< Luka 21 >

1 Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
Iyesus dambaan kawdek't b́s'ilfere gaaletswots bo imiruo [mebo] ms'watiy dek'eyiru sat'nots bo gedfere bek' b́k'r.
2 akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
Mank'o t'owu mááts iku, git santimu wotit gizo sat'nots b ged'fere bek' b́k'ri.
3 Basi, akasema, “Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
Hank'owere bíet, «Ariko itsh keewiruwe, t'owmáátsan jametsoniyere bogsh dek'at imranee.
4 Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi.”
Bo boimye bogalotse oortsoniye, bimo t'owu wotefetsatniye eegor b ooride'awon b detsts jamo imranee.»
5 Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
Ash ik ikuwots, «Ik'i maa han awuk'owe b́sheengi? Gizi shaawo kishit mang shútsuwotsnat Ik'osh t'ints sheeng keewone baats b́wutsi» et fetst bo keeweyiri b́ teshi.
6 “Haya yote mnayoyaona—zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
Ernmó Iyesus «It bek'iru jaman shútso shútsats kororeyar b́oorawu dúro weetuwe, shúts jamanots ik aawu gaahitune.»
7 Basi, wakamwuliza, “Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?”
Bowere «Danifono! man b́wotit awure? Hanuwere wotosh b́t'intsok'o eegi milktoneya nodaneti?» ett boaati.
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
Iyesus hank'o ett boosh bíaaniy, «It shelawok'o it atso korde'ere! ayuwots ‹Taa Krstos taane! hambe! bíaawo t'inre!› err t shutson weetune, bo shuutso sha'ak'ayere.
9 Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado.”
Kes'i jangonat dimbiron it shishor tek' k'ayere, shinshino man b́woto geyife, ernmó b́s'uwo manoor woteratse.»
10 Halafu akaendelea kusema: “Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
Manats dabt Iyesus hank'owa bíet, «Ash asho ashaashats, naasho naashats tuwitwee.
11 Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
B́ be beewoke kup' wotts dats shek'ewo, k'ak'onat maryi shodon wotituwe. Shatit keewuwotsnat mlikit een eenuwotsn darotse be'etúne.
12 Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
Ernmó jaman b́ woteftsere shino ash ashuwots itn detsetúno, gishitúno, ayhudi Ik' k'oni moonat tipi mootso beshide iti imetuno, t shútsi jangosho itn naash naashonat altswotsok de'e ametunee.
13 Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
Hanuwere t shútsi jango gawosh itsh iki sheeng b́wutsiti.
14 Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
Mansh itats bodet s'amiyewor it aanit keewosh it kic'erawok'o shino t'iwints de'ere.
15 kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
It balangaruwotsitse konuwor falr k'efo b́ bayaw nononat dani telefo taa itsh imetuwe.
16 Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
Iti ind nihuwtsnat it eshuwots, it jaguwotsnat it tohuwotswor bo oorerawo iti beshider imetune, itiste ik ikuwotsi úd'etuwe.
17 Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
T shútsi jangosh ash jami shinatse shit'eek wotitute.
18 Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
Ernmó it took s'iratse ik s'iru dab t'afratsane.
19 Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
It k'amon it kashu kashidek'etute» bí et.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
Manats dabt Iyesus hank'owa bíet, «Iyerusalem t'alaton gúrde bobefre it bek'or b t'afo b́ bodtsok'o dande'ere,
21 Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
Manoor Yihud datsatse fa'uwots guromants woc'no, kitutse fa'uwots biitse keeno, kituniyere úratse fa'uwots kitumand kind k'ayno.
22 Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
T'afan jangosh guut'etso shin bek'on keewetso b́ wotituwok'o hanweer wershikonat fayi dúrone.
23 Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
Manots, na'i mac'uwotsnat s'aats ishiru na'i induwotssh indowe boosha! datsatse kic'i gondo wotituwe, ash manotsatse Ik'i fayo weetuwe.
24 Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
Boyitsnowere ayuwots shik goradon úd'etuno, katsuwotsuwere kisho imr dats datsats dametuno, Ik'i ash woterawwots dúro b́ s'uufetsosh Iyerusalem Ik'i ash woterawwotsn net'etk wotitwaniye.»
25 “Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
Manats dabt Iyesus hank'o bíeti, «Aawonat aashitson, k'enuwotsatsnoor adits milikituwots be'etúno, datsatsnowere ash jamwots aats k'aronat b́ jongo tek'iyiru k'aratse tuutson sharr kic'ituno.
26 Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
Datsats weet keewo kotoke ashuwots shatoon k'ewitúnee, manoor daritsi angwots shek'etúno,
27 Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
Maniye hakon Ash na'o angi eenonat dawunots wotde'er b́waafere ashuwots bek'etúno.
28 Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”
Jamanots woto de'e botuwor it kashit aawo b́ bodtsotse dambaan kaaw de'er s'iilere.»
29 Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.
Manats dabt Iyesus jewurets keewuman boosh b́ keewu, «Belesi mitonat k'osh mituwotsi t'intsde s'iilere,
30 Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
Bo maaro ato de'e b́tuwo it bek'tsok'on k'aawo b́ t'intsok'o danfte.
31 Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
Mank'oon jaman woto de b́tuwo it bek'or Ik'i mengsto wosh b́karntsok'owo dande'ere.
32 Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
«Ariko itsh keewirwe, jaman b́ s'eenfetso and dúri s'oot'an besheratse.
33 Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
Daronat datson beshitune, t keewonmo besheratse.»
34 “Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
Manats dabt Iyesus hank'o b́ et «Móónat úshi ayon, mashon, ay finon maawonat datsatsi beyosh kic'on it nibo ay b́ maawrawok'o it atso korde'ere! Maniye okoon aawuman kambok'o gawerawon iti deshdek'etwe.
35 Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
Manots aawuman datsatse daatset ash jamwotsi gawerawo kambok'o deshdek'etwe.
36 Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu.”
Mansh, weet gond keewu jamatse oorosh ango it daatsituwok'o aani Ash Na'o shinatse ned'osh it falituwok'o jam aawo Ik' k'onoke kup'ore.»
37 Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
Iyesus aaw aawon Ik'i mootse b́ daniyfo, datso b́ ilor Debrezeyit gurats kede b́ k'eefoni.
38 Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.
Ash jamo Iyesusi k'ebosh guuron Ik'i mootsere b́ maants bo amfoni.

< Luka 21 >