< Luka 20 >
1 Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
Et il arriva, l’un de ces jours, comme il enseignait le peuple dans le temple et évangélisait, que les principaux sacrificateurs et les scribes survinrent avec les anciens.
2 wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
Et ils lui parlèrent, disant: Dis-nous par quelle autorité tu fais ces choses, ou qui est celui qui t’a donné cette autorité?
3 Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
Et répondant, il leur dit: Je vous demanderai, moi aussi, une chose, et dites-moi:
4 mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
Le baptême de Jean était-il du ciel, ou des hommes?
5 Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
Et ils raisonnèrent entre eux, disant: Si nous disons: Du ciel, il dira: Pourquoi ne l’avez-vous pas cru?
6 Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
Et si nous disons: Des hommes, tout le peuple nous lapidera, car il est persuadé que Jean était un prophète.
7 Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
Et ils répondirent qu’ils ne savaient pas d’où [il était].
8 Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
Et Jésus leur dit: Moi non plus, je ne vous dis pas par quelle autorité je fais ces choses.
9 Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
Et il se mit à dire au peuple cette parabole: Un homme planta une vigne, et la loua à des cultivateurs, et s’en alla hors du pays pour longtemps.
10 Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
Et en la saison, il envoya un esclave aux cultivateurs, afin qu’ils lui donnent du fruit de la vigne; mais les cultivateurs, l’ayant battu, le renvoyèrent à vide.
11 Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
Et il envoya encore un autre esclave; mais l’ayant battu lui aussi, et l’ayant traité ignominieusement, ils le renvoyèrent à vide.
12 Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
Et il en envoya encore un troisième; mais ils blessèrent aussi celui-ci, et le jetèrent dehors.
13 Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
Et le maître de la vigne dit: Que ferai-je? J’enverrai mon fils bien-aimé; peut-être que, quand ils verront celui-ci, ils le respecteront.
14 Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
Mais quand les cultivateurs le virent, ils raisonnèrent entre eux, disant: Celui-ci est l’héritier, tuons-le, afin que l’héritage soit à nous.
15 Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
Et l’ayant jeté hors de la vigne, ils le tuèrent. Que leur fera donc le maître de la vigne?
16 Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
Il viendra et fera périr ces cultivateurs, et donnera la vigne à d’autres. Et l’ayant entendu, ils dirent: Qu’ainsi n’advienne!
17 Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
Et lui, les regardant, dit: Qu’est-ce donc que ceci qui est écrit: « La pierre que ceux qui bâtissaient ont rejetée, celle-là est devenue la maîtresse pierre du coin »?
18 Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
Quiconque tombera sur cette pierre, sera brisé; mais celui sur qui elle tombera, elle le broiera.
19 Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
Et les principaux sacrificateurs et les scribes cherchèrent, en cette heure même, à mettre les mains sur lui; et ils craignaient le peuple, car ils connurent qu’il avait dit cette parabole contre eux.
20 Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
Et l’observant, ils envoyèrent des agents secrets, qui feignaient d’être justes, pour le surprendre en [quelque] parole, de manière à le livrer au magistrat et au pouvoir du gouverneur.
21 Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
Et ils l’interrogèrent, disant: Maître, nous savons que tu dis et que tu enseignes justement, et que tu n’as point égard à l’apparence des personnes, mais que tu enseignes la voie de Dieu avec vérité.
22 Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
Nous est-il permis de payer le tribut à César, ou non?
23 Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
Et s’apercevant de leur perfidie, il leur dit: Pourquoi me tentez-vous?
24 “Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
Montrez-moi un denier; de qui a-t-il l’image et l’inscription? Et répondant, ils dirent: De César.
25 Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
Et il leur dit: Rendez donc les choses de César à César, et les choses de Dieu à Dieu.
26 Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
Et ils ne pouvaient le surprendre dans ses paroles devant le peuple; et étonnés de sa réponse, ils se turent.
27 Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
Et quelques-uns des sadducéens, qui nient qu’il y ait une résurrection, s’approchèrent, et l’interrogèrent,
28 “Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
disant: Maître, Moïse nous a écrit, que si le frère de quelqu’un meurt, ayant une femme, et qu’il meure sans enfants, son frère prenne la femme et suscite de la postérité à son frère.
29 Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
Il y avait donc sept frères; et le premier, ayant pris une femme, mourut sans enfants;
30 Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
et le second [prit la femme, et celui-ci aussi mourut sans enfants];
31 na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
et le troisième la prit, et de même aussi les sept: ils ne laissèrent pas d’enfants et moururent;
32 Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
et après eux tous la femme aussi mourut.
33 Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
Dans la résurrection donc, duquel d’entre eux sera-t-elle la femme, car les sept l’ont eue pour femme?
34 Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn )
Et Jésus leur dit: Les fils de ce siècle se marient et sont donnés en mariage; (aiōn )
35 lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn )
mais ceux qui seront estimés dignes d’avoir part à ce siècle-là et à la résurrection d’entre les morts, ne se marient ni ne sont donnés en mariage, (aiōn )
36 Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
car aussi ils ne peuvent plus mourir; car ils sont semblables aux anges, et ils sont fils de Dieu, étant fils de la résurrection.
37 Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
Or que les morts ressuscitent, Moïse même l’a montré, au [titre]: “Du buisson”, quand il appelle le Seigneur: le Dieu d’Abraham, et le Dieu d’Isaac, et le Dieu de Jacob.
38 Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
Or il n’est pas le Dieu des morts, mais des vivants; car pour lui tous vivent.
39 Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
Et quelques-uns des scribes, répondant, dirent: Maître, tu as bien dit.
40 Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
Et ils n’osèrent plus l’interroger sur rien.
41 Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
Et il leur dit: Comment dit-on que le Christ est fils de David?
42 Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
Et David lui-même dit, dans le livre des Psaumes: « Le Seigneur a dit à mon seigneur: Assieds-toi à ma droite,
43 mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
jusqu’à ce que je mette tes ennemis pour marchepied de tes pieds ».
44 Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
David donc l’appelle seigneur; et comment est-il son fils?
45 Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
Et comme tout le peuple écoutait, il dit à ses disciples:
46 “Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
Soyez en garde contre les scribes, qui se plaisent à se promener en longues robes, et qui aiment les salutations dans les places publiques, et les premiers sièges dans les synagogues, et les premières places dans les repas;
47 Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”
qui dévorent les maisons des veuves, et pour prétexte font de longues prières; – ceux-ci recevront une sentence plus sévère.