< Luka 18 >

1 Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
Then Jesus told them a parable about the need to pray at all times and not lose heart.
2 Alisema: “Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
He said, “In a certain city there was a judge who neither feared God nor respected man.
3 Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
There was also a widow in that city who kept coming to him and saying, ‘Give me justice against my adversary.’
4 Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
For a while he would not do so, but afterward he said to himself, ‘Though I neither fear God nor respect man,
5 lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!”
yet because this widow keeps bothering me, I will give her justice, so that she will not wear me out by continually coming to me.’”
6 Basi, Bwana akaendelea kusema, “Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
Then the Lord said, “Consider what this unrighteous judge said.
7 Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
If even he ultimately rendered a just decision, will not God patiently listen to his chosen ones, who cry out to him day and night, and give them justice?
8 Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?”
I tell you that he will bring about justice for them quickly. Nevertheless, when the Son of Man comes, will he find faith on the earth?”
9 Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
He also told this parable to some who were confident in their own righteous and regarded others with contempt:
10 “Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
“Two men went up to the temple to pray. One was a Pharisee and the other was a tax collector.
11 Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
The Pharisee stood by himself and prayed like this: ‘God, I thank yoʋ that I am not like other people: swindlers, unrighteous, adulterers, or even like this tax collector.
12 Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
I fast twice a week, and I give tithes of all that I get.’
13 Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
But the tax collector stood at a distance and would not even lift up his eyes to heaven, but beat his breast, saying, ‘God, be merciful to me, a sinner!’
14 Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa.”
I tell you, this man went down to his home justified rather than the other one. For everyone who exalts himself will be humbled, but he who humbles himself will be exalted.”
15 Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
Now people were even bringing their babies to Jesus so that he might touch them. When the disciples saw this, they rebuked those who were bringing them,
16 Lakini Yesu akawaita kwake akisema: “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
but Jesus called for them and said, “Let the little children come to me and do not hinder them, for the kingdom of God belongs to such as these.
17 Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo.”
Truly I say to you, whoever does not receive the kingdom of God like a little child will certainly not enter it.”
18 Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?” (aiōnios g166)
Then a certain ruler asked him, “Good Teacher, what must I do to inherit eternal life?” (aiōnios g166)
19 Yesu akamwambia, “Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
Jesus said to him, “Why do yoʋ call me good? No one is good except God alone.
20 Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako.”
Yoʋ know the commandments: ‘Do not commit adultery, Do not murder, Do not steal, Do not give false testimony, Honor yoʋr father and yoʋr mother.’”
21 Yeye akasema, “Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
The man said, “I have kept all these commandments from the time I was a young boy.”
22 Yesu aliposikia hayo akamwambia, “Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate.”
When Jesus heard this, he said to him, “One thing yoʋ still lack: Sell everything yoʋ have and distribute the money to the poor, and yoʋ will have treasure in heaven; then come follow me.”
23 Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
But when the man heard this, he became very sorrowful, for he was extremely rich.
24 Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, “Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
When Jesus saw that the man had become very sorrowful, he said, “How difficult it will be for those who have riches to enter the kingdom of God!
25 Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
For it is easier for a camel to go through the eye of a needle than for a rich person to enter the kingdom of God.”
26 Wale watu waliposikia hayo, wakasema, “Nani basi, atakayeokolewa?”
Those who heard this said, “Who then can be saved?”
27 Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu.”
Jesus said, “What is impossible with men is possible with God.”
28 Naye Petro akamwuliza, “Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!”
Then Peter said, “Behold, we have left everything and followed yoʋ.”
29 Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
Jesus said to them, “Truly I say to you, there is no one who has left house, parents, brothers, wife, or children, for the sake of the kingdom of God,
30 atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao.” (aiōn g165, aiōnios g166)
who will not surely receive many times more in this present age—and in the age to come, eternal life.” (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
Then Jesus took the twelve aside and said to them, “Behold, we are going up to Jerusalem, and everything written by the prophets about the Son of Man will be fulfilled.
32 Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
For he will be delivered up to the Gentiles, and he will be mocked, insulted, and spit upon.
33 Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
After flogging him, they will kill him, and on the third day he will rise again.”
34 Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
But the disciples did not understand any of these things; this statement was hidden from them, and they did not comprehend what was being said.
35 Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
As Jesus drew near to Jericho, a blind man was sitting by the road begging.
36 Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”
When he heard a crowd going by, he asked what was happening.
37 Wakamwambia, “Yesu wa Nazareti anapita.”
They told him that Jesus of Nazareth was passing by.
38 Naye akapaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
So he cried out, “Jesus, Son of David, have mercy on me!”
39 Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: “Mwana wa Daudi, nihurumie;”
Then those who were out in front rebuked him, telling him to be silent. But he cried out all the more, “Son of David, have mercy on me!”
40 Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
So Jesus stopped and ordered the man to be brought to him. When the man drew near, Jesus asked him,
41 “Unataka nikufanyie nini?” Naye akamjibu, “Bwana, naomba nipate kuona tena.”
“What do yoʋ want me to do for yoʋ?” He said, “Lord, I want to receive my sight.”
42 Yesu akamwambia, “Ona! Imani yako imekuponya.”
So Jesus said to him, “Receive yoʋr sight; yoʋr faith has healed yoʋ.”
43 Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.
Immediately he received his sight and began following Jesus, glorifying God. And when all the people saw it, they gave praise to God.

< Luka 18 >