< Yohana 9 >

1 Yesu alipokuwa akipita alimwona mtu mmoja, kipofu tangu kuzaliwa.
tataH paraM yIshurgachChan mArgamadhye janmAndhaM naram apashyat|
2 Basi, wanafunzi wakamwuliza, “Mwalimu! Ni nani aliyetenda dhambi: mtu huyu, ama wazazi wake, hata akazaliwa kipofu?”
tataH shiShyAstam apR^ichChan he guro naroyaM svapApena vA svapitrAH pApenAndho. ajAyata?
3 Yesu akajibu, “Jambo hili halikutukia kwa sababu ya dhambi zake yeye, wala dhambi za wazazi wake; ila alizaliwa kipofu ili nguvu ya Mungu ionekane ikifanya kazi ndani yake.
tataH sa pratyuditavAn etasya vAsya pitroH pApAd etAdR^ishobhUda iti nahi kintvanena yatheshvarasya karmma prakAshyate taddhetoreva|
4 Kukiwa bado mchana yatupasa kuendelea kufanya kazi za yule aliyenituma; maana usiku unakuja ambapo mtu hawezi kufanya kazi.
dine tiShThati matprerayituH karmma mayA karttavyaM yadA kimapi karmma na kriyate tAdR^ishI nishAgachChati|
5 Wakati ningali ulimwenguni, mimi ni mwanga wa ulimwengu.”
ahaM yAvatkAlaM jagati tiShThAmi tAvatkAlaM jagato jyotiHsvarUposmi|
6 Baada ya kusema hayo, akatema mate chini, akafanyiza tope, akampaka yule kipofu machoni,
ityukttA bhUmau niShThIvaM nikShipya tena pa NkaM kR^itavAn
7 akamwambia, “Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu.” (maana ya jina hili ni “aliyetumwa”). Basi, huyo kipofu akaenda, akanawa, kisha akarudi akiwa anaona.
pashchAt tatpa Nkena tasyAndhasya netre pralipya tamityAdishat gatvA shilohe. arthAt preritanAmni sarasi snAhi| tatondho gatvA tatrAsnAt tataH prannachakShu rbhUtvA vyAghuTyAgAt|
8 Basi, jirani zake na wale waliokuwa wanajua kwamba hapo awali alikuwa maskini mwombaji, wakasema, “Je, huyu siye yule maskini aliyekuwa akiketi na kuomba?”
apara ncha samIpavAsino lokA ye cha taM pUrvvamandham apashyan te bakttum Arabhanta yondhaloko vartmanyupavishyAbhikShata sa evAyaM janaH kiM na bhavati?
9 Baadhi yao wakasema, “Ndiye.” Wengine wakasema, “La! Ila anafanana naye.” Lakini huyo aliyekuwa kipofu akasema, “Ni mimi!”
kechidavadan sa eva kechidavochan tAdR^isho bhavati kintu sa svayamabravIt sa evAhaM bhavAmi|
10 Basi, wakamwuliza, “Sasa, macho yako yalipataje kufumbuliwa?”
ataeva te. apR^ichChan tvaM kathaM dR^iShTiM pAptavAn?
11 Naye akawajibu, “Yule mtu aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka machoni na kuniambia: Nenda ukanawe katika bwawa la Siloamu. Basi, mimi nikaenda, nikanawa, nikapata kuona.”
tataH sovadad yIshanAmaka eko jano mama nayane pa Nkena pralipya ityAj nApayat shilohakAsAraM gatvA tatra snAhi| tatastatra gatvA mayi snAte dR^iShTimahaM labdhavAn|
12 Wakamwuliza, “Yeye yuko wapi?” Naye akawajibu, “Mimi sijui!”
tadA te. avadan sa pumAn kutra? tenokttaM nAhaM jAnAmi|
13 Kisha wakampeleka huyo mtu aliyekuwa kipofu kwa Mafarisayo.
aparaM tasmin pUrvvAndhe jane phirUshinAM nikaTam AnIte sati phirUshinopi tamapR^ichChan kathaM dR^iShTiM prAptosi?
14 Siku hiyo Yesu alipofanya tope na kumfumbua macho mtu huyo, ilikuwa siku ya Sabato.
tataH sa kathitavAn sa pa Nkena mama netre. alimpat pashchAd snAtvA dR^iShTimalabhe|
15 Basi, Mafarisayo wakamwuliza mtu huyo, “Umepataje kuona?” Naye akawaambia, “Alinipaka tope machoni, nami nikanawa na sasa naona.”
kintu yIshu rvishrAmavAre karddamaM kR^itvA tasya nayane prasanne. akarod itikAraNAt katipayaphirUshino. avadan
16 Baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Mtu huyu hakutoka kwa Mungu, maana hashiki sheria ya Sabato.” Lakini wengine wakasema, “Mtu mwenye dhambi awezaje kufanya ishara za namna hii?” Kukawa na mafarakano kati yao.
sa pumAn IshvarAnna yataH sa vishrAmavAraM na manyate| tatonye kechit pratyavadan pApI pumAn kim etAdR^isham AshcharyyaM karmma karttuM shaknoti?
17 Wakamwuliza tena huyo mtu aliyekuwa kipofu, “Maadam yeye amekufungua macho, wasemaje juu yake?” Naye akawaambia, “Yeye ni nabii!”
itthaM teShAM parasparaM bhinnavAkyatvam abhavat| pashchAt te punarapi taM pUrvvAndhaM mAnuSham aprAkShuH yo janastava chakShuShI prasanne kR^itavAn tasmin tvaM kiM vadasi? sa ukttavAn sa bhavishadvAdI|
18 Viongozi wa Wayahudi hawakusadiki kwamba mtu huyo alikuwa kipofu hapo awali na sasa anaona mpaka walipowaita wazazi wake.
sa dR^iShTim AptavAn iti yihUdIyAstasya dR^iShTiM prAptasya janasya pitro rmukhAd ashrutvA na pratyayan|
19 Basi, wakawauliza hao wazazi, “Je, huyu ndiye mtoto wenu ambaye ninyi mwasema alizaliwa kipofu? Sasa amepataje kuona?”
ataeva te tAvapR^ichChan yuvayo ryaM putraM janmAndhaM vadathaH sa kimayaM? tarhIdAnIM kathaM draShTuM shaknoti?
20 Wazazi wake wakajibu, “Tunajua kwamba huyu ni mtoto wetu, na kwamba alizaliwa kipofu.
tatastasya pitarau pratyavochatAm ayam AvayoH putra A janerandhashcha tadapyAvAM jAnIvaH
21 Lakini amepataje kuona, hatujui; na wala hatumjui yule aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima, anaweza kujitetea mwenyewe.”
kintvadhunA kathaM dR^iShTiM prAptavAn tadAvAM n jAnIvaH kosya chakShuShI prasanne kR^itavAn tadapi na jAnIva eSha vayaHprApta enaM pR^ichChata svakathAM svayaM vakShyati|
22 Wazazi wake walisema hivyo kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi kwani viongozi hao walikuwa wamepatana ya kwamba mtu yeyote atakayekiri kwamba Yesu ni Kristo atafukuzwa nje ya sunagogi.
yihUdIyAnAM bhayAt tasya pitarau vAkyamidam avadatAM yataH kopi manuShyo yadi yIshum abhiShiktaM vadati tarhi sa bhajanagR^ihAd dUrIkAriShyate yihUdIyA iti mantraNAm akurvvan
23 Ndiyo maana wazazi wake walisema: “Yeye ni mtu mzima, mwulizeni.”
atastasya pitarau vyAharatAm eSha vayaHprApta enaM pR^ichChata|
24 Basi, wakamwita tena aliyekuwa kipofu, wakamwambia, “Sema ukweli mbele ya Mungu! Sisi tunajua kwamba mtu huyu ni mwenye dhambi.”
tadA te punashcha taM pUrvvAndham AhUya vyAharan Ishvarasya guNAn vada eSha manuShyaH pApIti vayaM jAnImaH|
25 Yeye akajibu, “Kama ni mwenye dhambi mimi sijui. Lakini kitu kimoja najua: Nilikuwa kipofu, na sasa naona.”
tadA sa ukttavAn sa pApI na veti nAhaM jAne pUrvAmandha Asamaham adhunA pashyAmIti mAtraM jAnAmi|
26 Basi, wakamwuliza, “Alikufanyia nini? Alikufumbuaje macho yako?”
te punarapR^ichChan sa tvAM prati kimakarot? kathaM netre prasanne. akarot?
27 Huyo mtu akawajibu, “Nimekwisha waambieni, nanyi hamkusikiliza; kwa nini mwataka kusikia tena? Je, ninyi pia mnataka kuwa wafuasi wake?”
tataH sovAdId ekakR^itvokathayaM yUyaM na shR^iNutha tarhi kutaH punaH shrotum ichChatha? yUyamapi kiM tasya shiShyA bhavitum ichChatha?
28 Lakini wao wakamtukana wakisema, “Wewe ni mfuasi wake; sisi ni wafuasi wa Mose.
tadA te taM tiraskR^itya vyAharan tvaM tasya shiShyo vayaM mUsAH shiShyAH|
29 Sisi tunajua kwamba Mungu alisema na Mose, lakini mtu huyu hatujui ametoka wapi!”
mUsAvaktreNeshvaro jagAda tajjAnImaH kintveSha kutratyaloka iti na jAnImaH|
30 Naye akawajibu, “Hili ni jambo la kushangaza! Ninyi hamjui ametoka wapi, lakini amenifumbua macho yangu!
sovadad eSha mama lochane prasanne. akarot tathApi kutratyaloka iti yUyaM na jAnItha etad AshcharyyaM bhavati|
31 Tunajua kwamba Mungu hawasikilizi watu wenye dhambi, ila humsikiliza yeyote mwenye kumcha na kutimiza mapenzi yake.
IshvaraH pApinAM kathAM na shR^iNoti kintu yo janastasmin bhaktiM kR^itvA tadiShTakriyAM karoti tasyaiva kathAM shR^iNoti etad vayaM jAnImaH|
32 Tangu mwanzo wa ulimwengu haijasikika kwamba mtu ameyafumbua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu. (aiōn g165)
kopi manuShyo janmAndhAya chakShuShI adadAt jagadArambhAd etAdR^ishIM kathAM kopi kadApi nAshR^iNot| (aiōn g165)
33 Kama mtu huyu hakutoka kwa Mungu, hangeweza kufanya chochote!”
asmAd eSha manuShyo yadIshvarAnnAjAyata tarhi ki nchidapIdR^ishaM karmma karttuM nAshaknot|
34 Wao wakamjibu, “Wewe ulizaliwa na kulelewa katika dhambi; unawezaje kutufundisha sisi?” Basi, wakamfukuzia mbali.
te vyAharan tvaM pApAd ajAyathAH kimasmAn tvaM shikShayasi? pashchAtte taM bahirakurvvan|
35 Yesu alisikia kwamba walikuwa wamemfukuzia mbali, naye alipomkuta akamwuliza, “Je, wewe unamwamini Mwana wa Mtu?”
tadanantaraM yihUdIyaiH sa bahirakriyata yIshuriti vArttAM shrutvA taM sAkShAt prApya pR^iShTavAn Ishvarasya putre tvaM vishvasiShi?
36 Huyo mtu akajibu, “Mheshimiwa, niambie yeye ni nani, ili nipate kumwamini.”
tadA sa pratyavochat he prabho sa ko yat tasminnahaM vishvasimi?
37 Yesu akamwambia, “Umekwisha mwona, naye ndiye anayesema nawe sasa.”
tato yIshuH kathitavAn tvaM taM dR^iShTavAn tvayA sAkaM yaH kathaM kathayati saeva saH|
38 Basi, huyo mtu akasema, “Ninaamini Bwana!” Akamsujudia.
tadA he prabho vishvasimItyuktvA sa taM praNAmat|
39 Yesu akasema, “Mimi nimekuja ulimwenguni kutoa hukumu, kusudi wasioona wapate kuona, na wale wanaoona wawe vipofu.”
pashchAd yIshuH kathitavAn nayanahInA nayanAni prApnuvanti nayanavantashchAndhA bhavantItyabhiprAyeNa jagadAham AgachCham|
40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa pamoja naye walisikia maneno hayo, wakamwuliza, “Je, sisi pia ni vipofu?”
etat shrutvA nikaTasthAH katipayAH phirUshino vyAharan vayamapi kimandhAH?
41 Yesu akawajibu, “Kama mngekuwa vipofu, hamngekuwa na hatia; lakini sasa ninyi mwasema: Sisi tunaona, na hiyo yaonyesha kwamba mna hatia bado.
tadA yIshuravAdId yadyandhA abhavata tarhi pApAni nAtiShThan kintu pashyAmIti vAkyavadanAd yuShmAkaM pApAni tiShThanti|

< Yohana 9 >