< Luka 19 >

1 Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
And as Jesus entered and passed through Jericho,
2 Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
there was a certain man, whose name was Zaccheus, who was rich, and chief of the publicans;
3 Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
and he wished to see Jesus, who he was; and could not, on account of the crowd; because Zaccheus was small in stature.
4 Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
And he ran forward of Jesus, and climbed a wild fig-tree, in order to see him; for he was to pass that way.
5 Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
And when Jesus came to the place, he saw him, and said to him: Make haste and come down, Zaccheus; for I must be at thy house to-day.
6 Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
And he hastened, and came down, and received him with gladness.
7 Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
And when they all saw it, they murmured, and said: He hath gone in to be guest with a man that is a sinner.
8 Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
And Zaccheus stood up, and said to Jesus: Behold, my Lord, the half of my riches I give to the poor; and to every man, whom I have wronged in any thing, I restore fourfold.
9 Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
Jesus said to him: This day, life is to this house; for he also is a son of Abraham.
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
For the Son of man came, to seek and to vivify that which was lost.
11 Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
And when they heard these things, he proceeded to utter a similitude; because he was near to Jerusalem, and they supposed that the kingdom of God was to be soon developed.
12 Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
And he said: A certain man of high birth was going to a distant place, to obtain royalty, and return again.
13 Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
And he called his ten servants, and gave them ten pounds: and he said to them, Traffic until I come.
14 Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
But the inhabitants of his city hated him; and they sent envoys after him, saying: We wish this man not to reign over us.
15 “Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
And when he had obtained the royalty, and had returned, he commanded those servants to be called, to whom he had committed his money; that he might know what each of them had gained by trading.
16 Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
And the first came, and said: My Lord, thy pound hath gained ten pounds.
17 Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
He said to him: Well done, good servant! As thou hast been faithful over a little, thou shalt have authority over ten towns.
18 Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
And the second came, and said: My lord, thy pound hath produced five pounds.
19 Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
He said likewise to him: Thou also shalt have authority over five towns.
20 “Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
And another came, and said: My lord, lo, this is thy pound, which hath been with me, laid up in fine linen.
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
For I was afraid of thee, because thou art a hard man, and takest up that which thou layedst not down, and reapest that which thou sowedst not.
22 Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
He said to him: Out of thy own mouth will I judge thee, thou evil servant. Thou knewest me, that I am a hard man, and that I take up what I laid not down, and reap what I sowed not!
23 Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
Why didst thou not put my money into the broker's hands, that when I came, I might have demanded it with interest?
24 Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
And he said to them that stood before him: Take from him the pound, and give it to him with whom are the ten pounds.
25 Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
They say to him: Our lord, there are with him ten pounds.
26 Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
He said to them: I tell you, that to every one that hath, will be given; and from him that hath not, even what he hath will be taken away.
27 Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
But as for those my enemies, who would not have me to reign over them, bring them and slay them before me.
28 Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
And when Jesus had spoken these things, he went forward, to go to Jerusalem.
29 Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
And when he arrived at Bethphage and Bethany, near to the mount called the place of Olives, he sent two of his disciples,
30 akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
and said to them: Go ye to the village that is over against us, and as ye enter it, ye will find a colt tied, on which no man ever rode; loose him and bring him.
31 Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
And if any man ask you, Why do ye loose him? say to him: Our Lord needeth him.
32 Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
And they went who were sent, and they found, as he said to them.
33 Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
And as they loosed the colt, the owner of him said to them: Why do ye loose that colt?
34 Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
And they said: Because our Lord needeth him.
35 Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
And they brought him to Jesus. And they cast their garments upon the colt, and set Jesus upon him.
36 Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
And as he went, they spread their garments in the way.
37 Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
And when he came near to the descent of the place of Olives, the whole multitude of the disciples began to rejoice, and to praise God, with a loud voice, for all the mighty deeds which they had seen.
38 wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
And they said: Blessed be the king, that cometh in the name of the Lord: peace in heaven, and glory on high.
39 Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
And some of the Pharisees from among the crowd, said to him: Rabbi, rebuke thy disciples.
40 Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
He said to them: I tell you, that, if these should be silent, the stones would cry out.
41 Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
And as he drew near, and beheld the city, he wept over it:
42 akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
and said: O, hadst thou known the things that are of thy peace, at least in this thy day: but now they are hidden from thy eyes.
43 Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
For the days will come upon thee, when thy enemies will encompass thee, and besiege thee on every side.
44 Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
And they will destroy thee, and thy children within thee; and will not leave in thee one stone upon another; because thou knewest not the time of thy visitation.
45 Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
And when he entered the temple, he began to expel those who bought and sold in it.
46 akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
And he said to them: It is written, My house is a house of prayer; but ye have made it a den of robbers.
47 Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
And he taught daily in the temple: and the chief priests and Scribes and Elders of the people, sought to destroy him.
48 lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.
But they found not, what they could do to him; for all the people hung upon him to hear him.

< Luka 19 >