< Luka 12 >
1 Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
tadAnIM lokAH sahasraM sahasram Agatya samupasthitAstata ekaiko 'nyeSAmupari patitum upacakrame; tadA yIzuH ziSyAn babhASe, yUyaM phirUzinAM kiNvarUpakApaTye vizeSeNa sAvadhAnAstiSThata|
2 Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
yato yanna prakAzayiSyate tadAcchannaM vastu kimapi nAsti; tathA yanna jJAsyate tad guptaM vastu kimapi nAsti|
3 Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
andhakAre tiSThanato yAH kathA akathayata tAH sarvvAH kathA dIptau zroSyante nirjane karNe ca yadakathayata gRhapRSThAt tat pracArayiSyate|
4 “Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
he bandhavo yuSmAnahaM vadAmi, ye zarIrasya nAzaM vinA kimapyaparaM karttuM na zakruvanti tebhyo mA bhaiSTa|
5 Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna )
tarhi kasmAd bhetavyam ityahaM vadAmi, yaH zarIraM nAzayitvA narakaM nikSeptuM zaknoti tasmAdeva bhayaM kuruta, punarapi vadAmi tasmAdeva bhayaM kuruta| (Geenna )
6 Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
paJca caTakapakSiNaH kiM dvAbhyAM tAmrakhaNDAbhyAM na vikrIyante? tathApIzvarasteSAm ekamapi na vismarati|
7 Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
yuSmAkaM ziraHkezA api gaNitAH santi tasmAt mA vibhIta bahucaTakapakSibhyopi yUyaM bahumUlyAH|
8 “Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
aparaM yuSmabhyaM kathayAmi yaH kazcin mAnuSANAM sAkSAn mAM svIkaroti manuSyaputra IzvaradUtAnAM sAkSAt taM svIkariSyati|
9 Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
kintu yaH kazcinmAnuSANAM sAkSAnmAm asvIkaroti tam Izvarasya dUtAnAM sAkSAd aham asvIkariSyAmi|
10 “Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
anyacca yaH kazcin manujasutasya nindAbhAvena kAJcit kathAM kathayati tasya tatpApasya mocanaM bhaviSyati kintu yadi kazcit pavitram AtmAnaM nindati tarhi tasya tatpApasya mocanaM na bhaviSyati|
11 “Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
yadA lokA yuSmAn bhajanagehaM vicArakartRrAjyakartRNAM sammukhaJca neSyanti tadA kena prakAreNa kimuttaraM vadiSyatha kiM kathayiSyatha cetyatra mA cintayata;
12 Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
yato yuSmAbhiryad yad vaktavyaM tat tasmin samayaeva pavitra AtmA yuSmAn zikSayiSyati|
13 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
tataH paraM janatAmadhyasthaH kazcijjanastaM jagAda he guro mayA saha paitRkaM dhanaM vibhaktuM mama bhrAtaramAjJApayatu bhavAn|
14 Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
kintu sa tamavadat he manuSya yuvayo rvicAraM vibhAgaJca karttuM mAM ko niyuktavAn?
15 Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
anantaraM sa lokAnavadat lobhe sAvadhAnAH satarkAzca tiSThata, yato bahusampattiprAptyA manuSyasyAyu rna bhavati|
16 Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
pazcAd dRSTAntakathAmutthApya kathayAmAsa, ekasya dhanino bhUmau bahUni zasyAni jAtAni|
17 Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
tataH sa manasA cintayitvA kathayAmbabhUva mamaitAni samutpannAni dravyANi sthApayituM sthAnaM nAsti kiM kariSyAmi?
18 Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
tatovadad itthaM kariSyAmi, mama sarvvabhANDAgArANi bhaGktvA bRhadbhANDAgArANi nirmmAya tanmadhye sarvvaphalAni dravyANi ca sthApayiSyAmi|
19 Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
aparaM nijamano vadiSyAmi, he mano bahuvatsarArthaM nAnAdravyANi saJcitAni santi vizrAmaM kuru bhuktvA pItvA kautukaJca kuru| kintvIzvarastam avadat,
20 Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
re nirbodha adya rAtrau tava prANAstvatto neSyante tata etAni yAni dravyANi tvayAsAditAni tAni kasya bhaviSyanti?
21 Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
ataeva yaH kazcid Izvarasya samIpe dhanasaJcayamakRtvA kevalaM svanikaTe saJcayaM karoti sopi tAdRzaH|
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
atha sa ziSyebhyaH kathayAmAsa, yuSmAnahaM vadAmi, kiM khAdiSyAmaH? kiM paridhAsyAmaH? ityuktvA jIvanasya zarIrasya cArthaM cintAM mA kArSTa|
23 Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
bhakSyAjjIvanaM bhUSaNAccharIraJca zreSThaM bhavati|
24 Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
kAkapakSiNAM kAryyaM vicArayata, te na vapanti zasyAni ca na chindanti, teSAM bhANDAgArANi na santi koSAzca na santi, tathApIzvarastebhyo bhakSyANi dadAti, yUyaM pakSibhyaH zreSThatarA na kiM?
25 Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
aparaJca bhAvayitvA nijAyuSaH kSaNamAtraM varddhayituM zaknoti, etAdRzo lAko yuSmAkaM madhye kosti?
26 Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
ataeva kSudraM kAryyaM sAdhayitum asamarthA yUyam anyasmin kAryye kuto bhAvayatha?
27 Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
anyacca kAmpilapuSpaM kathaM varddhate tadApi vicArayata, tat kaJcana zramaM na karoti tantUMzca na janayati kintu yuSmabhyaM yathArthaM kathayAmi sulemAn bahvaizvaryyAnvitopi puSpasyAsya sadRzo vibhUSito nAsIt|
28 Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
adya kSetre varttamAnaM zvazcUllyAM kSepsyamAnaM yat tRNaM, tasmai yadIzvara itthaM bhUSayati tarhi he alpapratyayino yuSmAna kiM na paridhApayiSyati?
29 “Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
ataeva kiM khAdiSyAmaH? kiM paridhAsyAmaH? etadarthaM mA ceSTadhvaM mA saMdigdhvaJca|
30 Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
jagato devArccakA etAni sarvvANi ceSTanate; eSu vastuSu yuSmAkaM prayojanamAste iti yuSmAkaM pitA jAnAti|
31 Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
ataevezvarasya rAjyArthaM saceSTA bhavata tathA kRte sarvvANyetAni dravyANi yuSmabhyaM pradAyiSyante|
32 “Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
he kSudrameSavraja yUyaM mA bhaiSTa yuSmabhyaM rAjyaM dAtuM yuSmAkaM pituH sammatirasti|
33 Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
ataeva yuSmAkaM yA yA sampattirasti tAM tAM vikrIya vitarata, yat sthAnaM caurA nAgacchanti, kITAzca na kSAyayanti tAdRze svarge nijArtham ajare sampuTake 'kSayaM dhanaM saJcinuta ca;
34 Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
yato yatra yuSmAkaM dhanaM varttate tatreva yuSmAkaM manaH|
35 “Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
aparaJca yUyaM pradIpaM jvAlayitvA baddhakaTayastiSThata;
36 muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
prabhu rvivAhAdAgatya yadaiva dvAramAhanti tadaiva dvAraM mocayituM yathA bhRtyA apekSya tiSThanti tathA yUyamapi tiSThata|
37 Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
yataH prabhurAgatya yAn dAsAn sacetanAn tiSThato drakSyati taeva dhanyAH; ahaM yuSmAn yathArthaM vadAmi prabhustAn bhojanArtham upavezya svayaM baddhakaTiH samIpametya pariveSayiSyati|
38 Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
yadi dvitIye tRtIye vA prahare samAgatya tathaiva pazyati, tarhi taeva dAsA dhanyAH|
39 Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
aparaJca kasmin kSaNe caurA AgamiSyanti iti yadi gRhapati rjJAtuM zaknoti tadAvazyaM jAgran nijagRhe sandhiM karttayituM vArayati yUyametad vitta|
40 Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
ataeva yUyamapi sajjamAnAstiSThata yato yasmin kSaNe taM nAprekSadhve tasminneva kSaNe manuSyaputra AgamiSyati|
41 Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
tadA pitaraH papraccha, he prabho bhavAn kimasmAn uddizya kiM sarvvAn uddizya dRSTAntakathAmimAM vadati?
42 Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
tataH prabhuH provAca, prabhuH samucitakAle nijaparivArArthaM bhojyapariveSaNAya yaM tatpade niyokSyati tAdRzo vizvAsyo boddhA karmmAdhIzaH kosti?
43 Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
prabhurAgatya yam etAdRze karmmaNi pravRttaM drakSyati saeva dAso dhanyaH|
44 Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
ahaM yuSmAn yathArthaM vadAmi sa taM nijasarvvasvasyAdhipatiM kariSyati|
45 Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
kintu prabhurvilambenAgamiSyati, iti vicintya sa dAso yadi tadanyadAsIdAsAn praharttum bhoktuM pAtuM madituJca prArabhate,
46 bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
tarhi yadA prabhuM nApekSiSyate yasmin kSaNe so'cetanazca sthAsyati tasminneva kSaNe tasya prabhurAgatya taM padabhraSTaM kRtvA vizvAsahInaiH saha tasya aMzaM nirUpayiSyati|
47 Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
yo dAsaH prabherAjJAM jJAtvApi sajjito na tiSThati tadAjJAnusAreNa ca kAryyaM na karoti sonekAn prahArAn prApsyati;
48 Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
kintu yo jano'jJAtvA prahArArhaM karmma karoti solpaprahArAn prApsyati| yato yasmai bAhulyena dattaM tasmAdeva bAhulyena grahISyate, mAnuSA yasya nikaTe bahu samarpayanti tasmAd bahu yAcante|
49 “Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
ahaM pRthivyAm anaikyarUpaM vahni nikSeptum Agatosmi, sa ced idAnImeva prajvalati tatra mama kA cintA?
50 Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
kintu yena majjanenAhaM magno bhaviSyAmi yAvatkAlaM tasya siddhi rna bhaviSyati tAvadahaM katikaSTaM prApsyAmi|
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
melanaM karttuM jagad Agatosmi yUyaM kimitthaM bodhadhve? yuSmAn vadAmi na tathA, kintvahaM melanAbhAvaM karttuMm Agatosmi|
52 Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
yasmAdetatkAlamArabhya ekatrasthaparijanAnAM madhye paJcajanAH pRthag bhUtvA trayo janA dvayorjanayoH pratikUlA dvau janau ca trayANAM janAnAM pratikUlau bhaviSyanti|
53 Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
pitA putrasya vipakSaH putrazca pitu rvipakSo bhaviSyati mAtA kanyAyA vipakSA kanyA ca mAtu rvipakSA bhaviSyati, tathA zvazrUrbadhvA vipakSA badhUzca zvazrvA vipakSA bhaviSyati|
54 Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
sa lokebhyoparamapi kathayAmAsa, pazcimadizi meghodgamaM dRSTvA yUyaM haThAd vadatha vRSTi rbhaviSyati tatastathaiva jAyate|
55 Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
aparaM dakSiNato vAyau vAti sati vadatha nidAgho bhaviSyati tataH sopi jAyate|
56 Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
re re kapaTina AkAzasya bhUmyAzca lakSaNaM boddhuM zaknutha,
57 “Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
kintu kAlasyAsya lakSaNaM kuto boddhuM na zaknutha? yUyaJca svayaM kuto na nyASyaM vicArayatha?
58 Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
aparaJca vivAdinA sArddhaM vicArayituH samIpaM gacchan pathi tasmAduddhAraM prAptuM yatasva nocet sa tvAM dhRtvA vicArayituH samIpaM nayati| vicArayitA yadi tvAM praharttuH samIpaM samarpayati praharttA tvAM kArAyAM badhnAti
59 Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”
tarhi tvAmahaM vadAmi tvayA niHzeSaM kapardakeSu na parizodhiteSu tvaM tato muktiM prAptuM na zakSyasi|