< Luka 13 >

1 Wakati huo watu fulani walikuja, wakamweleza Yesu juu ya watu wa Galilaya ambao Pilato alikuwa amewaua wakati walipokuwa wanachinja wanyama wao wa tambiko.
And there were certain ones at that time announcing to him concerning the Galileans, whose blood Pilate mixed with their sacrifices.
2 Naye Yesu akawaambia, “Mnadhani Wagalilaya hao walikuwa wahalifu zaidi kuliko Wagalilaya wengine, ati kwa sababu wameteseka hivyo?
And responding to them He said, Do you think that those Galileans were sinners above all the Galileans, because they suffered these things?
3 Nawaambieni hakika sivyo; lakini nanyi, hali kadhalika, msipotubu, mtaangamia kama wao.
T say unto you, Nay: but unless you may repent, you shall all likewise perish.
4 Au wale kumi na wanane walioangukiwa na mnara kule Siloamu wakafa; mnadhani wao walikuwa wakosefu zaidi kuliko wengine wote walioishi Yerusalemu?
Or those eighteen, on whom the tower in Saloam fell, and killed them, do you think that they were offenders above all the men that dwell in Jerusalem?
5 Nawaambieni sivyo; lakini nanyi msipotubu, mtaangamia kama wao.”
I say unto you, Nay: but unless you may repent, you will all likewise perish.
6 Kisha, Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini katika shamba lake. Mtu huyu akaenda akitaka kuchuma matunda yake, lakini akaukuta haujazaa hata tunda moja.
And He spoke this parable, A certain one had a fig-tree planted in his vineyard; and came seeking fruit on it and found none;
7 Basi, akamwambia mfanyakazi wake: Angalia! Kwa miaka mitatu nimekuwa nikija kuchuma matunda ya mtini huu, nami nisiambulie kitu. Ukate! Kwa nini uitumie ardhi bure?
and he said to the vinedresser, Behold, three years from which I come seeking fruit on this fig-tree, and I find none: cut it down; why indeed does it cumber the ground?
8 Lakini naye akamjibu: Bwana, tuuache tena mwaka huu; nitauzungushia mtaro na kuutilia mbolea.
And responding he says to him, Lord, let it alone also this year, until I shall dig about it, and cast manures:
9 Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vema; la sivyo, basi utaweza kuukata.”
and if it may bear fruit in the future; and if not you shall cut it down.
10 Yesu alikuwa akifundisha katika sunagogi moja siku ya Sabato.
And He was teaching in one of the synagogues on the Sabbath.
11 Na hapo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa miaka kumi na minane kutokana na pepo aliyekuwa amempagaa. Kwa sababu hiyo, mwili wake ulikuwa umepindika vibaya hata asiweze kusimama wima.
And behold, a woman having a spirit of infirmity eighteen years; and she was bowed together, and not at all able to straighten up.
12 Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umeponywa ugonjwa wako.”
And Jesus seeing her, called to her, and said, Woman, thou art loosed from thy infirmity:
13 Akamwekea mikono, na mara mwili wake ukawa wima tena, akawa anamtukuza Mungu.
and He placed His hands on her: and immediately she straightened up, and continued to glorify God.
14 Lakini mkuu wa sunagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo akawaambia wale watu walikusanyika pale, “Mnazo siku sita za kufanya kazi. Basi, fikeni siku hizo mkaponywe magonjwa yenu; lakini msije siku ya Sabato.”
And the chief ruler of the synagogue, responding, being grieved because Jesus healed on the Sabbath, said to the multitude, There are six days in which it behooveth us to work: therefore during these, coming, be healed, and not on the Sabbath-day.
15 Hapo Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Nani kati yenu hangemfungua ng'ombe au punda wake kutoka zizini ampeleke kunywa maji, hata kama siku hiyo ni ya Sabato?
And the Lord responded to him, and said, Ye hypocrites, does not each one of you loose his ox or his donkey from the stall, and leading him away, give him water on the Sabbath?
16 Sasa, hapa yupo binti wa Abrahamu ambaye Shetani alimfanya kilema kwa muda wa miaka kumi na minane. Je, haikuwa vizuri kumfungulia vifungo vyake siku ya Sabato?”
Did it not behoove this one, being a daughter of Abraham, whom Satan bound, lo, these eighteen years, to be loosed from this bondage on the Sabbath-day?
17 Alipokwisha sema hayo, wapinzani wake waliona aibu lakini watu wengine wote wakajaa furaha kwa sababu ya mambo yote aliyotenda.
And He speaking these things, all opposing Him became ashamed: and the whole multitude rejoiced over all the illustrious works wrought by Him.
18 Yesu akauliza: “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaulinganisha na nini?
Then He said, To what is the kingdom of God like? and to what shall I liken it?
19 NI kama mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake; ikaota hata ikawa mti. Ndege wa angani wakajenga viota vyao katika matawi yake.”
It is like a grain of mustard seed, which a man having taken, cast into his garden; and it grew, and became a tree; and the birds of heaven lodged in its branches.
20 Tena akauliza: “Nitaulinganisha Ufalme wa Mungu na nini?
And again He said, To what shall I liken the kingdom of God?
21 Ni kama chachu aliyoitwaa mama mmoja na kuichanganya pamoja na unga debe moja kisha unga wote ukaumuka wote.”
It is like leaven, which a woman having taken, hid in three measures of meal, until the whole was leavened.
22 Yesu alindelea na safari yake kwenda Yerusalemu huku akipitia mijini na vijijini, akihubiri.
And He was journeying through cities and villages, teaching, and making His journey towards Jerusalem.
23 Mtu mmoja akamwuliza, “Je, Mwalimu, watu watakaookoka ni wachache?”
And one said to Him, Lord, are the saved few? And He said to them,
24 Yesu akawaambia, “Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; maana nawaambieni, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.
Agonize to enter in through the narrow gate: because many, I say unto you, will seek to enter in, and will not be able.
25 “Wakati utakuja ambapo mwenye nyumba atainuka na kufunga mlango. Ninyi mtasimama nje na kuanza kupiga hodi mkisema: Bwana, tufungulie mlango. Lakini yeye atawajibu: Sijui mmetoka wapi.
When the landlord may rise up, and close the door, and you may begin to stand without, and knock at the door, saying, Lord, open unto us; and responding he will say unto you, I know not whence you are.
26 Nanyi mtaanza kumwambia: Sisi ndio wale tuliokula na kunywa pamoja nawe; na wewe ulifundisha katika vijiji vyetu.
Then you will begin to say, We ate and drank in thy presence, and thou didst preach in our streets.
27 Lakini yeye atasema: Sijui ninyi mmetoka wapi; ondokeni mbele yangu, enyi nyote watenda maovu.
And he will say, I tell you, I know you not whence you are; depart from me, all you workers of iniquity.
28 Ndipo mtakuwa na kulia na kusaga meno, wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka na Yakobo, na manabii wote wapo katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mmetupwa nje!
And there shall be weeping and gnashing of teeth, when you shall see Abraham, and Isaac, and Jacob, and all the prophets, in the kingdom of God, and you cast out.
29 Watu watakuja kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini, watakuja na kukaa kwenye karamu katika Ufalme wa Mungu.
And they will come from the east and west, and the north and south, and will sit down in the kingdom of God.
30 Naam, wale walio wa mwisho watakuwa wa kwanza; na wale walio wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
And behold, the last shall be first, and the first shall be last.
31 Wakati huohuo, Mafarisayo na watu wengine walimwendea Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende mahali pengine, kwa maana Herode anataka kukuua.”
At that hour certain Pharisees came to Him, saying; Depart, and go hence: because Herod wishes to slay thee.
32 Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie huyo mbweha hivi: Leo na kesho ninafukuza pepo na kuponya wagonjwa, na siku ya tatu nitakamilisha kazi yangu.
And He said to them, Having gone, tell that fox, Behold, I cast out demons and perfect healings to-day and to-morrow, and on the third day I am made perfect.
33 Hata hivyo, kwa leo, kesho na kesho kutwa, ni lazima niendelee na safari yangu, kwa sababu si sawa nabii auawe nje ya Yerusalemu.
Moreover it behooves Me to travel to-day and to-morrow and the day following: because it does not behoove a prophet to perish outside of Jerusalem.
34 “Yerusalemu! We Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako pamoja kama kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, Lakini wewe umekataa.
O Jerusalem, Jerusalem, thou that killest the prophets, and stonest them that have been sent unto thee! how frequently did I wish to gather thy children, in the manner in which a hen doth gather her brood under her wings, and ye were not willing!
35 Haya, utaachiwa mwenyewe nyumba yako. Naam, hakika nawaambieni, hamtaniona mpaka wakati utakapofika mseme: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.”
Behold, your house is left unto you desolate. I say unto you, that you can see me no more, until it shall come to pass that you may say, Blessed is the One coming in the name of the Lord.

< Luka 13 >