< Luka 2 >

1 Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
那時,凱撒奧古斯都出了一道上諭,叫天下的人都要登記:
2 Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
這是在季黎敘利亞總督時,初次行的登記。
3 Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
於是眾人都去本城登記。
4 Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
若瑟因為是達味家族的人,也從加利肋亞納匝肋城,上猶大名叫白冷的達味城去,
5 Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
好同自己已懷孕的聘妻瑪利亞去登記。
6 Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
他們在那裡的時候,她分娩的日期滿了,
7 akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
便生了她的頭胎兒,用襁褓包裹起,放在馬槽裏,因為在客棧中為他們沒有地方。
8 Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
在那區有些牧人露宿,守夜看守羊群。
9 Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
有上主的一個天使站在他們身邊,上主的光輝環照著他們,他們便非常害怕。
10 Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
天使向他們說:「不要害怕! 看,我給你們報告一個為全民族的大喜訊:
11 Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
今天在達味城中,為你們誕生了一位救世者,他是主默西亞。
12 Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.”
這是給你們的記號:你們將要看見一個嬰兒,裹著襁褓,躺在馬槽裏。」
13 Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
忽然有一隊天軍,同那天使一起讚頌天主說:
14 “Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!”
「天主受享光榮於高天,主愛的人在世享平安。」
15 Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.”
眾天使離開他們往天上去了以後,牧人們就彼此說:「我們且往白冷去,看看上主所報告給我們所發生的事。」
16 Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
他們急忙去了,找到了瑪利亞和若瑟,並那躺在馬在槽中的嬰兒。
17 Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
他們看見以後,就把他們對他們論這小孩所說的事,傳揚開了,
18 Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
凡聽見的人都驚訝牧人向他們所說的的事。
19 Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
瑪利亞卻把這一切事默存在自己心中,反覆思想。
20 Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
牧人們為了他們所聽見和看見的一切,正如天使向他們說的一樣,就光榮讚美天主回去了。
21 Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
滿了八天,孩子應受割損,遂給祂起名叫耶穌,這是祂降孕母胎前,由天使所起的。
22 Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
按梅瑟的法律,一滿了他們取潔的日期,他們便帶孩子上耶路撒冷去獻給上主,
23 Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”
就如上主法律上所記載的:『凡開胎首生的男孩性,應祝聖於上主。』
24 Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
並該照上主法上所吩咐的,獻上禮物:一對斑鳩或兩隻鶵鴿。
25 Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
那時,在耶路撒冷有一個人,名叫西默盎。這人正義虔誠,期待以色列的安慰,而且聖神也在他身上。
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
他曾蒙聖神啟示:自己在未看見上主的受傅者以前,決見不到死亡
27 Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
他因聖神的感動,進了聖殿;那時,抱著嬰兒耶穌的父母正進來,要按著法律的慣例為祂行禮。
28 Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
西默盎就雙臂接過祂來,讚美天主說:
29 “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
「主啊! 現在可照你的話,放你的僕人平安去了!
30 Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
因為我親眼看見了你的救援,
31 ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
即你在萬民之早準備好的:
32 Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”
為作啟示異邦的光明,你百姓以色列的榮耀。」
33 Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
他的父親和母親就驚異他關於耶穌所說的這些話。
34 Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
西默盎祝福了他們,又向祂的母親瑪利亞說:「看,這孩子已被立定,為使以色列中許多人跌倒和復起,並成為夭對的記號─
35 na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”
至於妳,要有一把利劍刺透妳的心靈─為叫許多人心中的思念顯露在出來。」
36 Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
又有一位女先知亞納,是阿協爾支派法奴耳的女兒,已上了年紀。她出閣後,與丈夫同居了七年,
37 Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
以後就守寡,直到八十四歲。她齋戒祈禱,晝夜事奉天主,總不離開聖殿。
38 Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
正在那時刻,她也前來稱謝天主,並同一切希望耶路撒冷得救贖的人,講論這孩子。
39 Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
他們按著上主的法律,行完了一切,使返回了加利肋亞,他們的本城納匝肋。
40 Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
孩子漸漸長大而強壯,充滿智慧,天主的恩寵常在祂身上。
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
祂的父母每年逾越節往耶路撒冷去。
42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
祂到了十二歲時,他們又節日的慣例上去了。
43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
過完了節日,他們回去的時候,孩童耶穌卻留在耶路撒冷,祂的父母並未發覺。
44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
他們只以為祂在同行的人中間,遂走了一天的路程;以後就在親戚和相識的人中尋找祂。
45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
既找不著,便折回耶路撒冷找祂。
46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
過了三天,才在聖殿裏找到了祂。祂正坐在經師中,聆聽他們,也詢問他們。
47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
凡聽見祂的人,對祂的智慧和對答,都驚奇不止。
48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
他們一看見祂,便大為驚異,祂的母親就向祂說:「孩子,為什麼你這樣對待我們? 看,你的父親和我,一直痛苦的找你。」
49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
耶穌對他們說:「你們為什麼找我? 你們不知道我必須在我父親那裡嗎? 」
50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
但是,他們不明白祂對他們所說的話。
51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
祂就同他們下去,來到納匝肋,屬他們管轄。祂的母親逜把一切默存在心中。
52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.
耶穌在智慧和身體上,並在天主和人前的恩愛上,漸漸地增長。

< Luka 2 >