< Luka 3 >

1 Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
Now in the fifteenth year of the reign of Tiberius Caesar, when Pontius Pilate was governor of Judea, and Herod was tetrarch of Galilee, his brother Philip, tetrarch of Ituraea and Trachonitis, and Lysanias, tetrarch of Abilene;
2 na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
during the high priesthood of Annas and Caiaphas, the word of God came to John, the son of Zachariah, in the Desert.
3 Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
And Johnwent into all the region about the Jordan, preaching a baptism of repentance for the remission of sins.
4 Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
As it is written in the book of the prophet Isaiah. The voice of one crying in the desert, Prepare the way for God, make straight paths for him.
5 Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
Every ravine shall be filled up, Every hill and mountain shall be laid low, The crooked shall be made straight, And the rough roads smooth;
6 Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu.”
And all flesh shall see the salvation of God.
7 Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
So Johnused to say to the crowd of those who were going out to be baptized by him. "You breed of vipers, who has warned you to flee from the wrath to come?
8 Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
Then bring forth fruit befitting your penitence, and do not begin to say to yourselves, "We have Abraham as our father." I tell you that God is able to raise up sons to Abraham out of these stones.
9 Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
And now truly the axe is already laid at the root of the trees. So every tree which is not bearing good fruit is cut down and thrown into the fire."
10 Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?”
And the crowd began to ask him questions. "What shall we do then?" they asked. In reply he said to them.
11 Akawajibu, “Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
"If you have two shirts share with him who has none; and let him who has food do the same."
12 Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
There came to him publicans also to be baptized, and they said to him, "Master, what must we do?"
13 Naye akawaambia, “Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.”
And he said to them, "Exact no more than the sum allowed you."
14 Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.”
The soldiers also repeatedly questioned him, saying, "And we, what shall we do?" "Do not intimidate any one," he replied, "nor lay false charges, and be content with your pay."
15 Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
And while the people were in expectation, and all men were debating in their hearts about John,
16 Hapo Yohane akawaambia wote, “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
whether perhaps he were the Christ, Johnanswered, saying to all of them. "I indeed am baptizing you in water, but One is coming after me, mightier than I, whose shoe-latchet I am not worthy to unloose. He shall baptize you in the Holy Ghost and in fire.
17 Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.”
He has his fan in his hand to cleanse his threshing-floor thoroughly, and to gather the wheat into his storehouse, but the chaff will he burn with unquenchable fire."
18 Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
With many other exhortations then Johndeclared the gospel to the people;
19 Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
but Herod, the Tetrarch, when reproved by him because of Herodias, his brother’s wife, and because of all the wicked deeds that he had done,
20 Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
added yet this above them all that he shut up Johnin prison.
21 Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
Now after all the people had been baptized, and Jesus himself had been baptized and was praying,
22 na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
heaven opened, and the Holy Spirit, in bodily form like a dove, descended upon him. and a voice came out of heaven, saying. "Thou art my Son, dearly beloved; in thee is my delight."
23 Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
And Jesus himself when he began to teach was about thirty years of age. He was the son (as it was supposed) of Joseph, the son of Heli,
24 Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
son of Matthat, son of Levi, son of Melchi,
25 mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
son of Matthias, son of Nahum, son of Esli,
26 mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
son of Mahath, son of Matthias, son of Semein, son of Joseph, son of Joda,
27 mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
son of Johann, son of Resa, son of Zerubbabel, son of Shealtiel, son of Neri,
28 mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
son of Melchi, son of Addi, son of Cosam, son of Elmadam, son of Er,
29 mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
son of Joshua, son of Eliezar, son of Jorim, son of Mathat, son of Levi,
30 mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
son of Symeon, son of Judah, son of Joseph, son of Jonan, son of Eliakim,
31 mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
son of Melea, son of Menna, son of Mattatha, son of Nathan, son of David,
32 mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
son of Jesse, son of Obed, son of Boaz, son of Salmon, son of Nahshon,
33 mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
son of Amminadab, son of Admin, son of Arni, son of Hezron, son of Perez, son of Judah,
34 mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
son of Jacob, son of Isaac, son of Abraham, son of Terah, son of Nahor,
35 mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
son of Serug, son of Reu, son of Peleg, son of Eber, son of Shelah,
36 mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
son of Cainan, son of Arpachshad, son of Shem, son of Noah, son of Lamech,
37 mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
son of Methuselah, son of Enoch, son of Jared, son of Mahalel, son of Kenan,
38 mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.
son of Enos, son of Seth, son of Adam, son of God.

< Luka 3 >