< Luka 4 >
1 Yesu alitoka katika mto Yordani akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akaongozwa na Roho mpaka jangwani.
Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led by the Spirit into the wilderness
2 Huko alijaribiwa na Ibilisi kwa muda wa siku arubaini. Wakati huo wote hakula chochote, na baada ya siku hizo akasikia njaa.
for forty days, being tempted by the devil. He ate nothing in those days. When they were completed, he was hungry.
3 Ndipo Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”
The devil said to him, "If you are the Son of God, command this stone to become bread."
4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Mtu haishi kwa mkate tu.”
Jesus answered him, saying, "It is written, 'Humankind cannot live by bread alone.'"
5 Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,
And leading him up to a high mountain, the devil showed him all the kingdoms of the world in a moment of time.
6 “Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza.
The devil said to him, "I will give you all this authority, and their glory, for it has been delivered to me; and I give it to whomever I want.
7 Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu.”
If you therefore will worship before me, it will all be yours."
8 Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake.”
Jesus answered and said to him, "It is written, 'You are to worship the Lord your God, and serve him only.'"
9 Ibilisi akamchukua mpaka Yerusalemu, kwenye mnara wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu,
He led him to Jerusalem, and set him on the pinnacle of the temple, and said to him, "If you are the Son of God, cast yourself down from here,
10 kwa maana imeandikwa: Atawaamuru malaika wake wakulinde,
for it is written, 'He will put his angels in charge of you, to guard you;'
11 na tena, Watakuchukua mikononi mwao usije ukajikwaa mguu wako kwenye jiwe.”
and, 'On their hands they will bear you up, lest perhaps you dash your foot against a stone.'"
12 Lakini Yesu akamjibu, “Imeandikwa: Usimjaribu Bwana Mungu wako.”
And Jesus, answering, said to him, "It is said, 'Do not test the Lord, your God.'"
13 Ibilisi alipokwishamjaribu kwa kila njia, akamwacha kwa muda.
When the devil had completed every temptation, he departed from him until another time.
14 Yesu alirudi Galilaya akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, na habari zake zikaenea katika sehemu zote za jirani.
Jesus returned in the power of the Spirit into Galilee, and news about him spread through all the surrounding area.
15 Naye akawa anawafundisha watu katika masunagogi yao, akasifiwa na wote.
He taught in their synagogues, being praised by all.
16 Basi, Yesu alikwenda Nazareti, mahali alipolelewa, na siku ya Sabato, aliingia katika sunagogi, kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome Maandiko Matakatifu kwa sauti.
He came to Nazareth, where he had been brought up. He entered, as was his custom, into the synagogue on the Sabbath day, and stood up to read.
17 Akapokea kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na akakuta mahali palipoandikwa:
The scroll of the prophet Isaiah was handed to him, and unrolling the scroll, he found the place where it was written,
18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema. Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena; amenituma niwakomboe wanaoonewa,
"The Spirit of the Lord is upon me, because he has anointed me to preach good news to the poor. He has sent me to heal the brokenhearted, to proclaim liberty to the captives, recovering of sight to the blind, to deliver those who are crushed,
19 na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana.”
and to proclaim the acceptable year of the Lord."
20 Baada ya kusoma, akafunga kile kitabu, akampa mtumishi, kisha akaketi; watu wote wakamkodolea macho.
He closed the scroll, gave it back to the attendant, and sat down. The eyes of all in the synagogue were fastened on him.
21 Naye akaanza kuwaambia, “Andiko hili mlilosikia likisomwa, limetimia leo.”
He began to tell them, "Today, this Scripture has been fulfilled in your hearing."
22 Wote wakavutiwa sana naye, wakastaajabia maneno mazuri aliyosema. Wakanena, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”
All testified about him, and wondered at the gracious words which proceeded out of his mouth, and they said, "Is not this Joseph's son?"
23 Naye akawaambia, “Bila shaka mtaniambia msemo huu: Mganga jiponye mwenyewe, na pia mtasema: Yote tuliyosikia umeyafanya kule Kafarnaumu, yafanye hapa pia katika kijiji chako.”
He said to them, "Doubtless you will tell me this parable, 'Physician, heal yourself. Whatever we have heard done at Capernaum, do also here in your hometown.'"
24 Akaendelea kusema, “Hakika nawaambieni, nabii hatambuliwi katika kijiji chake.
He said, "Truly I tell you, no prophet is acceptable in his hometown.
25 Lakini, sikilizeni! Kweli kulikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli nyakati za Eliya. Wakati huo mvua iliacha kunyesha kwa muda wa miaka mitatu na nusu; kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.
But truly I tell you, there were many widows in Israel in the days of Elijah, when the sky was shut up three years and six months, when a great famine came over all the land.
26 Hata hivyo, Eliya hakutumwa kwa mjane yeyote ila kwa mwanamke mjane wa Sarepta, Sidoni.
Elijah was sent to none of them, except to Zarephath, in the land of Sidon, to a woman who was a widow.
27 Tena, katika nchi ya Israeli nyakati za Elisha kulikuwa na wenye ukoma wengi. Hata hivyo, hakuna yeyote aliyetakaswa ila tu Naamani, mwenyeji wa Siria.”
There were many lepers in Israel in the time of Elisha the prophet, yet not one of them was cleansed, except Naaman, the Syrian."
28 Wote waliokuwa katika lile sunagogi waliposikia hayo walikasirika sana.
They were all filled with wrath in the synagogue, as they heard these things.
29 Wakasimama, wakamtoa nje ya mji wao uliokuwa umejengwa juu ya kilima, wakampeleka mpaka kwenye ukingo wa kilima hicho ili wamtupe chini.
They rose up, threw him out of the city, and led him to the brow of the hill that their city was built on, that they might throw him off the cliff.
30 Lakini Yesu akapita katikati yao, akaenda zake.
But he, passing through the midst of them, went his way.
31 Kisha Yesu akashuka mpaka Kafarnaumu katika mkoa wa Galilaya, akawa anawafundisha watu siku ya Sabato.
He came down to Capernaum, a city of Galilee. He was teaching them on the Sabbath day,
32 Wakastaajabia uwezo aliokuwa nao katika kufundisha.
and they were astonished at his teaching, for his word was with authority.
33 Na katika lile sunagogi kulikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na roho ya pepo mchafu; akapiga ukelele wa kuziba masikio:
In the synagogue there was a man who had a spirit of an unclean demon, and he shouted with a loud voice,
34 “We! Yesu wa Nazareti! Kwa nini unatuingilia? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakufahamu wewe ni nani. Wewe ni mjumbe Mtakatifu wa Mungu!”
saying, "Ah. What have we to do with you, Jesus, Nazarene? Have you come to destroy us? I know you who you are — the Holy One of God."
35 Lakini Yesu akamkemea huyo pepo akisema: “Nyamaza! Mtoke mtu huyu!” Basi, huyo pepo baada ya kumwangusha yule mtu chini, akamtoka bila kumdhuru hata kidogo.
Jesus rebuked him, saying, "Be silent, and come out of him." When the demon had thrown him down in their midst, he came out of him, having done him no harm.
36 Watu wote wakashangaa, wakawa wanaambiana, “Hili ni jambo la ajabu, maana kwa uwezo na nguvu anawaamuru pepo wachafu watoke, nao wanatoka!”
Amazement came on all, and they spoke together, one with another, saying, "What is this word? For with authority and power he commands the unclean spirits, and they come out."
37 Habari zake zikaenea mahali pote katika mkoa ule.
News about him went out into every place of the surrounding region.
38 Yesu alitoka katika lile sunagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mmoja, mkwewe Simoni, alikuwa na homa kali; wakamwomba amponye.
He rose up from the synagogue, and entered into Simon's house. Now Simon's mother-in-law was suffering from a high fever, and they appealed to him about her.
39 Yesu akaenda akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, nayo ikamwacha. Mara yule mama akainuka, akawatumikia.
He stood over her, and rebuked the fever; and it left her. Immediately she rose up and served them.
40 Jua lilipokuwa linatua, wote waliokuwa na wagonjwa wao mbalimbali waliwaleta kwake; naye akaweka mikono yake juu ya kila mmoja wao, akawaponya wote.
When the sun was setting, all those who had any sick with various diseases brought them to him; and he laid his hands on every one of them, and healed them.
41 Pepo waliwatoka watu wengi, wakapiga kelele wakisema: “Wewe u Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea, wala hakuwaruhusu kusema, maana walimfahamu kwamba yeye ndiye Kristo.
Demons also came out from many, crying out, and saying, "You are the Son of God." But he rebuked them and did not allow them to speak, because they knew that he was the Christ.
42 Kesho yake asubuhi Yesu aliondoka akaenda mahali pa faragha. Watu wakawa wanamtafuta, na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia ili asiondoke kwao.
When it was day, he departed and went into an uninhabited place, and the crowds looked for him, and came to him, and held on to him, so that he would not go away from them.
43 Lakini yeye akawaambia, “Ninapaswa kuhubiri Habari Njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, maana nilitumwa kwa ajili hiyo.”
But he said to them, "I must proclaim the good news of the Kingdom of God to the other cities also. For this reason I have been sent."
44 Akawa anahubiri katika masunagogi ya Yudea.
And he was preaching in the synagogues of Galilee.