< Luka 2 >
1 Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
Now it happened in those days, that a decree went out from Caesar Augustus that the whole empire should be enrolled.
2 Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
This was the first enrollment made when Qurinos was governor of Syria.
3 Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
All went to enroll themselves, everyone to his own city.
4 Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
Yauseph also went up from Galila, out of the city of Natsrath, into Yehuda, to the city of Dawid, which is called Beth-Lekhem, because he was of the house and family of Dawid;
5 Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
to enroll himself with Maryam, who was pledged to be married to him, being pregnant.
6 Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
It happened, while they were there, that the day had come that she should give birth.
7 akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
And she gave birth to her firstborn son, and wrapped him with pieces of cloth, and placed him in a feeding trough, because there was no guest room available for them.
8 Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
There were shepherds in the same country staying in the field, and keeping watch by night over their flock.
9 Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
And look, an angel of the Lord stood by them, and the glory of the Lord shone around them, and they were terrified.
10 Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
The angel said to them, "Do not be afraid, for see, I bring you good news of great joy which will be to all the people.
11 Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
For there is born to you, this day, in the city of Dawid, a Savior, who is Meshikha, the Lord.
12 Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.”
This is the sign to you: you will find a baby wrapped in strips of cloth, lying in a feeding trough."
13 Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
Suddenly, there was with the angel a multitude of the heavenly army praising God, and saying,
14 “Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!”
"Glory to God in the highest, and on earth peace, good will toward humankind."
15 Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.”
And it happened that when the angels went away from them into the sky, the shepherds said one to another, "Let us go to Beth-Lekhem, now, and see this thing that has happened, which the Lord has made known to us."
16 Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
They came with haste, and found both Maryam and Yauseph, and the baby was lying in the feeding trough.
17 Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
When they saw it, they made known the saying which was spoken to them about this child.
18 Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
All who heard it wondered at the things which were spoken to them by the shepherds.
19 Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
But Maryam kept all these sayings, pondering them in her heart.
20 Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
The shepherds returned, glorifying and praising God for all the things that they had heard and seen, just as it was told them.
21 Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
When eight days were fulfilled to circumcise him, his name was called Yeshua, which was given by the angel before he was conceived in the womb.
22 Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
When the days of their purification according to the Law of Mushe were fulfilled, they brought him up to Urishlim, to present him to the Lord
23 Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”
(as it is written in the Law of the Lord, "Every male who opens the womb will be called holy to the Lord"),
24 Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
and to offer a sacrifice according to that which is said in the Law of the Lord, "A pair of turtledoves, or two young pigeons."
25 Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
And look, there was a man in Urishlim whose name was Shimon. This man was righteous and devout, looking for the consolation of Israyel, and the Rukha d'Qudsha was on him.
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
It had been revealed to him by the Rukha d'Qudsha that he should not see death before he had seen the Lord's Meshikha.
27 Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
He came in the Rukha into the temple. When the parents brought in the child, Yeshua, that they might do concerning him according to the requirement of the Law,
28 Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
then he received him into his arms, and blessed God, and said,
29 “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
"Now you are releasing your servant, Lord, according to your word, in peace;
30 Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
for my eyes have seen your salvation,
31 ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
which you have prepared before the face of all peoples;
32 Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”
a light for revelation to the nations, and the glory of your people Israyel."
33 Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
And his father and his mother were marveling at the things which were spoken concerning him,
34 Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
and Shimon blessed them, and said to Maryam, his mother, "Look, this child is set for the falling and the rising of many in Israyel, and for a sign which is spoken against.
35 na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”
Yes, a sword will pierce through your own soul, that the thoughts of many hearts may be revealed."
36 Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
There was one Khana, a prophetess, the daughter of Phanuel, of the tribe of Asher (she was of a great age, having lived with a husband seven years from her virginity,
37 Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
and she had been a widow for about eighty-four years), who did not depart from the temple, worshipping with fastings and petitions night and day.
38 Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
Coming up at that very hour, she gave thanks to God, and spoke of him to all those who were looking for the redemption of Urishlim.
39 Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
When they had accomplished all things that were according to the Law of the Lord, they returned into Galila, to their own city, Natsrath.
40 Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
The child was growing, and was becoming strong, being filled with wisdom, and the favor of God was upon him.
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
His parents went every year to Urishlim at the feast of the Passover.
42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
When he was twelve years old, they went up according to the custom of the feast,
43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
and when they had fulfilled the days, as they were returning, the boy Yeshua stayed behind in Urishlim. His parents did not know it,
44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
but supposing him to be in the company, they went a day's journey, and they looked for him among their relatives and acquaintances.
45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
When they did not find him, they returned to Urishlim, looking for him.
46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
It happened after three days they found him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both listening to them, and asking them questions.
47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
All who heard him were amazed at his understanding and his answers.
48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
When they saw him, they were astonished, and his mother said to him, "Son, why have you treated us this way? Look, your father and I were anxiously looking for you."
49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
He said to them, "Why were you looking for me? Did you not know that I must be doing the works of my Father?"
50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
They did not understand the saying which he spoke to them.
51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
And he went down with them, and came to Natsrath. He was subject to them, and his mother kept all these sayings in her heart.
52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.
And Yeshua increased in wisdom and stature, and in favor with God and people.