< Luka 5 >
1 Siku moja Yesu alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti, na watu wengi walikuwa wamemzunguka wakisongana wanalisikiliza neno la Mungu.
有一次,耶穌站在革乃撒勒湖邊,群眾擁到祂前來要聽天主的道理。
2 Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa; wavuvi wenyewe walikuwa wametoka, wanaosha nyavu zao.
祂看見兩隻船在湖邊停著,漁夫下了船正在洗網。
3 Baada ya Yesu kuingia katika mashua moja, iliyokuwa ya Simoni, alimtaka Simoni aisogeze majini, mbali kidogo na ukingo wa ziwa. Akaketi, akafundisha umati wa watu akiwa ndani ya mashua.
祂上了其中一隻屬於西滿的船,請他把船稍為划開,離開陸地;耶穌就坐下,從船上教訓群眾。
4 Alipomaliza kufundisha, akamwambia Simoni, “Peleka mashua mpaka kilindini, mkatupe nyavu zenu mpate kuvua samaki.”
一講完了,就對西滿說:「划到深處去,撒你們的網捕魚吧! 」
5 Simoni akamjibu, “Bwana, tumejitahidi kuvua samaki usiku kucha bila kupata kitu, lakini kwa kuwa umesema, nitatupa nyavu.”
西滿回答說:「我們已整夜辛苦,毫無所獲;但我們要遵照你的話撒網。」
6 Baada ya kufanya hivyo, wakavua samaki wengi, hata nyavu zao zikaanza kukatika.
他們照樣辦了,網了許多魚,網險些破裂了。
7 Wakawaita wenzao waliokuwa katika mashua nyingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakazijaza mashua zote mbili samaki, hata karibu zingezama.
他們遂招呼別隻船上的同伴來協助他們。他們來到,裝滿了兩隻船,以玫船也幾乎下沈。
8 Simoni Petro alipoona hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu akisema, “Ondoka mbele yangu, ee Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi!”
西滿伯多祿一見這事,就跪伏在耶穌膝前說:「主,請你離開我,因為我是罪人。」
9 Simoni pamoja na wenzake wote walishangaa kwa kupata samaki wengi vile.
西滿和同他一起的人,因為了他們所捕的魚,都驚駭起來。
10 Hali kadhalika Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, waliokuwa wavuvi wenzake Simoni. Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope; tangu sasa utakuwa ukivua watu.”
他的夥伴,即載伯德的兒子雅各伯和若望,也一驚駭。耶穌對西滿說:「不要害怕! 從今以後,你要做捕人的漁夫!」
11 Basi, baada ya kuzileta zile mashua ukingoni mwa ziwa, wakaacha yote, wakamfuata.
他們把船划到了岸邊,就捨棄了一切,跟隨了祂。
12 Ikawa, Yesu alipokuwa katika mmojawapo wa miji ya huko, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamwona. Basi, mtu huyo akaanguka kifudifudi akamwomba Yesu: “Mheshimiwa, ukitaka, waweza kunitakasa.”
有一次,耶穌在一座城裏,看,有一個遍體長了癩的人,見了耶穌,就俯首至地求祂說:「主,你若願意,就能潔淨我。」
13 Yesu akaunyosha mkono wake, akamgusa na kusema, “Nataka, takasika!” Mara ule ukoma ukamwacha.
耶穌便伸手撫摸他說:「我願意,你潔淨了吧! 」癩病就立刻從他身上退去。
14 Yesu akamwamuru: “Usimwambie mtu yeyote; bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama inavyotakiwa na Sheria ya Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
耶穌切切囑咐他不要告訴別人,並說:「但要叫司祭檢驗你,為你的潔淨,獻上梅瑟所規定的,給他們當作證據。」
15 Lakini habari za Yesu zilizidi kuenea kila mahali. Watu makundi mengi wakakusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
祂的名聲更摶揚開了,遂有許多人齊集來聽教,並為自己治好病症。
16 Lakini yeye alikwenda zake mahali pasipo na watu, akawa anasali huko.
耶穌卻退入荒野中去祈禱。
17 Siku moja Yesu alikuwa akifundisha. Mafarisayo na walimu wa Sheria kutoka katika kila kijiji cha Galilaya, Yudea na Yerusalemu, walikuwa wameketi hapo. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kwa ajili ya kuponyea wagonjwa.
有一天,耶穌正在施教,幾個法利賽人和法學士也在座,他們是從加利肋亞和猶太各鄉村及耶路撒冷來的;上主的德能摧迫祂治病。
18 Mara watu wakaja wamemchukua mtu mmoja aliyepooza maungo, amelala kitandani; wakajaribu kumwingiza ndani wamweke mbele ya Yesu.
看,有人用床抬來一個患癱瘓症的人,設法把他抬進去,放在耶穌跟前;
19 Lakini kwa sababu ya wingi wa watu, hawakuweza kuingia ndani. Basi, wakapanda juu ya dari, wakaondoa vigae, wakamshusha huyo aliyepooza pamoja na kitanda chake, wakamweka mbele ya Yesu.
但因人眾多,不得其門而入,遂上了屋頂,從瓦中間,把他連那小床繫到中間,正放在耶穌面前。
20 Yesu alipoona jinsi walivyokuwa na imani kubwa, akamwambia huyo mtu, “Rafiki, umesamehewa dhambi zako.”
耶穌一見他們的信心,就說:「人啊! 你的罪赦了。」
21 Walimu wa Sheria na Mafarisayo wakaanza kujiuliza: “Nani huyu anayemkufuru Mungu kwa maneno yake? Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi ila Mungu peke yake!”
經師和法利塞人開始忖度說:「這人是誰? 竟說褻瀆話! 除了天主一個外,誰能赦罪? 」
22 Yesu alitambua mawazo yao, akawauliza, “Mnawaza nini mioyoni mwenu?
耶穌看透了他們的心思,就向他們說:「你們心裡忖什麼呢?
23 Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi, au kusema, Simama utembee?
什麼比較容易? 是說:你的罪赦了,或是說:起來行走吧!
24 Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kusamehe dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Simama, chukua kitanda chako uende zako nyumbani.”
但為叫你們知道人子在地上有權赦罪─便對癱子說:我給你說:起來,拿起你的小床,回家去吧!
25 Mara, huyo mtu aliyepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda zake nyumbani huku akimtukuza Mungu.
那人立刻在他們在面前站了起來,拿著他躺過的小床,讚頌天主,回去了。
26 Wote wakashangaa na kushikwa na hofu; wakamtukuza Mungu wakisema: “Tumeona maajabu leo.”
眾人十分驚奇,並光榮天主,滿懷恐怖懼說:「今天我們看見了出奇的事。」
27 Baada ya hayo, Yesu akatoka nje, akamwona mtoza ushuru mmoja aitwaye Lawi, ameketi ofisini. Yesu akamwambia, “Nifuate!”
此後,耶穌出去,看見一個稅吏,名叫肋未,在稅關那裡坐著,便對他說:「跟隨我吧!
28 Lawi akaacha yote, akamfuata.
他便捨棄一切,起來跟隨了祂。
29 Kisha Lawi akamwandalia Yesu karamu kubwa nyumbani mwake; na kundi kubwa la watoza ushuru na watu wengine walikuwa wameketi pamoja nao.
肋未在自己家中擺設了盛筵,有許多稅吏和其他的人,與他們一同坐席。
30 Mafarisayo na walimu wa Sheria wakawanung'unikia wafuasi wake wakisema: “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?”
法利賽人和他們的經師就憤憤不平,對祂的門徒說:「你們為什麼同罪人和稅吏一起吃喝? 」
31 Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji daktari, lakini wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa.
耶穌回答他們說:「不是健康的人需要醫生,而是有病的人。
32 Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, ili wapate kutubu.”
我來不是召叫義人,而是召叫罪人悔改。」
33 Watu wengine wakamwambia Yesu, “Wafuasi wa Yohane mbatizaji hufunga mara nyingi na kusali; hata wafuasi wa Mafarisayo hufanya vivyo hivyo. Lakini wafuasi wako hula na kunywa.”
他們又對祂說:「若翰的門徒屢次禁食,行祈禱,法利賽人的門徒也是這樣;而你的卻又吃又喝。」
34 Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwataka wale walioalikwa arusini wafunge hali bwana arusi yuko pamoja nao?
耶穌回答說:「伴郎和新郎在一起的時候,你們豈能叫他們禁食?
35 Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao, na wakati huo ndipo watakapofunga.”
但日子將要來到,當新郎從他們人疲劫去時,在那些日子他們就要禁食了。
36 Yesu akawaambia mfano huu: “Hakuna mtu akataye kiraka cha nguo mpya na kukitia katika vazi kuukuu; kama akifanya hivyo, atakuwa amelikata hilo vazi jipya, na hicho kiraka hakitachukuana na hilo vazi kuukuu.
祂又對他們講比喻說:「沒有人從新衣服撕下一塊作補釘,補在舊衣上的;不然,新的撕破了,而且從新衣上撕下的補釘,與舊的也不相稱。
37 Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; kwani hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, divai itamwagika, na viriba vitaharibika.
也沒有把新酒裝入舊皮囊的,不然,新酒要漲破舊皮囊,酒要流出來,皮囊也破了。
38 Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!
但新酒應裝入新皮囊。
39 Wala hakuna mtu ambaye hutamani kunywa divai mpya baada ya kunywa ya zamani, kwani husema: Ile ya zamani ni nzuri zaidi.”
也沒有人喝著陳酒,願意喝新酒的,因為他說:「還是舊的好。」