< Luka 6 >
1 Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
Sabbath mhmüp üng Jesuh lo hmu lama cit se axüisaw he naw kyung cangvui jah kpyat u lü ami kut am mnawiki he naw ei u se,
2 Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
Pharise avang he naw, “Ivai Sabbath mhmüp üng am nghlawiki nami pawhki ni?” ami ti.
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
Jesuh naw jah msang lü, “Davit a ei cawi law lü, a püi he am i ami pawh am nami kheh khawiki aw?
4 Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
Pamhnama ima lut lü, ktaiyüe däng naw ami ei ngkawi muk lo lü, ei lü, a püi he üng pi a jah pet cen,” a ti.
5 Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
Acunüng Jesuh naw, “Khyanga capa hin Sabbatha bawi ni,” a ti.
6 Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
Sabbath akce üng Sinakoka lut lü a jah mthei. Acunüng khyang mat a kut kpat lam xoki awmki.
7 Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
Thum ksing he la Pharise he avang naw ami mkateinak vaia, Sabbath mhmüp üng mdaw law be khai aw tia a peia awm u lü ami mcih.
8 Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
Jesuh naw ami ngaihkyunak jah ksingki naw akutxo üng, “Tho law lü maa lawa” ti se, akxo cun tho law lü ngdüiki.
9 Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
Acunüng Jesuh naw, “Mat ka ning jah kthäh khai. Sabbath mhmüp üng kpüi vai aw angkawih? Kpyeh vai aw angkawih? Xünak küikyan vai aw angkawih? Kpyeh vai aw angkawi?” a ti.
10 Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
Acunüng ami van jah teng law päng lü; akxo üng, “Na kut sänga” ti se, acunkba a säng la vanglama ka kba a kut daw law beki.
11 Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
Acunüng ami mlung naw jah uimsoei se ikba Jesuh ami pawh vaia ngthäh kyuki he.
12 Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
Acunüng, Jesuh ktaiyü khaia mcunga ktawih lü, Pamhnama veia mthai mhlän lü ktaiyüki.
13 Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
Khaw athaih law la axüisaw he a veia jah khü lü, xaleinghngih ngsä hea a jah xü he cun,
14 Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
Pitaa a sui Sihmon la a na Andru; Jakuk la Johan, Philip la Batolame,
15 Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
Mahte la Thomah, Alaphaha capa Jakuk, Patriot naki Sihmon,
16 Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
Jakuka ca Judah la Jesuh ceng lawkia Judah Iskarota kyaki he.
17 Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
Jesuh a ngsä he am mcung üngka naw ami kyum law be üng, a donak üng axüisaw he khawjah am ngdüiki he. Acuia khyang khawjah, Judah khaw avan üngka he la, Jerusalem üngka he, Turah la Sidon mlüh lam tuikam üngka khyang khawjah;
18 Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
a ngthu ngai khai he la ami natnak a jah mdaw be vaia law hüki he. Acunüng ngmüimkhya kse hea jah pawhe pi law u se a jah mdaw be.
19 Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
A vei üngka naw khyaibahnak lut law lü jah yai sak se, khyang avan naw ami hnet vaia ktha naki he.
20 Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
Jesuh naw axüisaw he jah teng lü, “M'yenkseki he aw nami jo sen ve; Pamhnama khaw nami hama kyaki!
21 Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
“Nangmi atuh nami ei nami cawiki nami jo sen ve; nami ei nami phü law khaia kyaki! “Nangmi atuh nami mbawikyapki he nami jo sen ve; nami yaiyüng law khaia kyaki!
22 “Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
“Khyanga Capaa phäha khyang he naw ning jah hneng u lü, ning jah jüi u lü nami ngming am dawki ti u lü ami ning jah yawk üng nami jo senki!
23 Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
“Jekyai u lü, hlim u lü, nglam ua, khankhawa nami ngkhengnak vai khawjah awmki. Acukba ami pupa he naw sahma hea khana ana pawh khawiki he ni.
24 Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
“Cunsepi atuh nami bawimangki he nami jo se ve; hlimnak nami yah pängkia kyaki!
25 Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
“Nangmi atuh nami phüki nami jo se ve; nami cawi law khaia kyaki! “Nangmi atuh nami yaiyüngkie nami jo se ve; ktha se lü nami mbawikyap law khaia kyaki!
26 Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
“Khyang he naw ami ning jah mhlünmtai üng nami jo se ve; ami pupa he naw sahma kcang he am niki he khana acunkba ana pawh khawiki he ni.
27 “Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
“Ka ngthu ngjaki he aw, nami ye jawng na u lü ning jah hnengkie ami dawnak vaia pawh u.
28 Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
“Ning jah yünceki he josenak am jah kbe u lü ning jah mkhuimkhaki he jah ktaiyü pe u.
29 Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
“Nami ngbeng vanglam ning jah kbeiki üng vanglam pi dunei pe u, acunüng nami jih ning jah lawhei peki am nami kcu a lawhei vaia pi ä nami mkhyawh vai.
30 Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
“Ning jah kthäheiki üng pe u lü nami ka ning jah lawhei peki ä kthäh be u.
31 Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
“Khyang naw nami khana akdaw a pawh vai nami ngjak hlüa kba khyanga khana akdaw pawh ua.
32 “Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
“Ning jah jawng naki däng nami jawngnak be üng ngkhengnak i nami yah khai ni? Khyangka he naw pi jah jawng naki cun jawng na beki he ni.
33 Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
“Acunüng nami khana dawki hea veia däng nami daw be üng ngkhengnak i nami yah khai ni? Khyangka he naw pi acunkba cui pawh hngaki he ni.
34 Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
“Ning jah thung be thei khai däng üng yah be vaia ngak'uheinak am iyaw nami kpu üng ngkhengnak i nami yah khai ni? Khyangka he naw pi yah be vaia ngak'uhnak am khyangka he üng jah kpu hngaki he ni.
35 Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
“Cunsepi nami ye he jah jawng na u lü ami dawnak vai pawh u lü jah kpu ua, acunkba nami pawh üng ngkhengnak nami yah be vai ä ngai ua. Acunüng Akhlüng säih Mhnama ca hea nami kya khai. Mhnam cun bänak am ksingki la am dawki hea veia pi m'yeneinak taki ni.
36 Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
“Acunakyase nami Pa m'yeneinak am a bea kba khyang m'yenei hnga ua.
37 “Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
“Khyang ä nami jah ngthumkhya pet vai, acunüng ngthumkhyanak am am nami awm khai; ä nami jah mkatei vai, acunüng mkateinak am am nami awm khai; jah mhlät u, acunüng mhlätnak am nami awm hnga khai,
38 Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
“Khyang üng pe u, Pamhnam naw ning jah pe be khai. Akcanga kbäi dänga ä kyase hnawm u lü, khyün u lü, pyep khaia ning jah pe khai he. Nami kbäinak bä am Mhnam naw ning jah kbäi pe be khaia kyaki” a ti.
39 Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
Acunüng Jesuh naw msuimcäpnak mat ami veia pyen lü, “Amikmü naw, amikmü cehpüi thei khai aw? Amikmü naw a cehpüi üngta ani nghngih khuia k'uma am kya khai xawi aw?
40 Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
“Ngtheiki cun mtheikia kthaka am kyäp bawk naw, upi ami ngthei käna jah mtheikia mäih ni ami law kawm.
41 Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
“Ivaia nami mäta mik üng thingmtawn awmki am ngai u lü, nami bena mik üngka mik ek cun nami hmuh ni?
42 Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
“Ikba nami mäta mik üngka thingmtawn am hmuei u lü na benaa mik üngka ‘Na mik ek ning lawh pe vang’ nami ti thei ni?’ Hypocrit he, akcüka nami mäta mik üngka thingmtawn loei ma u lü, acunüng nami benaa mik üngka mik ek nami lawh pet vaia angsinga nami hmu khai.
43 “Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
“Thing kdaw naw akse am ngtheih khawi naw, thing kse pi akdawa am ngtheih khawi naw.
44 Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
“Thing avan a ktheih üng ksinga kyaki. Khyang u naw nghling kpyap üng ktheih am kbit khawi u, u naw kpyap üng capyit am kbit khawi u.
45 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
“Khyang kdaw naw akdaw a mlungmthin üngka akdaw mhluh law khawiki; khyang kse naw akse a mlungmthin üngka akse mhluh law khawiki. Isetiakyaküng a mlungmthin üng beki a mka naw a pyen khawia kyaki.
46 “Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
“Ivai ka ning jah mtheh am bi u lü, ‘Bawipa, Bawipa’ tia nami na khüki ni?
47 Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
“Khyang ka veia law lü ka ngthu ngai lü ka ngthua kba awmki avan cun u am tängki tia kyak üng,
48 Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
lunga khana angkyunga co lü imsaki am tängki ni. Tui däm law lü tui naw acuna im cun tu law se pi lunga khana saka kyase am ngsün lü awmki.
49 Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”
“Ka ngthu ngja lü ka ngthua kba am awmki cun, akhängnak am awmki, mdeka khana imksa am tängki. Tui däm law lü tui naw acuna im cun tu law se angxita kyu lü avan pyehki,” a ti.