< Luka 2 >

1 Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
อปรญฺจ ตสฺมินฺ กาเล ราชฺยสฺย สรฺเวฺวษำ โลกานำ นามานิ เลขยิตุมฺ อคสฺตไกสร อาชฺญาปยามาสฯ
2 Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
ตทนุสาเรณ กุรีณิยนามนิ สุริยาเทศสฺย ศาสเก สติ นามเลขนํ ปฺราเรเภฯ
3 Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
อโต เหโต รฺนาม เลขิตุํ สรฺเวฺว ชนา: สฺวียํ สฺวียํ นครํ ชคฺมุ: ฯ
4 Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
ตทานีํ ยูษผฺ นาม เลขิตุํ วาคฺทตฺตยา สฺวภารฺยฺยยา ครฺพฺภวตฺยา มริยมา สห สฺวยํ ทายูท: สชาติวํศ อิติ การณาทฺ คาลีลฺปฺรเทศสฺย นาสรตฺนคราทฺ
5 Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
ยิหูทาปฺรเทศสฺย ไพเตฺลหมาขฺยํ ทายูทฺนครํ ชคามฯ
6 Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
อนฺยจฺจ ตตฺร สฺถาเน ตโยสฺติษฺฐโต: สโต รฺมริยม: ปฺรสูติกาล อุปสฺถิเต
7 akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
สา ตํ ปฺรถมสุตํ ปฺราโสษฺฏ กินฺตุ ตสฺมินฺ วาสคฺฤเห สฺถานาภาวาทฺ พาลกํ วสฺเตฺรณ เวษฺฏยิตฺวา โคศาลายำ สฺถาปยามาสฯ
8 Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
อนนฺตรํ เย กิยนฺโต เมษปาลกา: สฺวเมษวฺรชรกฺษาไย ตตฺปฺรเทเศ สฺถิตฺวา รชนฺยำ ปฺรานฺตเร ปฺรหริณ: กรฺมฺม กุรฺวฺวนฺติ,
9 Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
เตษำ สมีปํ ปรเมศฺวรสฺย ทูต อาคโตฺยปตเสฺถา; ตทา จตุษฺปารฺเศฺว ปรเมศฺวรสฺย เตชส: ปฺรกาศิตตฺวาตฺ เต'ติศศงฺกิเรฯ
10 Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
ตทา ส ทูต อุวาจ มา ไภษฺฏ ปศฺยตาทฺย ทายูท: ปุเร ยุษฺมนฺนิมิตฺตํ ตฺราตา ปฺรภุ: ขฺรีษฺโฏ'ชนิษฺฏ,
11 Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
สรฺเวฺวษำ โลกานำ มหานนฺทชนกมฺ อิมํ มงฺคลวฺฤตฺตานฺตํ ยุษฺมานฺ ชฺญาปยามิฯ
12 Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.”
ยูยํ (ตตฺสฺถานํ คตฺวา) วสฺตฺรเวษฺฏิตํ ตํ พาลกํ โคศาลายำ ศยนํ ทฺรกฺษฺยถ ยุษฺมานฺ ปฺรตีทํ จิหฺนํ ภวิษฺยติฯ
13 Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
ทูต อิมำ กถำ กถิตวติ ตตฺรากสฺมาตฺ สฺวรฺคียา: ปฺฤตนา อาคตฺย กถามฺ อิมำ กถยิเตฺวศฺวรสฺย คุณานนฺววาทิษุ: , ยถา,
14 “Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!”
สรฺโวฺวรฺทฺวฺวไสฺถรีศฺวรสฺย มหิมา สมฺปฺรกาศฺยตำฯ ศานฺติรฺภูยาตฺ ปฺฤถิวฺยาสฺตุ สนฺโตษศฺจ นรานฺ ปฺรติ๚
15 Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.”
ตต: ปรํ เตษำ สนฺนิเธ รฺทูตคเณ สฺวรฺคํ คเต เมษปาลกา: ปรสฺปรมฺ อเวจนฺ อาคจฺฉต ปฺรภุ: ปรเมศฺวโร ยำ ฆฏนำ ชฺญาปิตวานฺ ตสฺยา ยาถรฺยํ ชฺญาตุํ วยมธุนา ไพเตฺลหมฺปุรํ ยาม: ฯ
16 Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
ปศฺจาตฺ เต ตูรฺณํ วฺรชิตฺวา มริยมํ ยูษผํ โคศาลายำ ศยนํ พาลกญฺจ ททฺฤศุ: ฯ
17 Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
อิตฺถํ ทฺฤษฺฏฺวา พาลกสฺยารฺเถ โปฺรกฺตำ สรฺวฺวกถำ เต ปฺราจารยาญฺจกฺรุ: ฯ
18 Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
ตโต เย โลกา เมษรกฺษกาณำ วทเนภฺยสฺตำ วารฺตฺตำ ศุศฺรุวุเสฺต มหาศฺจรฺยฺยํ เมนิเรฯ
19 Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
กินฺตุ มริยมฺ เอตตฺสรฺวฺวฆฏนานำ ตาตฺปรฺยฺยํ วิวิจฺย มนสิ สฺถาปยามาสฯ
20 Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
ตตฺปศฺจาทฺ ทูตวิชฺญปฺตานุรูปํ ศฺรุตฺวา ทฺฤษฺฏฺวา จ เมษปาลกา อีศฺวรสฺย คุณานุวาทํ ธนฺยวาทญฺจ กุรฺวฺวาณา: ปราวฺฤตฺย ยยุ: ฯ
21 Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
อถ พาลกสฺย ตฺวกฺเฉทนกาเล'ษฺฏมทิวเส สมุปสฺถิเต ตสฺย ครฺพฺภสฺถิเต: ปุรฺวฺวํ สฺวรฺคียทูโต ยถาชฺญาปยตฺ ตทนุรูปํ เต ตนฺนามเธยํ ยีศุริติ จกฺริเรฯ
22 Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
ตต: ปรํ มูสาลิขิตวฺยวสฺถายา อนุสาเรณ มริยม: ศุจิตฺวกาล อุปสฺถิเต,
23 Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”
"ปฺรถมช: สรฺวฺว: ปุรุษสนฺตาน: ปรเมศฺวเร สมรฺปฺยตำ," อิติ ปรเมศฺวรสฺย วฺยวสฺถยา
24 Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
ยีศุํ ปรเมศฺวเร สมรฺปยิตุมฺ ศาสฺตฺรียวิธฺยุกฺตํ กโปตทฺวยํ ปาราวตศาวกทฺวยํ วา พลึ ทาตุํ เต ตํ คฺฤหีตฺวา ยิรูศาลมมฺ อายยุ: ฯ
25 Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
ยิรูศาลมฺปุรนิวาสี ศิมิโยนฺนามา ธารฺมฺมิก เอก อาสีตฺ ส อิสฺราเยล: สานฺตฺวนามเปกฺษฺย ตเสฺถา กิญฺจ ปวิตฺร อาตฺมา ตสฺมินฺนาวิรฺภูต: ฯ
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
อปรํ ปฺรภุณา ปรเมศฺวเรณาภิษิกฺเต ตฺราตริ ตฺวยา น ทฺฤษฺเฏ ตฺวํ น มริษฺยสีติ วากฺยํ ปวิเตฺรณ อาตฺมนา ตสฺม ปฺรากถฺยตฯ
27 Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
อปรญฺจ ยทา ยีโศ: ปิตา มาตา จ ตทรฺถํ วฺยวสฺถานุรูปํ กรฺมฺม กรฺตฺตุํ ตํ มนฺทิรมฺ อานินฺยตุสฺตทา
28 Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
ศิมิโยนฺ อาตฺมน อากรฺษเณน มนฺทิรมาคตฺย ตํ โกฺรเฑ นิธาย อีศฺวรสฺย ธนฺยวาทํ กฺฤตฺวา กถยามาส, ยถา,
29 “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
เห ปฺรโภ ตว ทาโสยํ นิชวากฺยานุสารต: ฯ อิทานีนฺตุ สกลฺยาโณ ภวตา สํวิสฺฤชฺยตามฺฯ
30 Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
ยต: สกลเทศสฺย ทีปฺตเย ทีปฺติรูปกํฯ
31 ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
อิสฺราเยลียโลกสฺย มหาเคารวรูปกํฯ
32 Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”
ยํ ตฺรายกํ ชนานานฺตุ สมฺมุเข ตฺวมชีชน: ฯ เสอว วิทฺยเต'สฺมากํ ธฺรวํ นยนนโคจเร๚
33 Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
ตทานีํ เตโนกฺตา เอตา: สกลา: กถา: ศฺรุตฺวา ตสฺย มาตา ยูษผฺ จ วิสฺมยํ เมนาเตฯ
34 Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
ตต: ปรํ ศิมิโยนฺ เตภฺย อาศิษํ ทตฺตฺวา ตนฺมาตรํ มริยมมฺ อุวาจ, ปศฺย อิสฺราเยโล วํศมเธฺย พหูนำ ปาตนาโยตฺถาปนาย จ ตถา วิโรธปาตฺรํ ภวิตุํ, พหูนำ คุปฺตมโนคตานำ ปฺรกฏีกรณาย พาลโกยํ นิยุกฺโตสฺติฯ
35 na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”
ตสฺมาตฺ ตวาปิ ปฺราณา: ศูเลน วฺยตฺสฺยนฺเตฯ
36 Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
อปรญฺจ อาเศรสฺย วํศียผินูเยโล ทุหิตา หนฺนาขฺยา อติชรตี ภวิษฺยทฺวาทิเนฺยกา ยา วิวาหาตฺ ปรํ สปฺต วตฺสรานฺ ปตฺยา สห นฺยวสตฺ ตโต วิธวา ภูตฺวา จตุรศีติวรฺษวย: ปรฺยฺยนตํ
37 Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
มนฺทิเร สฺถิตฺวา ปฺรารฺถโนปวาไสรฺทิวานิศมฺ อีศฺวรมฺ อเสวต สาปิ สฺตฺรี ตสฺมินฺ สมเย มนฺทิรมาคตฺย
38 Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
ปรเมศฺวรสฺย ธนฺยวาทํ จการ, ยิรูศาลมฺปุรวาสิโน ยาวนฺโต โลกา มุกฺติมเปกฺษฺย สฺถิตาสฺตานฺ ยีโศรฺวฺฤตฺตานฺตํ ชฺญาปยามาสฯ
39 Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
อิตฺถํ ปรเมศฺวรสฺย วฺยวสฺถานุสาเรณ สรฺเวฺวษุ กรฺมฺมสุ กฺฤเตษุ เตา ปุนศฺจ คาลีโล นาสรตฺนามกํ นิชนครํ ปฺรตสฺถาเตฯ
40 Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
ตตฺปศฺจาทฺ พาลก: ศรีเรณ วฺฤทฺธิเมตฺย ชฺญาเนน ปริปูรฺณ อาตฺมนา ศกฺติมำศฺจ ภวิตุมาเรเภ ตถา ตสฺมินฺ อีศฺวรานุคฺรโห พภูวฯ
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
ตสฺย ปิตา มาตา จ ปฺรติวรฺษํ นิสฺตาโรตฺสวสมเย ยิรูศาลมมฺ อคจฺฉตามฺฯ
42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
อปรญฺจ ยีเศา ทฺวาทศวรฺษวยเสฺก สติ เตา ปรฺวฺวสมยสฺย รีตฺยนุสาเรณ ยิรูศาลมํ คตฺวา
43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
ปารฺวฺวณํ สมฺปาทฺย ปุนรปิ วฺยาฆุยฺย ยาต: กินฺตุ ยีศุรฺพาลโก ยิรูศาลมิ ติษฺฐติฯ ยูษผฺ ตนฺมาตา จ ตทฺ อวิทิตฺวา
44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
ส สงฺคิภิ: สห วิทฺยต เอตจฺจ พุทฺวฺวา ทิไนกคมฺยมารฺคํ ชคฺมตุ: ฯ กินฺตุ เศเษ ชฺญาติพนฺธูนำ สมีเป มฺฤคยิตฺวา ตทุทฺเทศมปฺราปฺย
45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
เตา ปุนรปิ ยิรูศาลมมฺ ปราวฺฤตฺยาคตฺย ตํ มฺฤคยาญฺจกฺรตุ: ฯ
46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
อถ ทินตฺรยาตฺ ปรํ ปณฺฑิตานำ มเธฺย เตษำ กถา: ศฺฤณฺวนฺ ตตฺตฺวํ ปฺฤจฺฉํศฺจ มนฺทิเร สมุปวิษฺฏ: ส ตาภฺยำ ทฺฤษฺฏ: ฯ
47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
ตทา ตสฺย พุทฺธฺยา ปฺรตฺยุตฺตไรศฺจ สรฺเวฺว โศฺรตาโร วิสฺมยมาปทฺยนฺเตฯ
48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
ตาทฺฤศํ ทฺฤษฺฏฺวา ตสฺย ชนโก ชนนี จ จมจฺจกฺรตุ: กิญฺจ ตสฺย มาตา ตมวทตฺ, เห ปุตฺร, กถมาวำ ปฺรตีตฺถํ สมาจรสฺตฺวมฺ? ปศฺย ตว ปิตาหญฺจ โศกากุเลา สนฺเตา ตฺวามนฺวิจฺฉาว: สฺมฯ
49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
ตต: โสวทตฺ กุโต มามฺ อไนฺวจฺฉตํ? ปิตุรฺคฺฤเห มยา สฺถาตวฺยมฺ เอตตฺ กึ ยุวาภฺยำ น ชฺญายเต?
50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
กินฺตุ เตา ตไสฺยตทฺวากฺยสฺย ตาตฺปรฺยฺยํ โพทฺธุํ นาศกฺนุตำฯ
51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
ตต: ปรํ ส ตาภฺยำ สห นาสรตํ คตฺวา ตโยรฺวศีภูตสฺตเสฺถา กินฺตุ สรฺวฺวา เอตา: กถาสฺตสฺย มาตา มนสิ สฺถาปยามาสฯ
52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.
อถ ยีโศ รฺพุทฺธิ: ศรีรญฺจ ตถา ตสฺมินฺ อีศฺวรสฺย มานวานาญฺจานุคฺรโห วรฺทฺธิตุมฺ อาเรเภฯ

< Luka 2 >