< Luka 3 >

1 Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
Now in the fifteenth year of the reign of Tiberius Caesar, Pontius Pilate being governor of Judaea, and Herod tetrarch of Galilee, and his brother Philip tetrarch of Ituraea and of the region of Trachonitis, and Lysanias tetrarch of Abilene,
2 na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
when Annas and Caiaphas were high-priests, the word of God came to John, the son of Zachariah, in the wilderness.
3 Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
And he came into all the country about the Jordan, preaching the baptism of repentance for the remission of sins;
4 Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
as it is written in the book of the words of Isaiah the prophet: “The voice of one crying in the wilderness, Prepare the way of the Lord, make straight his paths!
5 Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
Every valley shall be filled, and every mountain and hill shall be made low; and the crooked places shall be made straight, and the rough ways smooth;
6 Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu.”
and all flesh shall see the salvation of God.”
7 Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
He said therefore to the multitudes that came forth to be baptized by him, Brood of vipers, who warned you to flee from the coming wrath?
8 Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
Bring forth therefore fruits worthy of repentance; and begin not to say within yourselves, We have Abraham for our father; for I say to you, that God is able out of these stones to raise up children to Abraham.
9 Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
And already also is the axe lying at the root of the trees; every tree therefore that beareth not good fruit is to be cut down, and cast into the fire.
10 Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?”
And the multitudes asked him, saying, What then must we do?
11 Akawajibu, “Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
He answered and said to them, He that hath two coats, let him impart to him that hath none; and he that hath food, let him do likewise.
12 Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
And there came also publicans to be baptized, and said to him, Teacher, what must we do?
13 Naye akawaambia, “Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.”
And he said to them, Exact no more than hath been ordered you.
14 Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.”
And soldiers also asked him, saying, And what must we do? And he said to them, Do violence to no one, accuse no one falsely, and be content with your wages.
15 Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
And while the people were in expectation, and all were considering in their hearts concerning John, whether he were the Christ,
16 Hapo Yohane akawaambia wote, “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
John answered and said to them all, I indeed baptize you with water; but he who is mightier than I is coming, the latchet of whose sandals I am not worthy to loose; he will baptize you in the Holy Spirit and in fire.
17 Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.”
His winnowing-shovel is in his hand to thoroughly cleanse his threshing-floor, and gather the wheat into his garner; but the chaff he will burn up with unquenchable fire.
18 Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
And giving many other exhortations he published the glad tidings to the people.
19 Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
But Herod the tetrarch, being reproved by him on account of Herodias the wife of his brother, and on account of all the evil deeds which Herod had done,
20 Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
added this also to them all, that he shut up John in prison.
21 Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
And it came to pass, when all the people had been baptized, and Jesus also had been baptized, and was praying, that the heaven was opened,
22 na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
and the Holy Spirit descended upon him in a bodily shape as a dove; and a voice came from heaven: “Thou art my beloved Son; with thee I am well pleased.”
23 Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
And Jesus himself was, when he began, about thirty years of age, being, as was supposed, the son of Joseph, who was the son of Heli,
24 Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
who was the son of Matthath, who was the son of Levi, who was the son of Melchi, who was the son of Jannai, who was the son of Joseph,
25 mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
who was the son of Mattathias, who was the son of Amos, who was the son of Nahum, who was the son of Esli, who was the son of Naggai,
26 mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
who was the son of Maath, who was the son of Mattathias, who was the son of Shimei, who was the son of Josech, who was the son of Joda,
27 mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
who was the son of Joanan, who was the son of Rhesa, who was the son of Zerubbabel, who was the son of Shealtiel, who was the son of Neri,
28 mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
who was the son of Melchi, who was the son of Addi, who was the son of Kosam, who was the son of Elmadam, who was the son of Er,
29 mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
who was the son of Jesus, who was the son of Eliezer, who was the son of Jorim, who was the son of Matthath, who was the son of Levi,
30 mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
who was the son of Simeon, who was the son of Judah, who was the son of Joseph, who was the son of Jonam, who was the son of Eliakim,
31 mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
who was the son of Melea, who was the son of Menna, who was the son of Mattatha, who was the son of Nathan, who was the son of David,
32 mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
who was the son of Jesse, who was the son of Obed, who was the son of Boaz, who was the son of Salma, who was the son of Nahshon,
33 mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
who was the son of Amminadab, who was the son of Admin, who was the son of Arni, who was the son of Hezron, who was the son of Pharez, who was the son of Judah,
34 mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
who was the son of Jacob, who was the son of Isaac, who was the son of Abraham, who was the son of Terah, who was the son of Nahor,
35 mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
who was the son of Serug, who was the son of Reu, who was the son of Peleg, who was the son of Eber, who was the son of Shelah,
36 mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
who was the son of Cainan, who was the son of Arphaxad, who was the son of Shem, who was the son of Noah, who was the son of Lamech,
37 mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
who was the son of Methuselah, who was the son of Enoch, who was the son of Jared, who was the son of Mahalaleel, who was the son of Cainan,
38 mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.
who was the son of Enos, who was the son of Seth, who was the son of Adam, who was the son of God.

< Luka 3 >