< Luka 10 >
1 Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
After these things the Lord chose seventy others also, and sent them out two by two before His face, into every place and city, where He was about to come.
2 Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
And He said to them, The harvest is indeed great, but the laborers are few: therefore pray you the Lord of the harvest, that He may send forth laborers into His harvest.
3 Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
Go: behold, I send you forth as lambs in the midst of wolves.
4 Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
Take neither purse, nor valise, nor sandals: salute no one by the way.
5 Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
Into whatsoever house you may enter, first say, Peace be unto this house.
6 Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
And if the son of peace may be there, your peace shall rest upon it: but if not, it shall return unto you.
7 Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
Abide in the same house, eating and drinking those things which are with them: for the laborer is worthy of his hire. Go not from house to house.
8 Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
Into whatsoever city you may enter and they may receive you, eat those things which are placed by you:
9 Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
and heal the sick who are in it, and say to them, The kingdom of God has come nigh unto you.
10 Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
And into whatsoever city you may enter, and they may not receive you, having come out into the streets of the same, say,
11 Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
Even the dust from your city, that cleaveth to our feet, do we wipe off against you: but know this, that the kingdom of God is at hand.
12 Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
For I say unto you, that it will be more tolerable in that day for Sodom than for that city.
13 “Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
Woe unto thee, Chorazin! woe unto thee, Bethsaida! for if the mighty works which were wrought in you had been in Tyre and Sidon, they would have repented long ago, sitting down in sackcloth and ashes.
14 Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
Moreover it shall be more tolerable for Tyre and Sidon in the judgment than for you.
15 Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs )
And thou, Capernaum, art thou not exalted up to heaven? thou shalt be cast down to Hades. (Hadēs )
16 Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
He that heareth you heareth me; he that rejecteth you rejecteth me; and he that rejecteth me rejecteth Him that sent me.
17 Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
And the seventy returned with joy, saying, Lord, even the demons are subordinated to us in thy name.
18 Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
And He said to them, I saw Satan having fallen as the lightning from heaven.
19 Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
Behold I have given you authority to tread upon serpents and scorpions, and over all the power of the enemy; and nothing shall hurt you.
20 Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
Moreover do not rejoice in this, that the spirits are subject unto you; but rejoice that your names are written in the heavens.
21 Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
At the same hour He rejoiced in the Holy Spirit, and said, I praise thee, O Father, Lord of the heaven and the earth, because thou hast hidden these things from the wise and prudent, and revealed them to babes: yea, Father, because it was thus pleasing in thy sight.
22 Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
And turning to His disciples, He said, All things have been delivered to me by my Father: and no one knoweth who the Son is, except the Father; and who the Father is, except the Son, and he to whom He may wish to reveal Him.
23 Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
And turning to His disciples, privately He said, Happy are your eyes, seeing those things which you see.
24 Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
For I say unto you, that many kings and prophets desired to see those things which you see, and saw them not; and to hear those things which you hear, and heard them not.
25 Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios )
And behold, a certain lawyer stood up tempting Him, saying, Teacher, having done what shall I inherit eternal life? (aiōnios )
26 Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
He said to him, What has been written in the law? how do you read it?
27 Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
And he responding said, Thou shalt love the Lord thy God with divine love from all thy heart, and with all thy soul, and with all thy strength, and with all thy mind; and thy neighbor as thyself.
28 Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
And He said to him, You answered correctly: do this, and you shall live.
29 Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
But he, wishing to justify himself, said to Jesus, And who is my neighbor?
30 Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
Jesus responding said, A certain man was going down from Jerusalem to Jericho; and fell among thieves, who indeed having stripped him of his raiment, administered blows, went away, leaving him half dead.
31 Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
And by chance a certain priest came down that way: and seeing him, passed by on the other side.
32 Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
And likewise also a Levite, being at the place, coming and seeing, passed by on the other side.
33 Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
And a certain Samaritan, on a journey, came near him: and seeing, had compassion on him,
34 Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
and having come to him, he bound up his wounds, pouring in oil and wine: and having mounted him on his own beast, carried him to a tavern, and cared for him.
35 Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
And on the morrow, taking out two denaria, gave them to the host, and said, Care for him; and whatsoever you expend in addition, on my return, I will pay you.
36 Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
Which one of these three seems to you to have been the neighbor of him who fell among the thieves?
37 Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
And he said, The one having done mercy with him. And Jesus said to him, Go, thou, and do likewise.
38 Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
And it came to pass while they were going round, He also came into a certain village: and a certain woman by name Martha received Him into her house.
39 Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
And there was a sister to her called Mary, who indeed sitting down at the feet of the Lord, continued to hear his word:
40 Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
and Martha was very busy about much serving. And standing over Him, she said, Lord, is there no care to thee that my sister has left me to serve alone? then say to her that she must assist me.
41 Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
And the Lord responding said to her, Martha, Martha, you are solicitous and encumbered concerning many things:
42 Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”
but there is need of one thing: for Mary has chosen the good part, which shall not be taken from her.