< Luka 12 >

1 Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
In the meantime, myriads of the multitude having gathered together, So that they trode on one another, He began to speak to His disciples first; Take heed unto yourselves from the leaven of the Pharisees, which is hypocrisy.
2 Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
But there is nothing hidden, which shall not be revealed: and concealed, that shall not be made known.
3 Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
Therefore so many things as you spoke in the darkness shall be heard in the light; and whatsoever you spoke in the ear in the secret chambers shall be proclaimed upon the houses.
4 “Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
And I say unto you, my friends, Be not afraid of those killing the body, and after these things, having nothing more to do.
5 Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
But I will show you whom you must fear: Fear him, who after he kills has power to cast into hell. Yea, I say unto you, Fear him. (Geenna g1067)
6 Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
Are not five sparrows sold for two pennies? and one of them is not forgotten before God.
7 Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
But even the hairs of your head are all numbered. Fear not: ye are more important than many sparrows.
8 “Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
But I say unto you, that every one who may confess me before the people, the Son of man will also confess him before the angels of God.
9 Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
But the one denying me before the people will be denied before the angels of God.
10 “Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
And every one who shall speak a word against the Son of man, it shall be forgiven him: but to him having blasphemed against the Holy Ghost, it shall not be forgiven.
11 “Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
But when they may carry you into the synagogues, and tribunals, and authorities; do not be solicitous as to what you may apologize, or what you may say:
12 Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
for the Holy Spirit will teach you in that hour the things which it behooveth you to speak.
13 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
And a certain one from the multitude said to Him, Teacher, speak to my brother, to divide the inheritance with me.
14 Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
And He said to him; Man, who established me judge or a divider over you?
15 Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
And He said to them, See, and beware of all covetousness: because his life is not in that which aboundeth to any one, from those things belonging to him.
16 Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
He spake a parable to them, saying, The farm of a certain rich man was very productive:
17 Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
and he was reasoning in himself, saying, What shall I do, because I have no place where I shall store my fruits?
18 Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
And he said, I will do this: I will take down my barns, and build greater, and there I will gather all my fruits and my goods.
19 Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
And I will say to my soul, Soul, thou hast much goods laid up for many years; take thine ease, eat, drink, be merry.
20 Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
But God said to him, Thou fool, this night they are demanding thy soul from thee; and to whom shall those things which thou hast prepared, belong?
21 Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
So is every one laying up treasure for himself, and not rich toward God.
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
And He spoke to His disciples, Therefore I say unto you, Be not solicitous for your soul, what you may eat; nor for your body, what you may put on.
23 Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
The soul is more than food, and the body more than raiment.
24 Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
Observe the ravens, because they neither sow nor reap; to which there is no storehouse nor barn, and God feeds them; are you not much better than the fowls?
25 Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
And which one of you being solicitous is able to add one moment to his existence?
26 Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
If then you are powerless in the smallest matter, why are you solicitous about other things?
27 Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
Observe the lilies, how they toil not, neither do they spin: and I say unto you, That Solomon in all his glory was not arrayed as one of these.
28 Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
And if God so clothes the verdure flourishing in the fields to-day, and to-morrow cast into the oven; how much more are you, O ye of little faith?
29 “Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
And do not seek what you may eat, and what you may drink, and with what you are clothed;
30 Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
for the heathens of the world are seeking after all these things: but your Father knows that you have need of these things.
31 Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
Moreover seek His kingdom and these things shall be added unto you.
32 “Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
Fear not, little flock; because your Father is well pleased to give you the kingdom.
33 Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
Sell your possessions and give alms; make for yourselves purses that will not get old, and treasure in the heavens which can not be stolen, where the thief does not draw nigh, nor the moth corrupt.
34 Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
For where your treasure is, there your heart will be.
35 “Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
Let your loins be girted, and your lamps burning;
36 muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
and be you like unto men waiting for their lord, when he may rise up from the marriage feast; in order that, coming and knocking, they may open unto him immediately.
37 Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
Blessed are those servants, whom the lord having come will find watching: truly I say unto you, that he will gird himself, and have them sit down, and having come will serve them.
38 Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
If at the second, and third, watch he may come, happy are ye.
39 Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
Know this, that if the landlord knew at what hour the thief cometh, he would not have permitted his house to be broken into.
40 Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
Be ye also ready: because at an hour you do not think the Son of man cometh.
41 Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
And Peter said to Him, Lord, do you speak this parable to us, or to all?
42 Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
The Lord said, Who then is the faithful, wise steward, whom the lord will establish over his house-hold, to give them their food in season?
43 Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
Happy is that servant, whom his lord having come shall thus find watching.
44 Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
Truly I say unto you, that he will establish him over all his possessions.
45 Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
But if that servant may say in his heart, my lord delayeth his coming, and may begin to smite the servants and handmaidens, and to eat and drink, and be drunken;
46 bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
the lord of that servant will come in a day in which he does not expect, and in an hour in which he does not know, and will cut him off, and will appoint his part with the unbelievers.
47 Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
But that servant knowing the will of his lord, and not preparing or doing according to his will, shall be beaten with many stripes.
48 Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
But the one not knowing, and doing things worthy of stripes, shall be beaten with few. But to every one to whom much is given, much will be required of him: and to whom they commit much, of him they will ask the more.
49 “Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
I have come to send fire on the earth; and what do I will, if it is already kindled?
50 Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
And I have a baptism to be baptized with; and how am I straitened till it may be perfected!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
Do you think that I have come to give peace on the earth? I say unto you, Nay, but division.
52 Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
For from now, there shall be five in one house divided, three shall be divided against two, and two against three:
53 Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
the father against the son, and the son against the father; and the mother against the daughter, and the daughter against the mother; the mother-in-law against the daughter-in-law, and the daughter-in-law against the mother-in-law.
54 Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
And he also spoke to the multitudes, When you may see a cloud rising from the west, you immediately say, that the rain cometh; and it is so:
55 Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
and when the south wind is blowing, you say, that it will be hot; and it is so.
56 Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
You hypocrites, you know how to discern the face of the earth and the firmament; and how do you not discern this time?
57 “Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
Why do you not judge righteous judgment, even with reference to yourselves?
58 Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
For as you go with your adversary to the ruler, give attention on the way that you be reconciled with him; lest he may deliver you to the judge, and the judge shall turn you over to the officer, and the officer will cast you into prison.
59 Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”
I say unto you, You can by no means come out thence, till you have even paid the last mite.

< Luka 12 >