< Luka 2 >
1 Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
And in those days it occurred, that a decree went forth from Augustus Caesar, that all the people of his dominion should be enrolled.
2 Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
And this enrollment was first made under the presidency of Quirinus in Syria.
3 Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
And everyone went to his own city to be enrolled.
4 Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
And Joseph also went up from Nazareth of Galilee to Judaea, to the city of David which is called Bethlehem, because he was of the house and lineage of David,
5 Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
with Mary his espoused, then pregnant, to be enrolled.
6 Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
And it was while they were there, that the days for her to bring forth were completed.
7 akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
And she brought forth her firstborn son, and wrapped him in bandages, and laid him in the stall; for they had no place where they could lodge.
8 Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
And there were shepherds in that region, who abode there and kept watch of their flocks by night.
9 Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
And lo, the angel of God came to them, and the glory of the Lord shone upon them: and they feared with great fear.
10 Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
And the angel said to them: Fear not; for, behold I announce to you great joy, which will be to all the world.
11 Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
For there is born to you this day a deliverer, who is the Lord Messiah, in the city of David
12 Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.”
And this is the sign for you: Ye will find the babe wrapped in bandages, and placed in a stall.
13 Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
And instantly there were seen with the angel, the many hosts of heaven, praising God, and saying:
14 “Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!”
Glory to God in the highest heavens, and on earth peace and good hope for men.
15 Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.”
And it was so, that when the angels had gone from them into heaven, the shepherds conferred with one another, and said: Let us go down to Bethlehem, and see this thing which hath occurred, as the Lord hath made known to us.
16 Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
And they came hastily, and found Mary and Joseph, and the babe laid in the stall.
17 Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
And when they saw, they made known the information which was given to them concerning the child.
18 Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
And all that heard, wondered at the things that were told them by the shepherds.
19 Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
And Mary laid up all these things, and pondered them in her heart.
20 Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
And the shepherds returned glorifying and praising God for all that they had seen and heard, as it was told them.
21 Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
And when the eight days for the circumcision of the child were completed, his name was called JESUS; as he was named by the angel, before he was conceived in the womb
22 Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
And when the days of their purification were completed, according to the law of Moses, they carried him to Jerusalem, to present him before the Lord:
23 Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”
(as it is written in the law of the Lord, that every male opening the womb shall be called holy to the Lord: )
24 Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
and to offer a sacrifice, according as it is written in the law of the Lord, A pair of turtle-doves, or two young pigeons.
25 Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
And there was a certain man in Jerusalem, whose name was Simeon. This man was upright and just, and was waiting for the consolation of Israel, and the Holy Spirit was upon him.
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
And it had been told him by the Holy Spirit, that he would not see death, until he should see the Messiah of the Lord.
27 Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
This man came, by the Spirit, into the temple; and when his parents brought in the child Jesus, to do for him as is commanded in the law,
28 Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
he took him in his arms, and blessed God, and said:
29 “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
My Lord, now release thou thy servant in peace, as thou hast said:
30 Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
for lo, my eyes have seen thy mercy,
31 ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
which thou hast prepared in the presence of all nations,
32 Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”
a light for a revelation to the Gentiles, and a glory for thy people Israel.
33 Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
And Joseph and his mother were astonished at those things which were spoken concerning him.
34 Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
And Simeon blessed them, and said to Mary his mother: Behold, this child is set forth for the fall and for the rising of many in Israel, and for a standard of contention;
35 na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”
(and also a dart will pierce thy own soul); that the thoughts of the hearts of many may be disclosed.
36 Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
And Hanna, a prophetess, the daughter of Phanuel, of the tribe of Asher, she also was aged in days, and, from her maidenhood, had lived seven years with her husband,
37 Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
and was a widow of about eighty and four years, and departed not from the temple, but worshipped by day and by night with fasting and prayer;
38 Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
and she too stood up, in that hour, and gave thanks to the Lord, and spoke of him to every one that waited for the redemption of Jerusalem.
39 Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
And when they had accomplished all things, according to the law of the Lord, they returned to Galilee, to their city Nazareth.
40 Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
And the child grew, and was strengthened in spirit, and was filled with wisdom; and the grace of God was upon him.
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
And his people went up to Jerusalem every year, at the feast of the passover.
42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
And when he was twelve years old, they went up to the feast, as they were accustomed.
43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
And when the days were completed, they returned: but the child Jesus remained at Jerusalem, and Joseph and his mother knew not of it;
44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
for they supposed he was with his companions. And when they had travelled a day's journey, they sought him among their people, and inquired of every one that knew them.
45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
And they did not find him. And they returned again to Jerusalem, searching for him.
46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
And after three days, they found him in the temple, sitting in the midst of the teachers, and listening to them, and asking them questions.
47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
And all they that heard him, were astonished at his wisdom and his answers.
48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
And when they saw him they were amazed. And his mother said to him: My son, why hast thou done so to us? For lo, I and thy father have been seeking for thee with great anxiety.
49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
He said to them: Why did ye seek me? Do ye not know, that it behooveth me to be in my Father's house?
50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
But they did not comprehend the word that he spoke to them.
51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
And he went down with them, and came to Nazareth, and was obedient to them. And his mother laid up all these things in her heart.
52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.
And Jesus increased in stature, and in wisdom, and in grace, before God and men.