< Luka 16 >

1 Yesu aliwaambia wanafunzi wake: “Tajiri mmoja alikuwa na karani wake. Huyu karani alichongewa kwamba alitumia ovyo mali ya tajiri wake.
uYesu akavavula avavulanisivua vake, “palyale nu muunhu jumonga m'mofu alyale nu m'baha mu mbombo jake,
2 Yule tajiri akamwita akamwambia: Ni mambo gani haya ninayosikia juu yako? Toa hesabu ya mapato na matumizi ya mali yangu, kwa maana huwezi kuwa karani tena.
pe vakampela umm imhola sa m'baha jula kuuti, um'bombi ghwako um'baha itaghania ifyuma fyako. pe ummo akan'kemela akam'bula akati, “kwe kiliku ulyuve kino nipulika? humia imhola ija vuvaha vwako, ulwakuva nungave m'baha kange mu mbombo jango.
3 Yule karani akafikiri: Bwana wangu amenifukuza kazi ya ukarani; nitafanya nini? Kwenda kulima siwezi; kwenda kuombaomba kama maskini ni aibu.
um'baha jula akijovela mu mwoojo ghwake, nivombe kiki, ulwakuva untwa ghwango ikunivusia mu mbombo jango ija vuvaha? nisila ngufu sa kulima, na kusuma nivona soni.
4 Naam, najua la kufanya, ili nitakapofukuzwa kazi, watu waweze kunikaribisha nyumbani kwao.
nikagula lino kyale nivomba kyande vanivusisie mu mbombo jango ja kwimilila avaanhu vanyupile mu nyuma save.
5 Basi, akawaita wadeni wa bwana wake, mmoja mmoja, akamwambia yule wa kwanza: Unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?
pe pano umweimilili jula akavakemhela voni vano visighilua nu ntwa ghwake akam'bula ughwa kwanda, 'ghusighilua ilingi nu ntwa ghwango?'
6 Yeye akamjibu: Mapipa mia ya mafuta ya zeituni. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, keti haraka, andika hamsini.
akati, 'fighelelo kilundo fya mafuta akam'bula,' tola ilikalataasi lyako ng'ani ng'ani lemba ifijigho fihaano,
7 Kisha akamwuliza mdeni mwingine: Wewe unadaiwa kiasi gani? Yeye akamjibu: Magunia mia ya ngano. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, andika themanini.
pe akam'bula ujunge najuve ghusighilua ilingi? akati, 'ifighelelo kilundo kimo ifya vutine vwa ngano'. tola ilikalataasi lyako, lemba ifijigho lekela kwoni'.
8 “Basi, yule bwana akamsifu huyo karani asiye mwaminifu, kwa kuwa alitumia busara. Kwa maana watu wa dunia hii wana busara zaidi na mambo yao kuliko watu wa mwanga.” (aiōn g165)
untwa jula akamughinia um'baha jula ulakuva alyavombile nu vukagusi. ulwakuva avaanha va pa iisi iji vali nuvukagusi vyinga kukila avaanha va Nguluve. (aiōn g165)
9 Naye Yesu akaendelea kusema, “Nami nawaambieni, jifanyieni marafiki kutokana na mali ya dunia, ili zitakapowaishieni, mweze kupokewa nao katika makao ya milele. (aiōnios g166)
lino une nikuvavula kuuti, muvatangaghe avajinu ni kyuma kino mulinakyo, neke kyande kisilile, mwupilue ku vukalo vwa kusila na kusila. (aiōnios g166)
10 Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, atakuwa mwaminifu katika mambo makubwa; na yeyote asiye mwaminifu katika mambo madogo, hatakuwa mwaminifu katika mambo makubwa.
juno mugholofu mu lidebe kyongo iva mugholofu na mulikome. ghwope juno namugholofu mu lidebe naiva mugholofu na mulikome kange.
11 Kama basi, ninyi si hamjawa waaminifu mali mbaya za dunia, ni nani atakayewakabidhi zile mali za kweli?
nave umue namulyale vagholofu mu kyuma kino na kyakyangani pe ghwevene juno ikuvitika ku kyuma ikya lweli?
12 Na kama hamjakuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewakabidhi mali yenu wenyewe?
kange nave namulyale vagholofu kutumila ikyuma kya muunhu junge, ghweveni juno ikuvapela sino sinu jumue?
13 “Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au ataambatana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.”
nakwale um'bombi juno ikuvavombela avatwa vavili, ulwakuva ghukunkalalilagha jumo na kumughana ujunge, nambe kukolana nuju na kum'benapula uju. nungawesie kukum'bombela uNguluve ni kyuma.
14 Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, kwa vile wao walikuwa wanapenda sana fedha, wakamdharau Yesu.
pe avafarisayi, vano valyale vinoghua indalama ye vapulike aghuo ghoni vakam'benafula.
15 Hapo akawaambia, “Ninyi mnajifanya wema mbele ya watu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana kile kinachoonekana kuwa kitukufu mbele ya watu, Mungu anakiona kuwa takataka.
kange akavavula, “umue mwemwemu mukuvona hwene vanya kyang'ani pa maaso gha vaanhu, neke UNguluve akagwile amoojo ghinu. ulwakuva lino lyimike kwa muunhu liva ng'alasi pa maaso ghwa Nguluve.
16 “Sheria na maandishi ya manabii vilikuweko mpaka wakati wa Yohane mbatizaji. Tangu hapo, Ufalme wa Mungu unahubiriwa, na kila mmoja anauingia kwa nguvu.
indaghilo na vavili pwefilyale kuhanga uYohani panoa akisile. kuhuma unsiki ughuo, imhola inofu ja vutwa vwa Nguluve jikapulisivue, nu muunhu ghweni ighela kukwingila ku ngufu.
17 Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita, kuliko hata herufi moja ya Sheria kufutwa.
neke kihugu ku kyanya ni iisi fivuke kuliko ililembe limo lya ndaghilo likosekane.
18 “Yeyote anayemwacha mke wake na kuoa mwingine, anazini; na yeyote anayemwoa mwanamke aliyepewa talaka, anazini.
ghweni juno ikumuleka un'dala ghwake na kun'toola un'dala ujunge ivwafuka, ghwope juno ikun'toola juno alekilue numughosi ghwake ivwafuka.
19 “Palikuwa na mtu mmoja tajiri, ambaye alikuwa anavaa mavazi ya bei kubwa sana ya rangi ya zambarau, na ya kitani safi, na kufanya sherehe kila siku.
palyale nu mmofu jumonga alyafwalile amhenda aghanya sambalau na gha ndalama akale ihovokela uvumofu vwake uvukome.
20 Kulikuwa pia na maskini mmoja jina lake Lazaro, aliyekuwa amejaa vidonda na alikuwa analazwa mlangoni pa nyumba ya huyo tajiri.
nu nkotofu jumonga ilitavua lyake Lasali vakam'biki pa mulyango ghwa kunji kwa mofu jula, alyale ni fikongo.
21 Lazaro alitamani kula makombo yaliyoanguka kutoka meza ya tajiri; na zaidi ya hayo, mbwa walikuwa wanakuja na kulamba vidonda vyake!
ghwope akinoghelua kulia ikyakulia kino kikaghwisagha pasi pa mofu jula nasi mbua sikisa sikamumyanga ifikong'o fyake.
22 “Ikatokea kwamba huyo maskini akafa, malaika wakamchukua, wakamweka karibu na Abrahamu. Na yule tajiri pia akafa, akazikwa.
jikava unkotofu jula akafua, avanyaMhola vakantola kuhanga pakifuva pa Abulahamu. ummofu jula ghwope akafua akasyulua.
23 Huyo tajiri, alikuwa na mateso makali huko kuzimu, akainua macho yake, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro karibu naye. (Hadēs g86)
ye alyale mumuko kuvulungu kula akadindula amaaso ghake akamwagha uAbulahamu kuvutali ali nu Lasali pakifuva kyake. (Hadēs g86)
24 Basi, akaita kwa sauti: Baba Abrahamu, nionee huruma; umtume Lazaro angalau achovye ncha ya kidole chake katika maji, auburudishe ulimi wangu, maana ninateseka mno katika moto huu.
akalila akati, 'baba Abulahamu, nisaghile un'sung'e u Lasali asase ulwove lwake mumalenga, alunoghelesie ululimi lwango; ulwakuva nipumusivua mu mwoto ughu.
25 Lakini Abrahamu akamjibu: Kumbuka mwanangu, kwamba ulipokea mema yako katika maisha, naye Lazaro akapokea mabaya. Sasa lakini, yeye anatulizwa, nawe unateswa.
neke uAbulahamu akati, 'mwanago kumbuka kuuti mu vwumi vwako ukupile isako sino nono, nu Lasali vule vule alyapatile inyivi. neke lino alyapa uhuvilisivua, najuve ghupumusivua.
26 Licha ya hayo, kati yetu na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wanaotaka kuja kwenu kutoka huku wasiweze, wala wanaotaka kutoka kwenu kuja kwetu wasiweze.
na kukila aghuo, kuvikilie ilina ilikome pakate jitu kuuti vano vilonda kuluta kulyumue vakunuaghe na vaanhu va kulyumue navangalovokaghe kukwisa kulyusue'
27 Huyo aliyekuwa tajiri akasema: Basi baba, nakuomba umtume aende nyumbani kwa baba yangu,
umofu jula akati, 'nisuuma baba Abulahamu kuuti unsung'e ku nyumba kwa baba ghwango.
28 maana ninao ndugu watano, ili awaonye wasije wakaja huku kwenye mateso.
ulwakuva nili navanyalukolo vahano neke avavunge na veene ku vwoghofi piti vope vilikwisa pa mhumhuko apa.
29 Lakini Abrahamu akamwambia: Ndugu zako wanao Mose na manabii; waache wawasikilize hao.
neke uAbulahamu akati, 'kwale uMoose na vavili, valeke vavapulikisie vavuo.
30 Lakini yeye akasema: Sivyo baba Abrahamu, ila kama mtu atafufuka kutoka wafu na kuwaendea, watatubu.
umofu jula akati, 'Ndali, baba Abulamahu, neke nave angalute umuunhu juno ahumile kuvafue vilaata,
31 Naye Abrahamu akasema: Kama hawawasikilizi Mose na manabii, hawatajali hata kama mtu angefufuka kutoka wafu.”
neke uAbulahamu akam'bula akati, 'ndeve navikuvapulikisia uMoose na vavili navangampulikisie nambe umuunhu angasyuke kuhuma kuvafue.

< Luka 16 >