< Yuda 1 >
1 Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo.
Mi Yahuza urere Uyesu, uhenu Uyakubu uhana an desa a titti we anu insa tize ta Asere amu riba, an desa Yesu ma zauka we.
2 Nawatakieni huruma, amani na upendo kwa wingi.
Ugoggoni, unata iriba, nan uhem vat ti cukuno anyimo ashi.
3 Ndugu wapenzi, wakati nimo katika jitihada ya kuwaandikieni juu ya ule wokovu tunaoshiriki sote, nimeona lazima ya kuwaandikieni na kuwahimizeni mwendelee kupigana kwa ajili ya imani ambayo Mungu amewajalia watu wake mara moja tu kwa wakati wote.
Shi nihenu, mazi gusi inda nyertike shi ni ba, a banga ubura uru ugino me, haru vat nan shi, ine ini ma ira ya wuna uri in nyertike shi in nya shi tize, nyani ace ahira u inso iriba igono me sa anya ana lau ka'inde cas sarki ukinki.
4 Maana watu wasiomcha Mungu wamepata kujiingiza kwa siri miongoni mwetu, watu ambao, kwa faida ya maisha yao mabaya, wanaupotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu na kumkana Yesu Kristo aliye peke yake kiongozi na Bwana wetu. Maandiko Matakatifu yalikwisha bashiri tangu awali hukumu inayowangojea watu hao.
Aye anyimo ashi me wa ribe nihunzi andesa datti unu tubanaceki we anu zatu utarsa Asere, anu kurzuzo utize ta Asere imumu ini basa, wa gasiwe vana u'inde wa Asere.
5 Nataka kuwakumbusheni mambo fulani ambayo mmekwisha yajua: kumbukeni jinsi Bwana alivyowaokoa watu wa Israeli na kuwatoa katika nchi ya Misri, lakini baadaye aliwaangamiza wale ambao hawakuamini.
Ana me in nyara ni ringi shi, isa rusa vat mum, Asere a burin duru anyimo Umasar, vat in ani me ma huu an desa wa game uhem in me.
6 Na, malaika ambao hawakuridhika na cheo chao, wakayaacha makao yao ya asili, Mungu amewafunga gizani kwa minyororo ya milele wahukumiwe Siku ile kuu. (aïdios )
Ibe ikadura daa wa benki ace awe ba, wa ceki ahira aticukum tu we me, ma ceki we anyimo inyang nan mare ma bibit uhan a uwui sa madi kode avi imum me sa ma bira. (aïdios )
7 Kumbukeni pia Sodoma na Gomora, na miji ya kandokando yake; wenyeji wake walifanya kama wale malaika; walifanya uzinzi na mambo yaliyo kinyume cha maumbile, wakapewa hukumu ya moto wa milele, iwe onyo kwa watu wote. (aiōnios )
Ane ani usaduma nan Ugwamrata, nan ti pin sa ti raa mamu nan we, an desa wareki acen aweme utarsa ahana e nan katuma kani pum, a bezi we barki ukasu wa anu wa iri nirere sa wa zinu sa me anyimo ura. (aiōnios )
8 Hivyo ndivyo pia walivyo watu hawa. ndoto zao huwaongoza katika kuichafua miili yao wenyewe, kuyadharau mamlaka ya Mungu na kuvitukana viumbe vitukufu vya huko juu.
Ane ani ana tiroo, wa mu cara apumnawe me nin, wa gaa we utarsa uti gomo wazini boo tize ti buri a hira ana je.
9 Hata Mikaeli, malaika mkuu, hakufanya hivyo. Katika ule ubishi kati yake na Ibilisi waliobishana juu ya mwili wa Mose, Mikaeli hakuthubutu kumhukumu Ibilisi kwa matusi; ila alisema: “Bwana mwenyewe na akukaripie.”
Uganiya sa bibe bikadura Mika'ilu ma zin unu zito in bibe bi buri, wazin matara ahira ikizi i Musa, me Muka, ilu daki ma wu debe u nya na ma buki tize ti bit ba, me dai ma gu Asere aceki we ani me.
10 Lakini watu hawa hutukana chochote wasichokielewa; mambo yaleyale wanayoyajua kwa silika kama vile wanyama wanayoyajua ndiyo yanayowaangamiza.
Anu agino me daki wa hem vat ini mum be sa da wa tinka ba, barki imum be sa wa rusa anyimo ani pum wazi gusi izenki unu dira uni ce, una iwono iwe ya zigino me.
11 Ole wao! Watu hao wamefuata mwenendo uleule wa Kaini. Kwa ajili ya fedha, wamejiingiza katika mkosi uleule wa Baalamu. Wameasi kama Kora alivyoasi na wameangamizwa kama yeye alivyoangamizwa.
Wadi ziti wa tarsa iriba i Kayinu, wa tarsa una u hunne me barki imumu iriba iwe wa kuri wa ribe iwono barki wazi gbas kasi kora.
12 Kwa makelele yao yasiyo na adabu, watu hao ni kama madoa machafu katika mikutano yenu ya karamu ya Bwana. Hujipendelea wao wenyewe tu, na wako kama mawingu yanayopeperushwa huko na huko na upepo bila ya kuleta mvua. Wao ni kama miti isiyozaa matunda hata wakati wa majira yake, wamekufa kabisa.
Ana gino me wazi gusi tinaa ti rizizo tini anyimo ani ori nishi me nan nu uhem wazi gusi matiti mu zatu uyozo in ma'ino, wa wijo vat gusi ti kbeki sa aruba.
13 Watu hao ni kama mawimbi makali ya bahari, na matendo yao ya aibu yanaonekana dhahiri kama vile mapovu ya mawimbi. Wao ni kama nyota zinazotangatanga, ambao Mungu amewawekea mahali pao milele katika giza kuu. (aiōn )
Wazi gusi maronkomi mamu 'i. Wazi gusi iwiran ya sesere wa haba wa haba ane ani a inki we har iwono. (aiōn )
14 Henoki, ambaye ni babu wa saba tangu Adamu, alibashiri hivi juu ya watu hawa: “Sikilizeni! Bwana atakuja pamoja na maelfu ya malaika wake watakatifu
Anu cangi desa mamani unu Usunare adumo Adamu me ma ma reki tizze ahira anu agi Asere a'aye ina nu utarsa umeme gbardang.
15 kutoa hukumu juu ya binadamu wote, kuwahukumu wote kwa ajili ya matendo yao yote maovu waliyotenda na kwa ajili ya maneno yote mabaya ambayo watu waovu walimkashifu nayo.”
Barki ma bezi iriba imeme ahira kode vi ma kuri bezi anu zatu utarsa Asere sa wa wuzi imum be sa iriba iwe ya hem nan tizze ti buri sa buu ti zatu tame Asere.
16 Watu hawa wananung'unika daima na kuwalaumu watu wengine. Hufuata tamaa zao mbaya, hujigamba na kuwasifu watu wengine mno kusudi wafaulu katika mipango yao.
Anaa gino me we wani ana tize ti muriba, anu hunzizebace, anu tarsa ma ree wa nonzo ana je barki wa kem ire imum ahira aweme.
17 Lakini ninyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali ni mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo.
Shi, nihenu ringi ni tizze sa anu Yesu Asere aru wa busi shi.
18 Waliwaambieni: “Siku za mwisho zitakapofika, watatokea watu watakaowadhihaki ninyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya.”
Wa gun shi, umara une adi kem aye anyimo ashi me sa wadi, zunzi shi anu tarsa une da Asere ba.
19 Hao ndio watu wanaosababisha mafarakano, watu wanaotawaliwa na tamaa zao za kidunia, watu wasio na Roho wa Mungu.
Aye wadi cukuno anu harsa anu henu, anu tarsa muriba muwe, wa zo me in bibe biriri ba.
20 Lakini ninyi, wapenzi wangu, endeleeni kujijenga kikamilifu katika imani yenu takatifu. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu,
Shi nihenu, inta nin u'inko iriba ishi me gangan imumu ihuma, i wuzi birigira anyimo bibe biriri.
21 na kubaki katika upendo wa Mungu, mkiwa mnamngojea Bwana wetu Yesu Kristo awapeni uzima wa milele kwa huruma yake. (aiōnios )
onno unu hem me sa Asere ahem in haru i insi aje in ni mum be sa ogomo Asere madi wuzin duru uhana uwui uge be sa madi e. (aiōnios )
22 Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka;
Kunna ni ugogoni wan desa da wa nya iriba ba.
23 waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni; na kwa wengine muwe na huruma pamoja na hofu, lakini chukieni hata mavazi yao ambayo yamechafuliwa na tamaa zao mbaya.
Izinu bursa aye, usuzo aye anyimo ura, aye i kunna ugogoni uwe, in biyaubi hira uzenzen utirunga tiwe me nan iribaniwe me ya nyimo nipum.
24 Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta ninyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake,
Ana me an desa ma bari ma buri we, kati wa piliko, ma kuri ma witi shi anu zatu umadini ini riba irum.
25 kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina. (aiōn )
Ahira Asere cas unu bura uru, usuro uvana umeme Yesu, ninonzo, ubari, tigomo ti cukuno ahira me datti utuba nan ana me nan uhana aje, ca i cukuno anime. (aiōn )