< Luka 13 >
1 Wakati huo watu fulani walikuja, wakamweleza Yesu juu ya watu wa Galilaya ambao Pilato alikuwa amewaua wakati walipokuwa wanachinja wanyama wao wa tambiko.
Now there were some present at that very time who told Jesus about the Galileans whose blood Pilate had mixed with their sacrifices.
2 Naye Yesu akawaambia, “Mnadhani Wagalilaya hao walikuwa wahalifu zaidi kuliko Wagalilaya wengine, ati kwa sababu wameteseka hivyo?
Jesus responded to them, “Do you think that those Galileans were worse sinners than all the other Galileans because they suffered such things?
3 Nawaambieni hakika sivyo; lakini nanyi, hali kadhalika, msipotubu, mtaangamia kama wao.
No, I tell you, but if you do not repent, you will all likewise perish.
4 Au wale kumi na wanane walioangukiwa na mnara kule Siloamu wakafa; mnadhani wao walikuwa wakosefu zaidi kuliko wengine wote walioishi Yerusalemu?
Or those eighteen who were killed when the tower in Siloam fell on them, do you think they were worse offenders than all the other people who dwell in Jerusalem?
5 Nawaambieni sivyo; lakini nanyi msipotubu, mtaangamia kama wao.”
No, I tell you, but if you do not repent, you will all likewise perish.”
6 Kisha, Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini katika shamba lake. Mtu huyu akaenda akitaka kuchuma matunda yake, lakini akaukuta haujazaa hata tunda moja.
Then he told this parable: “A man had a fig tree planted in his vineyard, and he came looking for fruit on it but did not find any.
7 Basi, akamwambia mfanyakazi wake: Angalia! Kwa miaka mitatu nimekuwa nikija kuchuma matunda ya mtini huu, nami nisiambulie kitu. Ukate! Kwa nini uitumie ardhi bure?
So he said to the vinedresser, ‘Behold, for three years I have come looking for fruit on this fig tree and have not found any. Cut it down! Why should it use up the soil?’
8 Lakini naye akamjibu: Bwana, tuuache tena mwaka huu; nitauzungushia mtaro na kuutilia mbolea.
But the vinedresser said to him in response, ‘Sir, allow it to remain for this year also, and I will dig around it and put manure on it.
9 Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vema; la sivyo, basi utaweza kuukata.”
If it bears fruit, fine; but if not, yoʋ can cut it down in the coming year.’”
10 Yesu alikuwa akifundisha katika sunagogi moja siku ya Sabato.
One Sabbath Jesus was teaching in one of the synagogues.
11 Na hapo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa miaka kumi na minane kutokana na pepo aliyekuwa amempagaa. Kwa sababu hiyo, mwili wake ulikuwa umepindika vibaya hata asiweze kusimama wima.
And behold, there was a woman who had suffered from a spirit of disability for eighteen years. She was bent over and could not stand up completely straight.
12 Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umeponywa ugonjwa wako.”
When Jesus saw her, he called her over and said to her, “Woman, yoʋ are set free from yoʋr disability.”
13 Akamwekea mikono, na mara mwili wake ukawa wima tena, akawa anamtukuza Mungu.
Then he laid his hands on her, and at once her back was made straight, and she began glorifying God.
14 Lakini mkuu wa sunagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo akawaambia wale watu walikusanyika pale, “Mnazo siku sita za kufanya kazi. Basi, fikeni siku hizo mkaponywe magonjwa yenu; lakini msije siku ya Sabato.”
But the ruler of the synagogue, indignant because Jesus had healed on the Sabbath, said to the crowd in response, “There are six days in which work should be done; so come and be healed on those days and not on the Sabbath day.”
15 Hapo Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Nani kati yenu hangemfungua ng'ombe au punda wake kutoka zizini ampeleke kunywa maji, hata kama siku hiyo ni ya Sabato?
Then the Lord said to him in response, “Hypocrites! Do not each of you on the Sabbath untie yoʋr ox or donkey from the manger, lead it away, and give it water?
16 Sasa, hapa yupo binti wa Abrahamu ambaye Shetani alimfanya kilema kwa muda wa miaka kumi na minane. Je, haikuwa vizuri kumfungulia vifungo vyake siku ya Sabato?”
Then should not this woman, a daughter of Abraham whom Satan has bound for eighteen long years, be released from this bondage on the Sabbath day?”
17 Alipokwisha sema hayo, wapinzani wake waliona aibu lakini watu wengine wote wakajaa furaha kwa sababu ya mambo yote aliyotenda.
When he said this, all his adversaries were put to shame, and the entire crowd was rejoicing over all the glorious things he was doing.
18 Yesu akauliza: “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaulinganisha na nini?
Then Jesus said, “What is the kingdom of God like? To what should I compare it?
19 NI kama mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake; ikaota hata ikawa mti. Ndege wa angani wakajenga viota vyao katika matawi yake.”
It is like a grain of mustard seed that a man took and sowed in his garden. It grew and became a large tree, and the birds of the sky nested in its branches.”
20 Tena akauliza: “Nitaulinganisha Ufalme wa Mungu na nini?
Again he said, “To what should I compare the kingdom of God?
21 Ni kama chachu aliyoitwaa mama mmoja na kuichanganya pamoja na unga debe moja kisha unga wote ukaumuka wote.”
It is like leaven that a woman took and mixed into three measures of flour until it had all been leavened.”
22 Yesu alindelea na safari yake kwenda Yerusalemu huku akipitia mijini na vijijini, akihubiri.
Then Jesus traveled through towns and villages, teaching and making his way to Jerusalem.
23 Mtu mmoja akamwuliza, “Je, Mwalimu, watu watakaookoka ni wachache?”
Someone said to him, “Lord, will only a few be saved?” Jesus said to them,
24 Yesu akawaambia, “Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; maana nawaambieni, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.
“Strive to enter through the narrow gate. For many, I tell you, will seek to enter and will not be able to.
25 “Wakati utakuja ambapo mwenye nyumba atainuka na kufunga mlango. Ninyi mtasimama nje na kuanza kupiga hodi mkisema: Bwana, tufungulie mlango. Lakini yeye atawajibu: Sijui mmetoka wapi.
Once the master of the house gets up and shuts the door, you will begin to stand outside and knock at the door, saying, ‘Lord, Lord, open the door for us.’ But he will answer you, ‘I do not know you or where you are from.’
26 Nanyi mtaanza kumwambia: Sisi ndio wale tuliokula na kunywa pamoja nawe; na wewe ulifundisha katika vijiji vyetu.
Then you will begin to say, ‘We ate and drank in yoʋr presence, and yoʋ taught in our streets.’
27 Lakini yeye atasema: Sijui ninyi mmetoka wapi; ondokeni mbele yangu, enyi nyote watenda maovu.
But he will say, ‘I tell you, I do not know you or where you are from. Depart from me, all you workers of unrighteousness.’
28 Ndipo mtakuwa na kulia na kusaga meno, wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka na Yakobo, na manabii wote wapo katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mmetupwa nje!
In that place there will be weeping and gnashing of teeth, when you see Abraham, Isaac, Jacob, and all the prophets in the kingdom of God, but you yourselves cast out.
29 Watu watakuja kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini, watakuja na kukaa kwenye karamu katika Ufalme wa Mungu.
People will come from east and west, and from north and south, and recline at the banquet table in the kingdom of God.
30 Naam, wale walio wa mwisho watakuwa wa kwanza; na wale walio wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
And behold, some are last who will be first, and some are first who will be last.”
31 Wakati huohuo, Mafarisayo na watu wengine walimwendea Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende mahali pengine, kwa maana Herode anataka kukuua.”
On that same day some Pharisees came up and said to Jesus, “Leave this place and go somewhere else, for Herod wants to kill yoʋ.”
32 Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie huyo mbweha hivi: Leo na kesho ninafukuza pepo na kuponya wagonjwa, na siku ya tatu nitakamilisha kazi yangu.
But he said to them, “Go tell that fox, ‘Behold, I will continue casting out demons and performing healings today and tomorrow, and on the third day I will finish my work.’
33 Hata hivyo, kwa leo, kesho na kesho kutwa, ni lazima niendelee na safari yangu, kwa sababu si sawa nabii auawe nje ya Yerusalemu.
Nevertheless, I must go on my way today, tomorrow, and the following day; for it is unthinkable that a prophet should perish outside of Jerusalem.
34 “Yerusalemu! We Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako pamoja kama kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, Lakini wewe umekataa.
O Jerusalem, Jerusalem, the city that kills the prophets and stones those who are sent to yoʋ! How often I have wanted to gather yoʋr children together as a hen gathers her brood under her wings, but you were not willing!
35 Haya, utaachiwa mwenyewe nyumba yako. Naam, hakika nawaambieni, hamtaniona mpaka wakati utakapofika mseme: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.”
Behold, your house is left to you desolate. I tell you, you will certainly not see me again until the time comes when you say, ‘Blessed is he who comes in the name of the Lord!’”