< Luka 3 >

1 Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
凱撒提庇留執政第十五年,般雀比拉多作猶太總督,黑落德作分封侯,他的兄弟斐理伯作依突勒雅和特辣曷地方的分封侯,呂撒尼雅作阿彼肋乃分封侯,
2 na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
亞納斯和蓋作大司祭時,在荒野中有天主的話,傳給匝加利亞的兒子若翰。
3 Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
他遂來走遍約旦河一帶地方,宣講悔改的洗禮,為得罪之赦。
4 Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
正如依撒意亞先知預言書上記載的:『在荒野中有呼號者的聲音:你們當預備上主的道路,修直祂的途徑! 』
5 Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
一切深谷要填滿,一切山丘岳邱陵要剷平,彎曲的要修直,崎嶇的要開成炟途!
6 Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu.”
凡有血肉的,都要看見天主的救援。』
7 Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
於是,他對那些前來要受他洗禮的群眾說:「毒蛇的種類! 誰指教你們逃避那就要來的忿怒?
8 Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
那麼,結與悔改相稱的果實吧! 你們心裡不要以為:我們有亞巴郎為父。我給你們說:天主能從這些石頭中給亞巴郎興起子孫來。
9 Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
斧子已放到樹根上了;凡不結好果子的樹,必被砍倒,投入火中。」
10 Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?”
群眾向他說:「那麼,失們該作什麼呢?
11 Akawajibu, “Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
他答覆他們說:「有兩件內衣的,要分給那沒有的;有食物的,也應照樣做。」
12 Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
稅吏也來受洗,並問說:「師傅,我們該作什麼呢? 」
13 Naye akawaambia, “Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.”
他向他門說:「除給你們規定的外,不要多徵收! 」
14 Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.”
軍人也問說:「我們該作什麼呢? 」他向他門說:「不要勒索人,不要敲詐;對你的糧餉應該知足! 」
15 Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
那時,百姓都在期待(默西亞),為此人人心中推想:也許若翰就是默西亞。
16 Hapo Yohane akawaambia wote, “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
若翰便向眾人說道:「我固然以水洗你們,但是比我強的一位要來,就是解祂的鞋帶,我也不配。祂要以聖神和火洗你們。
17 Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.”
木欣已放在祂手中,祂要揚淨自己的禾場,把麥粒收在倉內;至於糠秕,卻要用不滅的火焚燒。」
18 Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
他還講了許多別的勸言,給百姓傳報喜訊。
19 Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
分封侯黑落德卻為了自已兄弟的妻子黑落狄雅,並為了本人所作的一切惡事,受了若翰的指謫,
20 Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
又在一切的惡事上加了這一件:即把若翰囚在監中。
21 Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
眾百姓受洗後,耶穌也受了洗;當祂祈禱時,天開了;
22 na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
聖神藉著一個形像,如同鴿子,降祂上面;並有聲音從天上說:「你是我的愛子,我因你喜悅。」
23 Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
耶穌開始傳教hapi 時候,大約三十歲,人都以祂為若瑟的兒子:若瑟是赫里的兒子,赫是瑪塔特的兒子,
24 Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
瑪塔特是肋未的兒子,肋未是默爾希的兒子,默爾希是雅乃的兒子,雅乃是約色夫的兒子,
25 mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
約色夫是瑪塔提雅的兒子,瑪塔提雅是阿摩斯的兒子,阿摩斯是納洪的兒子,納洪是厄斯里的兒子,厄斯里是納革的兒子,
26 mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
納革是瑪哈特的兒子,瑪哈特是瑪提雅的兒子,瑪特提雅是史米的兒子,史米是約色黑的兒子,約色黑是約達的兒子,
27 mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
約達是約哈南的兒子,約哈南是肋撒的兒子,肋撒是則魯巴貝耳的兒子,則魯巴貝耳是沙耳提耳的兒子,沙耳提耳是乃黎的兒子,
28 mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
乃黎是默耳希的兒子,默耳希阿狄的兒子,阿狄是科散的兒子,科散是厄耳瑪丹的兒子,厄耳瑪丹是厄爾的兒子,
29 mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
厄爾是耶蘇的兒子,耶蘇是厄里厄則爾的兒子,厄里厄則爾是約楞的兒子,約楞是瑪塔特的兒子,瑪塔特是肋未的兒子,
30 mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
肋未是西默盎的兒子,西默盎是猶達的兒子,猶達是約色夫的兒子,約色夫是約南的兒子,約南是厄耳雅金的兒子,
31 mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
厄耳雅金是默肋阿的兒子,默肋阿是門納的兒子,門納是瑪塔塔的兒子,瑪塔塔是納堂的兒子,納堂是達味的兒子,
32 mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
達味是葉瑟的兒子,葉瑟是敖貝得的兒子,敖貝得是波阿次的兒子,波阿次是撒拉的兒子,撒拉是納赫雄的兒子,
33 mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
納赫雄是阿米納達的兒子,阿米納達是阿得明的兒子,阿得明是阿爾的兒子,是阿爾是赫茲龍的兒子,赫茲龍是培勒茲的兒子,培勒茲是猶大的兒子,
34 mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
猶大是雅各伯的兒子,雅各伯是依撒格的兒子,依撒格是亞巴郎的兒子,亞巴郎是特辣黑的兒子,特辣黑是納曷爾的兒子,
35 mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
納曷爾是色魯格的兒子,色魯格是勒伍的兒子,勒伍是培勒格的兒子,培勒格是厄貝爾的兒子,厄貝爾是舍拉的兒子,
36 mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
舍拉是刻南的兒子,刻南是阿帕革沙的兒子,阿帕革沙是閃的兒子,閃是諾厄的兒子,諾厄是拉默客的兒子,
37 mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
拉默客是默突舍拉的兒子,默突舍拉是哈諾客的兒子,哈諾客是耶勒得的兒子,耶勒得是瑪拉勒耳的兒子,瑪拉勒耳是刻南的兒子,
38 mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.
刻南是厄諾士的兒子,厄諾士是舍特的兒子,舍特是亞當的兒子,亞當是天主的兒子。

< Luka 3 >