< Luka 12 >
1 Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
In the meantime so many thousands of people had gathered that they were stepping on each another. Jesus began speaking first to his disciples. “Beware the yeast of the Pharisees—hypocrisy.
2 Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
For there's nothing hidden that won't be revealed, nothing secret that won't be made known.
3 Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
Whatever you have said in the dark will be heard in the light, and whatever you whispered in private will be announced from the rooftops.
4 “Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
I tell you, my friends, don't be afraid of those who kill the body, for once they've done that there's no more they can do.
5 Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna )
Let me make it clear whom you should be afraid of. You should be afraid of the one who after he has killed has the power to dispose of them in Gehenna. That's the one you should be afraid of. (Geenna )
6 Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
Aren't five sparrows sold for two pennies? But God doesn't forget a single one of them.
7 Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
Even the hairs on your head have been counted. Don't be afraid—you're worth more than many sparrows!
8 “Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
I tell you the truth, those who declare they belong to me, the Son of man will also declare they belong to him before God's angels,
9 Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
but those who deny me will be denied before God's angels.
10 “Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Everyone who speaks against the Son of man will be forgiven, but anyone who blasphemes against the Holy Spirit will not be forgiven.
11 “Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
When you're brought to trial before synagogues, rulers, and authorities, don't worry about how to defend yourself, or what you should say.
12 Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
The Holy Spirit will teach you at that time what's important to say.”
13 Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
Someone in the crowd asked Jesus, “Teacher, please tell my brother to share the inheritance with me.”
14 Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
“My friend,” Jesus replied, “Who appointed me as your judge to decide how your inheritance should be divided?” He told the people,
15 Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
“Watch out, and beware of all greedy thoughts and actions, for a person's life isn't summed up by all the things they own.”
16 Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
Then he told them a story as an illustration. “Once there was a rich man who owned land that was very productive.
17 Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
The man said to himself, ‘What shall I do? I've nowhere to store my crops.
18 Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
I know what I'll do,’ he decided. ‘I'll pull down my barns and build bigger ones, and then I'll be able to store all my crops and everything I own.
19 Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
Then I'll tell myself: You have enough to live on for many years, so take life easy: eat, drink, and enjoy yourself!’
20 Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
But God said to him, ‘You foolish man! Your life will be demanded back this very night, and then who will get everything you've stored up?’
21 Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
This is what happens to people who hoard up wealth for themselves but are not rich as far as God is concerned.”
22 Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
Jesus told his disciples, “That's why I tell you don't worry about life, about what to eat, or about what clothes you should wear.
23 Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
Life is about more than food, and the body is about more than wearing clothes.
24 Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
Look at the ravens. They don't sow or reap, they don't have any storerooms or barns, but God feeds them. And you're far more valuable than birds!
25 Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
Can you add an hour to your life by worrying about it?
26 Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
If you can't do anything about such small things, why worry about the rest?
27 Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
Think of the lilies and how they grow. They don't work, and they don't spin thread for clothes, but I tell you, not even Solomon in all his glory was as beautifully dressed as one of them.
28 Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
So if God clothes the fields with such beautiful flowers, which are here today but gone tomorrow when they are burned in a fire to heat an oven, how much more will God clothe you, you who have so little trust!
29 “Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
Don't be concerned about what you're going to eat or drink—don't worry about it.
30 Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
These are all things that people in the world worry about, but your Father knows you need them.
31 Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
Search for God's kingdom, and you'll be given these things as well.
32 “Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
Don't be afraid, little flock, for your Father is happy to give you the kingdom.
33 Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
Sell what you have, and give the money to the poor. Get yourselves purses that don't wear out: treasure in heaven that will never run out, where no thief can steal it and no moth can destroy it.
34 Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
For what you value the most shows who you really are.
35 “Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
Be dressed and ready, and keep your lamps lit,
36 muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
like servants waiting for their master when he returns from his wedding feast, prepared to open the door quickly for him when he comes and knocks.
37 Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
How good it will be for those servants that the master finds watching when he returns. I tell you the truth, he will get dressed, have them sit down for a meal, and will come and serve them himself!
38 Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
Even if he comes at midnight, or just before dawn—how good for them if he finds them watching and ready!
39 Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
But remember this: if the master knew when a thief was coming, he would keep watch, and not allow his house be broken into.
40 Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
You must also be ready, for the Son of man is coming when you don't expect him.”
41 Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
“Is this story you're telling just for us, or for everyone?” Peter asked.
42 Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
The Lord replied, “Who then is the trustworthy and wise manager, the one person in the household that the master puts in charge to share out their food at the right time?
43 Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
It will be good for that servant when his master returns and finds him doing what he should.
44 Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
I tell you the truth, the master will put that servant in charge of everything.
45 Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
But what if the servant were to say to himself, ‘My master is taking a long time in coming,’ and then starts beating the other servants, both men and women, feasting and getting drunk?
46 bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
That servant's master will return unexpectedly one day at a time he wasn't aware of, and will punish him severely, treating him as totally untrustworthy.
47 Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
That servant who knew what his master wanted and yet didn't get ready or follow his instructions, will be beaten severely;
48 Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
but the servant who didn't know and did things deserving punishment will be beaten only lightly. From those who are given much, much will be required, and from those who are entrusted with more, more will be demanded.
49 “Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
I have come to set the earth on fire, and I really wish it was already burning!
50 Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
But I have a baptism to go through, and I'm in agony, wishing it was over!
51 Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
Do you think that I came to bring peace on earth? No, I tell you, I bring division.
52 Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
From now on, if there are five in a family, they will be divided against each other: three against two, and two against three.
53 Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
They will be divided against each other—father against son, son against father, mother against daughter, daughter against mother, mother-in-law against daughter-in-law, and daughter-in-law against mother-in-law.”
54 Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
Then Jesus spoke to the crowds. “When you see a cloud rising in the west, you immediately say, ‘a rain-shower's coming,’ and it happens.
55 Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
When a south wind blows, you say ‘it's going to be hot,’ and it is.
56 Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
You hypocrites, how is it that you know how to rightly interpret the weather but you don't know how to interpret the present time?
57 “Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
Why don't you think for yourselves and judge what's the right thing to do?
58 Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
As you go with your accuser to the magistrate, on the way you should be working on a settlement. Otherwise you may be dragged before the judge, and the judge hand you over to the officer, and the officer throw you into prison.
59 Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”
I tell you, you won't get out until you've paid the last penny.”