< Luka 12 >

1 Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
Med tem ko se je bilo zbralo na tisoče ljudstva, tako, da so eden po drugem gazili, začne govoriti učencem svojim: Najprej se varujte kvasú Farizejskega, kteri je hinavstvo.
2 Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
Nič pa ni skritega, kar se ne bo odkrilo; in skrivnega, kar se ne bo zvedelo.
3 Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
Za to se bo to, kar ste pravili v temi, slišalo na svetlem; in kar ste na uho šepetali v kletih, oznanjevalo se bo na strehah.
4 “Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
Pravim pa vam prijateljem svojim: Ne bojte se jih, kteri ubijajo telo, a po tem ne morejo nič več storiti.
5 Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
Pokazal pa vam bom, koga se bojte: bojte se tistega, kteri ima oblast, po tem ko je ubil, zagnati v pekel. Dà, pravim vam, tega se bojte. (Geenna g1067)
6 Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
Ne prodaja li se pet vrabcev za dva solda! in ne eden od njih ni pozabljen pred Bogom.
7 Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
A vam so tudi lasje na glavi vsi razšteti. Ne bojte se torej; vi ste bolji od mnogo vrabcev.
8 “Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
Pravim vam pa: Vsak kdor bo spoznal mene pred ljudmí, spoznal bo tudi sin človečji njega pred angelji Božjimi;
9 Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
Kdor bo pa zatajil mene pred ljudmí, zatajil se bo pred angelji Božjimi.
10 “Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
In vsak, kdor reče besedo zoper sina človečjega, odpustila mu se bo; a kdor se zarotí zoper Duha svetega, ne bo mu se odpustilo.
11 “Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
Kedar vas pa popeljejo v shajališča in h gosposki in pred oblasti, ne skrbite, kako ali kaj bi odgovorili, ali kaj bi povedali:
12 Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
Kajti naučil vas bo Duh sveti tisti čas, kaj je treba reči.
13 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
Reče pa mu nekdo izmed ljudstva: Učenik, reci bratu mojemu, naj razdeli z menoj dedovino.
14 Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
On mu pa reče: Človek, kdo me je postavil za sodnika ali delilca med vama?
15 Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
In reče jim: Glejte in varujte se lakomnosti; kajti nikdor ne živí ob obilnosti imenja svojega.
16 Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
Pové jim pa priliko, govoreč: Nekemu človeku bogatemu obrodila je njiva;
17 Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
In premišljeval je v sebi, govoreč: Kaj bom storil, ko nimam kam spraviti letine svoje?
18 Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
Pa reče: To bom storil: podrl bom žitnice svoje, in naredil bom veče, in spravil bom tu vse pridelke svoje in blago svoje.
19 Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
Ter porečem duši svojej: Duša! veliko blaga imaš na veliko let; počivaj, jej, pij, veseli se.
20 Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
Reče pa mu Bog: Neumnež! to noč bom tirjal dušo tvojo od tebe; a kar si pripravil, čegavo bo?
21 Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
Tako, kdor sebi zaklade nabira, pa se ne bogati v Bogu.
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
Reče pa učencem svojim: Za to vam pravim, da ne skrbite za življenje svoje, kaj boste jedli; tudi za telo svoje ne, kaj boste oblekli.
23 Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
Življenje je več kakor hrana, in telo več kakor obleka.
24 Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
Poglejte krokarje, da ne sejejo, in ne žanjejo; kteri nimajo kleti ne žitnice, in Bog jih živí: koliko bolji ste vi od tic?
25 Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
Kdo od vas pa skrbeč more postavi svojej primakniti en komolec?
26 Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
Če torej tudi najmanjega ne morete, čemu skrbite za drugo?
27 Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
Poglejte lilije, kako rastejo; ne trudijo se in ne predejo; pravim vam pa: Tudi Solomon v vsej slavi svojej se ni oblekel, kakor teh ena.
28 Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
Če pa travo na polji, ktera danes stojí, a jutri se meče v peč, Bog tako oblači, koliko bolj vas, maloverni?
29 “Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
Tudi vi ne iščite, kaj boste jedli, ali kaj boste pili; in ne skrbite.
30 Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
Kajti vsega tega iščejo pogani: a oče vaš vé, da tega potrebujete.
31 Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
Nego iščite kraljestva Božjega, in vse to vam se bo pridalo.
32 “Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
Ne boj se, mala čreda! kajti volja je očeta vašega dati vam kraljestvo.
33 Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
Prodajte imenje svoje, in dajte miloščino. Napravite si mošnje, ktere ne ostaré, zaklad na nebesih, kteri ne izgine, kjer se tat ne približuje, in tudi molj ne razjeda.
34 Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
Kajti kjer je zaklad vaš, tam bo tudi srce vaše.
35 “Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
Bodi vam ledje opasano, in sveče prižgane;
36 muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
In vi podobni ljudém, kteri pričakujejo gospodarja svojega, kedaj se bo vrnil z ženitnine, da mu, kedar pride in potrka, precej odpró.
37 Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
Blagor tistim hlapcem, ktere bo našel gospodar, kedar pride, da čujejo. Resnično vam pravim, da se bo opasal in jih bo posadil, ter bo pristopil in jim bo stregel.
38 Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
In če pride o drugej straži, ali če o tretjej straži pride in bo našel tako, blagor tistim hlapcem.
39 Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
Vedite pa to, da ko bi vedel gospodar, o kterej straži bo prišel tat, čul bi, in ne bi dal podkopati hiše svoje.
40 Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
Za to bodite tudi vi pripravljeni; kajti sin človečji bo prišel ob uri, ko se vam ne bo dozdevalo.
41 Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
Reče pa mu Peter: Gospod, praviš li to priliko nam, ali vsem?
42 Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
Gospod pa reče: Kdo je torej zvesti in modri pristavnik, kterega je postavil gospodar nad družino svojo, naj jim daje hrano o svojem času?
43 Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
Blagor tistemu hlapcu, kterega bo našel gospodar, kedar pride, da tako dela.
44 Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
Resnično vam pravim, da ga bo postavil nad vsem imenjem svojim.
45 Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
Če pa reče ta hlapec v srcu svojem: Gospodarja mojega še ne bo! in začne pretepati hlapce in dekle, ter jesti in piti in pijančevati:
46 bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
Prišel bo gospodar tega hlapca o dnevu, ko ne pričakuje, in ob uri, ktere ne vé: in presekal ga bo, in del njegov bo položil z neverniki.
47 Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
Tisti pa hlapec, kteri je voljo gospodarja svojega vedel, pa se ni pripravil in tudi ni storil po volji njegovej, tepen bo zeló;
48 Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
A tisti, kteri ni vedel, pa je storil, kar je kazni vredno, tepen bo malo. Vsakemu pa, komur se je mnogo dalo, tirjalo se bo od njega mnogo; in komor so izročili mnogo, tirjali bodo od njega več.
49 “Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
Prišel sem, da vržem ogenj na zemljo, in kaj hočem, če se je uže užgal?
50 Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
Ali s krstom se imam krstiti, in kako britko mi je, dokler se ne dopolni!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
Menite li, da sem prišel, da dam na zemljo mir? Ne! pravim vam, nego razpor.
52 Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
Kajti odslej jih bo pet v enej hiši razprtih, trije z dvema, in dva s tremi.
53 Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
Oče se bo razprl s sinom, in sin z očetom; mati s hčerjo, in hčer z materjo; tašča s sneho svojo, in sneha s taščo svojo.
54 Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
Pravil je pa tudi ljudstvu: Kedar vidite oblak, da vzhaja od zahoda, precej pravite: Dež bo! in zgodí se tako.
55 Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
In kedar jug, da vleče, pravite: Vroče bo! in zgodí se.
56 Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
Hinavci! lice zemlje in neba véste razločevati: tega časa pa kako ne razločujete?
57 “Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
Za kaj pa tudi sami od sebe ne sodite, kar je prav?
58 Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
Kedar greš pa z zopernikom svojim k poglavarju, potrudi se po poti, da se ga rešiš: da te ne privleče k sodniku, in sodnik da te ne izročí beriču, in berič da te ne vrže v ječo.
59 Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”
Pravim ti: Ne boš izšel odtod, dokler ne plačaš tudi zadnjega solda.

< Luka 12 >