餓。你們現今歡笑的是禍的,因為你們將要哀慟哭泣。
26 Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
幾時,眾人都誇讚你們,你們是禍的,因為他們的祖先也同樣對待了假先知。
27 “Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
但是我給你們這些聽眾說:應愛你們的仇人,善待惱恨你們的人;
28 Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
應祝福詛咒你們的人,為毀謗你們的人祈禱。
29 Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
有人打你的面頰,也把另一面轉給他,有人拿去你的外衣,也不要阻擋他拿你的內衣。
30 Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
凡求你的,就給他;有人拿你的東西,別再索回。
31 Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
你們願意人怎麼待你們,也要怎麼待人。
32 “Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
若你們愛那愛你們的,為你們還算什麼功德? 因為連罪人也愛那愛他們的人。
33 Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
你們善待那善待你們的,為你們還算什麼功德? 因為連罪人也這樣做。
34 Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
你們若借給那些有希望償還的,,為你們還算什麼功德? 就是連罪人也借給罪人,為能如數收回。
35 Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
但是,當愛你們的仇人,善待他們;借出,不要再有所希望:如此,你們的賞報必定豐厚,且要成為至高者的子女,因為祂對待忘恩的和惡人,是仁慈的。
36 Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
你們應當慈悲,就像你們的父那樣慈悲。
37 “Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
你們不要判斷,你們也就不受判斷;不要定罪,也就不被定罪;你們要赦免,也就蒙赦免。
38 Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
你們給也就給你們;並且還要用好的,連按帶搖,以致外溢的升斗,倒在你們的懷裏,因為你們用什麼升斗量,也用什麼升斗量給你們。
39 Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
祂又向他們講比喻說:「瞎子豈能給瞎子領路? 不是兩人都要跌在坑裏嗎?
40 Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
沒有徒弟勝過師父的:凡受過完備教育的,僅相似自己的師父而已。
41 Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
怎麼,你看見你兄弟眼中的木屑,而你眼中的大樑,倒不理會呢?
42 Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
你怎能對你的兄弟說:兄弟,讓我取出你眼中的木屑吧! 而你竟看不見你眼中的大樑呢? 假善人啊! 先取出你眼中的大樑,然後才看得清楚,以便取出你兄弟眼中的木屑。
43 “Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
沒有好樹結壞果子的,也人壞樹結好果子的。
44 Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
每一棵樹,憑它的果子就可認出來。人從荊棘上收不到無花果,從茨藤上也剪不到葡萄。
45 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
善人從自己心中的善庫發出善來,惡人從惡庫中發出惡來,因為心裏充滿什麼,口裏就說什麼。
46 “Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
你們為什麼稱呼我:主啊! 主啊! 而不我所吩咐的呢? 」
47 Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
凡到我跟前,聽了我的道理,而實行的,我要給你們指出,他相似什麼人:
48 Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
他相似一個建築房屋的人,掘地深挖,把基礎立在盤石上,洪水瀑發時,大水沖擊那座房屋,而不能搖動它,因為它建築得好。
49 Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”
但那聽了而不實行的,相似在平地上不打基礎,而築房屋的人,洪水一沖擊,那房屋立刻傾倒,且破壞的很慘。」