< Luka 4 >

1 Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
Jésus, rempli de l’Esprit-Saint, revint du Jourdain, et il fut poussé par l’Esprit dans le désert,
2 Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
pendant quarante jours, en butte aux tentations du diable. Il ne mangea rien durant ces jours-là, et quand ils furent passés, il eut faim.
3 Ndipo Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
Alors le diable lui dit: « Si tu es Fils de Dieu, commande à cette pierre de se changer en pain. »
4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu.”
Jésus lui répondit: « Il est écrit: L’homme ne vit pas seulement de pain, mais de toute parole de Dieu. »
5 Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
Et le diable l’ayant emmené sur une haute montagne, lui montra en un instant tous les royaumes de la terre,
6 “Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
et lui dit: « Je te donnerai toute cette puissance et toute la gloire de ces royaumes; car elle m’a été livrée, et je la donne à qui je veux.
7 Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu.”
Si donc tu te prosternes devant moi, elle sera toute à toi. »
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake.”
Jésus lui répondit: « Il est écrit: Tu adoreras le Seigneur ton Dieu, et tu le serviras lui seul. »
9 Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
Le démon le conduisit encore à Jérusalem, et l’ayant placé sur le pinacle du temple, il lui dit: « Si tu es Fils de Dieu, jettes-toi d’ici en bas.
10 kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
Car il est écrit: Il a été donné pour toi l’ordre à ses anges de te garder,
11 na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe.”
et ils te prendront entre leurs mains, de peur que ton pied ne heurte contre la pierre. »
12 Lakini Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako.”
Jésus lui répondit: « Il a été écrit: Tu ne tenteras pas le Seigneur ton Dieu. »
13 Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
Après l’avoir ainsi tenté de toutes manières, le diable se retira de lui pour un temps.
14 Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
Alors Jésus retourna en Galilée, dans la puissance de l’Esprit, et sa renommée se répandit dans tout le pays d’alentour.
15 Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
Il enseignait dans leurs synagogues, et tous publiaient ses louanges.
16 Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
Étant venu à Nazareth, où il avait été élevé, il entra, selon sa coutume, le jour du sabbat dans la synagogue, et se leva pour faire la lecture.
17 Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
On lui remit le livre du prophète Isaïe; et l’ayant déroulé, il trouva l’endroit où il était écrit:
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
« L’Esprit du Seigneur est sur moi, parce qu’il m’a consacré par son onction, pour porter la bonne nouvelle aux pauvres, et il m’a envoyé guérir ceux qui ont le cœur brisé,
19 na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”
annoncer aux captifs la délivrance, aux aveugles le retour à la vue, pour rendre libres les opprimés, publier l’année favorable du Seigneur. »
20 Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
Ayant roulé le livre, il le rendit au ministre et s’assit; et tous, dans la synagogue, avaient les yeux attachés sur lui.
21 Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo.”
Alors, il commença à leur dire: « Aujourd’hui vos oreilles ont entendu l’accomplissement de cet oracle. »
22 Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
Et tous lui rendaient témoignage, et admirant les paroles de grâce qui sortaient de sa bouche, ils disaient: « N’est-ce pas là le fils de Joseph? »
23 Naye akawaambia, “Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako.”
Et il leur dit: « Sans doute, vous m’alléguerez cet adage: Médecin, guéris-toi toi-même; et vous me direz: Les grandes choses que nous avons ouï dire que vous avez faites à Capharnaüm, faites-les ici dans votre patrie. »
24 Akaendelea kusema, “Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
Et il ajouta: « En vérité, je vous le dis, aucun prophète n’est bien reçu dans sa patrie.
25 Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
Je vous le dis, en vérité, il y avait beaucoup de veuves en Israël aux jours d’Élie, lorsque le ciel fut fermé pendant trois ans et six mois, et qu’il y eut une grande famine dans toute la terre;
26 Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
et pourtant Élie ne fut envoyé à aucune d’elles, mais à une veuve de Sarepta, dans le pays de Sidon.
27 Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria.”
Il y avait de même beaucoup de lépreux en Israël au jours du prophète Elisée; et pourtant aucun d’eux ne fut guéri, mais bien Naaman le Syrien. »
28 Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
En entendant cela, ils furent tous remplis de colère dans la synagogue.
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
Et s’étant levés, ils le poussèrent hors de la ville, et le menèrent jusqu’à un escarpement de la montagne sur laquelle leur ville était bâtie pour le précipiter en bas.
30 Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
Mais lui, passant au milieu d’eux, s’en alla.
31 Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
Il descendit à Capharnaüm, ville de Galilée, et là il enseignait les jours de sabbat.
32 Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
Et sa doctrine les frappait d’étonnement, parce qu’il parlait avec autorité.
33 Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
Il y avait dans la synagogue un homme possédé d’un démon impur, lequel jeta un grand cri,
34 “We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!”
disant: « Laissez-moi, qu’avons-nous à faire avec toi, Jésus de Nazareth? Es-tu venu pour nous perdre? Je sais qui tu es: le Saint de Dieu. »
35 Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: “Nyamaza! Mtoke mtu huyu!” Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
Mais Jésus lui dit d’un ton sévère: « Tais-toi, et sors de cet homme. » Et le démon l’ayant jeté par terre au milieu de l’assemblée, sortit de lui sans lui avoir fait aucun mal.
36 Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, “Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!”
Et tous, saisis de stupeur, se disaient entre eux: « Quelle est cette parole? Il commande avec autorité et puissance aux esprits impurs, et ils sortent! »
37 Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
Et sa renommée se répandait de tous côtés dans le pays.
38 Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
S’étant alors levé, Jésus quitta la synagogue, et entra dans la maison de Simon. Or, la belle-mère de Simon était atteinte d’une grosse fièvre, et ils le prièrent pour elle.
39 Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
Se penchant sur la malade, il commanda à la fièvre, et la fièvre la quitta; et s’étant levée aussitôt, elle se mit à les servir.
40 Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
Lorsque le soleil fut couché, tous ceux qui avaient chez eux des malades, quel que fût leur mal, les lui amenèrent; et Jésus, imposant la main à chacun d’eux, les guérit.
41 Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: “Wewe u Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
Des démons aussi sortaient de plusieurs, criant et disant: « Tu es le Fils de Dieu »; et il les réprimandait pour leur imposer silence, parce qu’ils savaient qu’il était le Christ.
42 Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
Dès que le jour parut, il sortit et s’en alla en un lieu désert. Une foule de gens se mirent à sa recherche, et étant arrivés jusqu’à lui, ils voulaient le retenir, pour qu’il ne les quittât point.
43 Lakini yeye akawaambia, “Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo.”
Mais il leur dit: « Il faut que j’annonce aussi aux autres villes le royaume de Dieu, car je suis envoyé pour cela. »
44 Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.
Et Jésus prêchait dans les synagogues de la Galilée.

< Luka 4 >