< Luka 2 >
1 Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
And it was don in tho daies, a maundement wente out fro the emperour August, that al the world schulde be discryued.
2 Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
This firste discryuyng was maad of Cyryn, iustice of Sirie.
3 Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
And alle men wenten to make professioun, ech in to his owne citee.
4 Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
And Joseph wente vp fro Galilee, fro the citee Nazareth, in to Judee, in to a citee of Dauid, that is clepid Bethleem, for that he was of the hous and of the meyne of Dauid,
5 Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
that he schulde knouleche with Marie, his wijf, that was weddid to hym, and was greet with child.
6 Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
And it was don, while thei weren there, the daies weren fulfillid, that sche schulde bere child.
7 akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
And sche bare hir first borun sone, and wlappide hym in clothis, and leide hym in a cratche, for ther was no place to hym in no chaumbir.
8 Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
And scheepherdis weren in the same cuntre, wakynge and kepynge the watchis of the nyyt on her flok.
9 Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
And lo! the aungel of the Lord stood bisidis hem, and the cleernesse of God schinede aboute hem; and thei dredden with greet drede.
10 Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
And the aungel seide to hem, Nyle ye drede; for lo! Y preche to you a greet ioye, that schal be to al puple.
11 Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
For a sauyoure is borun to dai to you, that is Crist the Lord, in the citee of Dauid.
12 Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.”
And this is a tokene to you; ye schulen fynde a yong child wlappid in clothis, and leid in a cratche.
13 Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
And sudenli ther was maad with the aungel a multitude of heuenli knyythod, heriynge God,
14 “Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!”
and seiynge, Glorie be in the hiyeste thingis to God, and in erthe pees be to men of good wille.
15 Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.”
And it was don, as the `aungelis passiden awei fro hem in to heuene, the scheephirdis spaken togider, and seiden, Go we ouer to Bethleem, and se we this word that is maad, which the Lord hath `maad, and schewide to vs.
16 Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
And thei hiyynge camen, and founden Marie and Joseph, and the yong child leid in a cratche.
17 Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
And thei seynge, knewen of the word that was seid to hem of this child.
18 Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
And alle men that herden wondriden, and of these thingis that weren seid to hem of the scheephirdis.
19 Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
But Marie kepte alle these wordis, berynge togider in hir herte.
20 Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
And the scheepherdis turneden ayen, glorifyinge and heriynge God in alle thingis that thei hadden herd and seyn, as it was seid to hem.
21 Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
And aftir that the eiyte daies weren endid, that the child schulde be circumcided, his name was clepid Jhesus, which was clepid of the aungel, bifor that he was conceyued in the wombe.
22 Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
And aftir that the daies of the purgacioun of Marie weren fulfillid, aftir Moyses lawe, thei token hym into Jerusalem, to offre hym to the Lord, as it is writun in the lawe of the Lord,
23 Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”
For euery male kynde openynge the wombe, schal be clepid holi to the Lord; and that thei schulen yyue an offryng,
24 Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
aftir that it is seid in the lawe of the Lord, A peire of turturis, or twei culuer briddis.
25 Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
And lo! a man was in Jerusalem, whos name was Symeon; and this man was iust and vertuous, and aboode the coumfort of Israel; and the Hooli Goost was in hym.
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
And he hadde takun an answere of the Hooli Goost, that he schulde not se deeth, but he sawy first the Crist of the Lord.
27 Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
And he cam in spirit into the temple. And whanne his fadir and modir ledden the child Jhesu to do aftir the custom of the lawe for hym,
28 Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
he took hym in to hise armes, and he blesside God,
29 “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
and seide, Lord, now thou leuyst thi seruaunt aftir thi word in pees;
30 Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
for myn iyen han seyn thin helthe,
31 ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
which thou hast maad redi bifor the face of alle puplis;
32 Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”
liyt to the schewyng of hethene men, and glorie of thi puple Israel.
33 Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
And his fadir and his modir weren wondrynge on these thingis, that weren seid of hym.
34 Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
And Symeon blesside hem, and seide to Marie, his modir, Lo! this is set in to the fallyng doun and in to the risyng ayen of many men in Israel, and in to a tokene, to whom it schal be ayenseid.
35 na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”
And a swerd schal passe thorou thin owne soule, that the thouytis ben schewid of many hertis.
36 Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
And Anna was a prophetesse, the douytir of Fanuel, of the lynage of Aser. And sche hadde goon forth in many daies, and hadde lyued with hir hosebonde seuene yeer fro hir maydynhode.
37 Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
And this was a widewe to foure scoor yeer and foure; and sche departide not fro the temple, but seruyde to God nyyt and dai in fastyngis and preieris.
38 Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
And this cam vpon hem in thilk our, and knoulechide to the Lord, and spak of hym to alle that abiden the redempcioun of Israel.
39 Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
And as thei hadden ful don alle thingis, aftir the lawe of the Lord, thei turneden ayen in to Galilee, in to her citee Nazareth.
40 Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
And the child wexe, and was coumfortid, ful of wisdom; and the grace of God was in hym.
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
And his fadir and modir wenten ech yeer in to Jerusalem, in the solempne dai of pask.
42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
And whanne Jhesus was twelue yeer oold, thei wenten vp to Jerusalem, aftir the custom of the feeste dai.
43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
And whanne the daies weren don, thei turneden ayen; and the child abood in Jerusalem, and his fadir and modir knewen it not.
44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
For thei gessynge that he hadde be in the felowschip, camen a daies iourney, and souyten hym among hise cosyns and hise knouleche.
45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
And whanne thei founden hym not, thei turneden ayen in to Jerusalem, and souyten hym.
46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
And it bifelle, that aftir the thridde dai thei founden hym in the temple, sittynge in the myddil of the doctours, herynge hem and axynge hem.
47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
And alle men that herden hym, wondriden on the prudence and the answeris of hym.
48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
And thei seyn, and wondriden. And his modir seide to hym, Sone, what hast thou do to vs thus? Lo! thi fadir and Y sorewynge han souyte thee.
49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
And he seide to hem, What is it that ye souyten me? wisten ye not that in tho thingis that ben of my fadir, it behoueth me to be?
50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
And thei vndurstoden not the word, which he spak to hem.
51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
And he cam doun with hem, and cam to Nazareth, and was suget to hem. And his moder kepte togidir alle these wordis, and bare hem in hir herte.
52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.
And Jhesus profitide in wisdom, age, and grace, anentis God and men.