< Luka 22 >
1 Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
La fête des pains sans levain, appelée la Pâque, approchait.
2 Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
Et les principaux sacrificateurs et les scribes cherchaient comment ils pourraient faire mourir Jésus; car ils craignaient le peuple.
3 Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
Or, Satan entra dans Judas, nommé Iscariote, qui était du nombre des Douze.
4 Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
Judas alla trouver les principaux sacrificateurs et les chefs des gardes, pour s'entendre avec eux sur les moyens de le leur livrer.
5 Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
Ceux-ci, remplis de joie, lui promirent de lui donner de l'argent.
6 Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
Il se mit d'accord avec eux, et il cherchait une occasion favorable pour livrer Jésus à l'insu de la foule.
7 Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
Le jour des pains sans levain, où l'on devait immoler la Pâque, étant arrivé,
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
Jésus envoya Pierre et Jean, et il leur dit: Allez nous préparer la Pâque, afin que nous la mangions.
9 Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
Ils lui dirent: Où veux-tu que nous la préparions?
10 Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
Il leur répondit: Lorsque vous entrerez dans la ville, vous rencontrerez un homme portant une cruche d'eau; suivez-le dans la maison où il entrera,
11 Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
et dites au maître de la maison: Le Maître te fait dire: Où se trouve la salle dans laquelle je dois manger la Pâque avec mes disciples?
12 Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
Et il vous montrera une grande chambre haute, toute meublée; préparez-y ce qu'il faut.
13 Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
Ils s'en allèrent et trouvèrent les choses comme Jésus le leur avait dit; et ils préparèrent la Pâque.
14 Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
Quand l'heure fut venue, il se mit à table, et les apôtres avec lui.
15 Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
Puis il leur dit: J'ai fort désiré de manger cette Pâque avec vous, avant que je souffre.
16 Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
Car, je vous le déclare, je ne la mangerai plus, jusqu'à ce qu'elle soit accomplie dans le royaume de Dieu.
17 Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
Et, ayant pris une coupe et rendu grâces, il dit: Prenez ceci, et partagez-le entre vous.
18 Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
Car, je vous le déclare, désormais je ne boirai plus du fruit de la vigne, jusqu'à ce que le royaume de Dieu soit venu.
19 Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
Puis il prit du pain, et, après avoir rendu grâces, il le rompit et le leur donna, en disant: Ceci est mon corps, qui est donné pour vous; faites ceci en mémoire de moi.
20 Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
De même, après avoir soupé, il leur donna la coupe, en disant: Cette coupe est la nouvelle alliance en mon sang, qui est répandu pour vous.
21 “Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
Au reste, la main de celui qui me trahit est près de moi: il est assis à cette table!
22 Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
En ce qui concerne le Fils de l'homme, il s'en va, conformément à ce qui a été arrêté; mais malheur à cet homme, par qui il est trahi!
23 Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
Alors ils se mirent à se demander les uns aux autres, quel était donc celui d'entre eux qui ferait cela.
24 Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
Il s'éleva aussi parmi eux une contestation, pour savoir lequel d'entre eux devait être regardé comme le plus grand.
25 Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
Mais Jésus leur dit: Les rois des nations leur commandent en maîtres, et ceux qui exercent l'autorité sur elles sont appelés bienfaiteurs.
26 Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
Pour vous, ne faites pas ainsi; mais, que le plus grand parmi vous soit comme le plus petit, et celui qui gouverne, comme celui qui sert.
27 Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
Car lequel est le plus grand, celui qui est à table, ou celui qui sert? N'est-ce pas celui qui est à table? Moi pourtant, je suis au milieu de vous comme celui qui sert.
28 “Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
Quant à vous, vous avez persévéré avec moi dans mes épreuves,
29 na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
et je dispose du royaume en votre faveur, comme mon Père en a disposé pour moi,
30 Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
afin que vous mangiez et que vous buviez à ma table dans mon royaume, et que vous soyez assis sur des trônes, jugeant les douze tribus d'Israël.
31 “Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
Simon, Simon, voici que Satan a demandé à vous passer au crible comme le blé.
32 Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
Mais j'ai prié pour toi, afin que ta foi ne défaille point. Toi donc, quand tu seras converti, affermis tes frères.
33 Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
Pierre lui dit: Seigneur, je suis prêt à aller avec toi, et en prison et à la mort!
34 Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
Jésus répondit: Pierre, je te le déclare, le coq ne chantera pas aujourd'hui, que tu n'aies par trois fois nié de me connaître.
35 Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
Puis il ajouta: Lorsque je vous ai envoyés sans bourse, sans sac et sans chaussures, avez-vous manqué de quelque chose? Ils répondirent: De rien.
36 Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
Mais maintenant, leur dit-il, que celui qui a une bourse, la prenne, et de même, celui qui a un sac; et que celui qui n'a point d'épée, vende son manteau et en achète une.
37 Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
Car, je vous le déclare, il faut que s'accomplisse en ma personne ce qui est écrit: «Il a été mis au rang des malfaiteurs.» En effet, ce qui me concerne touche à sa fin.
38 Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
Ils dirent: Seigneur, voici deux épées. Il leur répondit: Cela suffit.
39 Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
Puis, Jésus sortit et alla, selon sa coutume, à la montagne des Oliviers; et les disciples le suivirent.
40 Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
Quand il fut arrivé en ce lieu, il leur dit: Priez, afin que vous ne tombiez pas dans la tentation.
41 Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
Alors il s'éloigna d'eux d'un jet de pierre environ, et, s'étant mis à genoux, il priait,
42 “Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
disant: Père, si tu voulais éloigner de moi cette coupe! Toutefois, que ta volonté soit faite et non la mienne!
43 Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
Et un ange lui apparut du ciel, qui le fortifiait.
44 Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
Étant en agonie, il priait plus instamment, et sa sueur devint comme de grosses gouttes de sang qui tombaient à terre.
45 Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
Après avoir prié, il se leva et revint vers les disciples, qu'il trouva endormis de tristesse.
46 Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
Et il leur dit: Pourquoi dormez-vous? Levez-vous, et priez, afin que vous ne tombiez pas dans la tentation.
47 Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
Comme il parlait encore, une troupe parut. Celui qu'on nommait Judas, l'un des Douze, marchait devant elle, et il s'approcha de Jésus pour lui donner un baiser.
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
Jésus lui dit: Judas, tu trahis le Fils de l'homme par un baiser!
49 Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
Alors ceux qui étaient avec lui, voyant ce qui allait arriver, lui dirent: Seigneur, frapperons-nous de l'épée?
50 Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
Et l'un d'eux frappa le serviteur du souverain sacrificateur, et il lui emporta l'oreille droite.
51 Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
Mais Jésus, prenant la parole, dit: Arrêtez un moment! Et, ayant touché l'oreille de cet homme, il le guérit.
52 Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
Puis Jésus dit aux principaux sacrificateurs, aux chefs des gardes du temple et aux anciens, qui étaient venus vers lui: Vous êtes sortis avec des épées et des bâtons, comme après un brigand.
53 Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
J'étais tous les jours dans le temple avec vous, et vous n'avez pas mis la main sur moi. Mais c'est ici votre heure et la puissance des ténèbres.
54 Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
Alors, ils le saisirent et l'emmenèrent; et ils le firent entrer dans la maison du souverain sacrificateur, Pierre suivait de loin.
55 Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
Ils allumèrent du feu au milieu de la cour et s'assirent ensemble; et Pierre s'assit parmi eux.
56 Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
Une servante, le voyant assis près du feu et le regardant attentivement, dit: Cet homme était aussi avec lui.
57 Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
Mais il renia Jésus, en disant: Femme, je ne le connais point!
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
Un peu après, un autre, l'ayant vu, lui dit: Toi aussi, tu es de ces gens-là! Pierre répondit à cet homme: Je n'en suis pas!
59 Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
Environ une heure plus tard, un autre assurait la même chose et disait: Certainement, cet homme était aussi avec lui; car il est Galiléen.
60 Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
Mais Pierre reprit: homme, je ne sais ce que tu veux dire! Au même instant, comme il parlait encore, le coq chanta;
61 Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
et le Seigneur, s'étant retourné, regarda Pierre. Pierre se ressouvint de la parole que le Seigneur lui avait dite: Avant que le coq chante aujourd'hui, tu me renieras trois fois.
62 Hapo akatoka nje, akalia sana.
Et étant sorti, il pleura amèrement.
63 Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
Or, ceux qui gardaient Jésus se moquaient de lui et le frappaient;
64 Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
et, lui ayant couvert le visage, ils lui disaient: Prophétise, devine qui t'a frappé!
65 Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
Et ils proféraient beaucoup d'autres injures contre lui.
66 Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
Quand le jour fut venu, les anciens du peuple, les principaux sacrificateurs et les scribes se réunirent, et ils le firent venir dans leur Sanhédrin.
67 Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
Ils lui dirent: Si tu es le Christ, déclare-le-nous. Il leur répondit: Si je le disais, vous ne le croiriez pas;
68 na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
et si je vous interrogeais, vous ne me répondriez pas.
69 Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
Mais désormais le Fils de l'homme sera assis à la droite du Dieu tout-puissant.
70 Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
Ils dirent tous: Tu es donc le Fils de Dieu? Il leur répondit: Vous dites vous-mêmes que je le suis.
71 Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”
Alors ils s'écrièrent: Qu'avons-nous encore besoin de témoignage? Nous venons nous-mêmes de l'entendre de sa propre bouche!