< Luka 10 >

1 Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
After this, the Lord appointed seventy other disciples, and sent them in pairs to every town and place that he planned to visit.
2 Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
“The harvest is large, but the number of workers is small,” he told them. “Pray to the Lord of the harvest to send workers to his harvest fields.
3 Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
So get on your way: I'm sending you like sheep among wolves.
4 Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
Don't take any money or a bag or extra sandals, and don't spend time chatting with people you meet.
5 Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
Whatever house you enter, first of all say, ‘May this house have peace.’
6 Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
If there's a peaceful person living there, then your peace will rest on them; if not, it will return to you.
7 Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
Stay in that house, eating and drinking whatever they give you, for a worker deserves to be paid. Don't go from house to house.
8 Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
If you enter a town and the people there welcome you, then eat what's set before you
9 Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
and heal those who are sick. Tell them, ‘God's kingdom has come to you.’
10 Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
But if you enter a town and the people there don't welcome you, go through their streets telling them,
11 Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
‘We are wiping off even the dust from your town that clings to our feet to show you our disapproval. But you should recognize this: God's kingdom has come.’
12 Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
I tell you, in the Day of Judgment it will be better for Sodom than for such a town.
13 “Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
Shame on you Korazin! Shame on you Bethsaida! For if the miracles you saw happen had happened in Tyre and Sidon they would have repented a long time ago, and they would be sitting in sackcloth and ashes.
14 Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
That's why in the judgment it will be better for Tyre and Sidon than for you.
15 Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
And you, Capernaum, you won't be exalted to heaven; you will go down to Hades. (Hadēs g86)
16 Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
Anyone who hears you hears me, and anyone who rejects you rejects me. But anyone who rejects me rejects the one who sent me.”
17 Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
The seventy disciples returned in great excitement, saying, “Lord, even the demons do what we tell them in your name!”
18 Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
Jesus replied, “I saw Satan fall like lightning from heaven.
19 Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
Yes, I have given you power to tread on snakes and scorpions, and to overcome all the enemy's strength, and nothing will harm you.
20 Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
But don't take delight that the spirits do what you tell them—just be glad that your names are written in heaven.”
21 Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
At that moment Jesus was filled with the joy of the Holy Spirit, and said, “I thank you Father, Lord of heaven and earth, for you hid these things from the wise and clever people and revealed them to children! Yes, Father, you were pleased to do it in this way.
22 Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
My Father has handed over everything to me. No one understands the Son except the Father, and no one understands the Father except the Son, and those to whom the Son chooses to reveal him.”
23 Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
When they were by themselves Jesus turned to the disciples and told them, “Those who see what you're seeing should be really happy!
24 Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
I tell you, many prophets and kings have wanted to see what you're seeing, but they didn't see, and wanted to hear the things you're hearing, but didn't hear.”
25 Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
Once an expert in religious law stood up and tried to trap Jesus. “Teacher,” he asked, “What do I have to do to gain eternal life?” (aiōnios g166)
26 Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
“What is written in the law? How do you read it?” asked Jesus.
27 Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
“You shall love the Lord your God with your whole heart, and your whole spirit, and your whole strength, and your whole mind; and love your neighbor as yourself,” the man replied.
28 Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
“You're right,” Jesus told him. “Do this, and you will live.”
29 Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
But the man wanted to vindicate himself, so he asked Jesus, “And who is my neighbor?”
30 Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
Jesus replied, saying, “A man was going down from Jerusalem to Jericho. He was attacked by robbers who stripped him and beat him, and left him for dead.
31 Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
It so happened that a priest was going the same way. He saw the man, but he passed by on the other side of the road.
32 Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
Then a Levite came along. But when he got to the place and saw the man, he also passed by on the other side.
33 Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
Finally a Samaritan man came along. As he passed by, he saw the man and felt sorry for him.
34 Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
He went over and treated the man's wounds with oil and wine, and bandaged them. Then he placed the man on his own donkey and took him to an inn where he took care of him.
35 Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
The next day he gave two denarii to the innkeeper and told him, ‘Take care of him, and if you spend more than this, I'll pay you back when I return.’
36 Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
Which one of these three do you think was a neighbor to the man who was attacked by robbers?”
37 Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
“The one who showed him kindness,” the man replied. “Go and do the same,” Jesus told him.
38 Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
While they were on their way, Jesus arrived at a village, and a woman called Martha invited him to her home.
39 Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
She had a sister called Mary, who sat at the Lord's feet and listened to his teaching.
40 Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
Martha was concerned about all that needed to be done to prepare the meal, so she came to Jesus and said, “Master, don't you care that my sister has left me to do all the work by myself? Tell her to come and help me!”
41 Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
“Martha, Martha,” the Lord replied, “you're worried and upset about all this.
42 Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”
But only one thing is really necessary. Mary has chosen the right thing, and it shall not be taken away from her.”

< Luka 10 >