< Yohana 8 >
1 lakini Yesu akaenda kwenye mlima wa Mizeituni.
And at dawn he came again to the temple,
2 Kesho yake asubuhi na mapema alikwenda tena Hekaluni. Watu wote wakamwendea, naye akaketi akawa anawafundisha.
and all the people were coming unto him, and having sat down, he was teaching them;
3 Basi, walimu wa Sheria na Mafarisayo wakamletea mwanamke mmoja aliyefumaniwa katika uzinzi. Wakamsimamisha katikati yao.
and the scribes and the Pharisees bring unto him a woman having been taken in adultery, and having set her in the midst,
4 Kisha wakamwuliza Yesu, “Mwalimu! Mwanamke huyu alifumaniwa katika uzinzi.
they say to him, 'Teacher, this woman was taken in the very crime — committing adultery,
5 Katika Sheria yetu Mose alituamuru mwanamke kama huyu apigwe mawe. Basi, wewe wasemaje?”
and in the law, Moses did command us that such be stoned; thou, therefore, what dost thou say?'
6 Walisema hivyo kumjaribu, wapate kisa cha kumshtaki. Lakini Yesu akainama chini, akaandika ardhini kwa kidole.
and this they said, trying him, that they might have to accuse him. And Jesus, having stooped down, with the finger he was writing on the ground,
7 Walipozidi kumwuliza, Yesu akainuka, akawaambia, “Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe.”
and when they continued asking him, having bent himself back, he said unto them, 'The sinless of you — let him first cast the stone at her;'
8 Kisha akainama tena, akawa anaandika ardhini.
and again having stooped down, he was writing on the ground,
9 Waliposikia hivyo, wakaanza kutoweka mmojammoja, wakitanguliwa na wazee. Yesu akabaki peke yake, na yule mwanamke amesimama palepale.
and they having heard, and by the conscience being convicted, were going forth one by one, having begun from the elders — unto the last; and Jesus was left alone, and the woman standing in the midst.
10 Yesu alipoinuka akamwuliza huyo mwanamke, “Wako wapi wale watu? Je, hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?”
And Jesus having bent himself back, and having seen no one but the woman, said to her, 'Woman, where are those — thine accusers? did no one pass sentence upon thee?'
11 Huyo mwanamke akamjibu, “Mheshimiwa, hakuna hata mmoja!” Naye Yesu akamwambia, “Wala mimi sikuhukumu. Nenda zako; na tangu sasa usitende dhambi tena.”
and she said, 'No one, Sir;' and Jesus said to her, 'Neither do I pass sentence on thee; be going on, and no more sin.'
12 Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, “Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu. Anayenifuata mimi hatembei kamwe gizani, bali atakuwa na mwanga wa uzima.”
Again, therefore, Jesus spake to them, saying, 'I am the light of the world; he who is following me shall not walk in the darkness, but he shall have the light of the life.'
13 Basi, Mafarisayo wakamwambia, “Wewe unajishuhudia mwenyewe; kwa hiyo ushahidi wako si halali.”
The Pharisees, therefore, said to him, 'Thou of thyself dost testify, thy testimony is not true;'
14 Yesu akawajibu, “Hata kama ninajishuhudia mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli kwa sababu mimi najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
Jesus answered and said to them, 'And if I testify of myself — my testimony is true, because I have known whence I came, and whither I go, and ye — ye have not known whence I come, or whither I go.
15 Ninyi mnahukumu kwa fikira za kibinadamu, lakini mimi simhukumu mtu.
'Ye according to the flesh do judge; I do not judge any one,
16 Hata nikihukumu, hukumu yangu ni ya haki kwa sababu mimi siko peke yangu; Baba aliyenituma yuko pamoja nami.
and even if I do judge my judgment is true, because I am not alone, but I and the Father who sent me;
17 Imeandikwa katika Sheria yenu ya kwamba ushahidi wa watu wawili ni halali.
and also in your law it hath been written, that the testimony of two men are true;
18 Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma, ananishuhudia pia.”
I am [one] who is testifying of myself, and the Father who sent me doth testify of me.'
19 Hapo wakamwuliza, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu “Ninyi hamnijui mimi wala hamumjui Baba. Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”
They said, therefore, to him, 'Where is thy father?' Jesus answered, 'Ye have neither known me nor my Father: if me ye had known, my Father also ye had known.'
20 Yesu alisema maneno hayo kwenye chumba cha hazina alipokuwa anafundisha Hekaluni. Wala hakuna mtu aliyemtia nguvuni, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
These sayings spake Jesus in the treasury, teaching in the temple, and no one seized him, because his hour had not yet come;
21 Yesu akawaambia tena, “Naenda zangu nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi, ninyi hamwezi kufika.”
therefore said Jesus again to them, 'I go away, and ye will seek me, and in your sin ye shall die; whither I go away, ye are not able to come.'
22 Basi, viongozi wa Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Mbona anasema: Niendako ninyi hamwezi kufika?”
The Jews, therefore, said, 'Will he kill himself, because he saith, Whither I go away, ye are not able to come?'
23 Yesu akawaambia, “Ninyi mmetoka papa hapa chini, mimi nimetoka juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
and he said to them, 'Ye are from beneath, I am from above; ye are of this world, I am not of this world;
24 Ndiyo maana niliwaambieni mtakufa katika dhambi zenu. Kama msipoamini kwamba Mimi ndimi, mtakufa katika dhambi zenu.”
I said, therefore, to you, that ye shall die in your sins, for if ye may not believe that I am [he], ye shall die in your sins.'
25 Nao wakamwuliza, “Wewe ni nani?” Yesu akawajibu, “Nimewaambieni tangu mwanzo!
They said, therefore, to him, 'Thou — who art thou?' and Jesus said to them, 'Even what I did speak of to you at the beginning;
26 Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu. Lakini yule aliyenituma ni kweli; nami nauambia ulimwengu mambo yale tu niliyoyasikia kutoka kwake.”
many things I have to speak concerning you and to judge, but He who sent me is true, and I — what things I heard from Him — these I say to the world.'
27 Hawakuelewa kwamba Yesu alikuwa akisema nao juu ya Baba.
They knew not that of the Father he spake to them;
28 Basi, Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha mwinua Mwana wa Mtu hapo ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi, na kwamba sifanyi chochote mimi mwenyewe, ila nasema tu yale Baba aliyonifundisha.
Jesus, therefore, said to them, 'When ye may lift up the Son of Man then ye will know that I am [he]; and of myself I do nothing, but according as my Father did teach me, these things I speak;
29 Yule aliyenituma yuko pamoja nami; yeye hakuniacha peke yangu kwani nafanya daima yale yanayompendeza.”
and He who sent me is with me; the Father did not leave me alone, because I, the things pleasing to Him, do always.'
30 Baada ya kusema hayo watu wengi walimwamini.
As he is speaking these things, many believed in him;
31 Basi, Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkiyazingatia mafundisho yangu mtakuwa kweli wanafunzi wangu.
Jesus, therefore, said unto the Jews who believed in him, 'If ye may remain in my word, truly my disciples ye are, and ye shall know the truth,
32 Mtaujua ukweli, nao ukweli utawapeni uhuru.”
and the truth shall make you free.'
33 Nao wakamjibu, “Sisi ni wazawa wa Abrahamu, na hatujapata kamwe kuwa watumwa wa mtu yeyote yule. Una maana gani unaposema: mtakuwa huru?”
They answered him, 'Seed of Abraham we are; and to no one have we been servants at any time; how dost thou say — Ye shall become free?'
34 Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, kila mtu anayetenda dhambi ni mtumwa wa dhambi.
Jesus answered them, 'Verily, verily, I say to you — Every one who is committing sin, is a servant of the sin,
35 Mtumwa hana makao ya kudumu nyumbani, lakini mwana anayo makao ya kudumu. (aiōn )
and the servant doth not remain in the house — to the age, the son doth remain — to the age; (aiōn )
36 Kama mwana akiwapeni uhuru mtakuwa huru kweli.
if then the son may make you free, in reality ye shall be free.
37 Najua kwamba ninyi ni wazawa wa Abrahamu. Hata hivyo, mnataka kuniua kwa sababu hamuyakubali mafundisho yangu.
'I have known that ye are seed of Abraham, but ye seek to kill me, because my word hath no place in you;
38 Mimi nasema yale aliyonionyesha Baba, lakini ninyi mwafanya yale aliyowaambieni baba yenu.”
I — that which I have seen with my Father do speak, and ye, therefore, that which ye have seen with your father — ye do.'
39 Wao wakamjibu, “Baba yetu ni Abrahamu!” Yesu akawaambia, “Kama ninyi mngekuwa watoto wa Abrahamu, mngefanya kama alivyofanya Abrahamu,
They answered and said to him, 'Our father is Abraham;' Jesus saith to them, 'If children of Abraham ye were, the works of Abraham ye were doing;
40 Mimi nimewaambieni ukweli niliousikia kwa Mungu; hata hivyo, ninyi mwataka kuniua. Abrahamu hakufanya hivyo!
and now, ye seek to kill me — a man who hath spoken to you the truth I heard from God; this Abraham did not;
41 Ninyi mnafanya mambo yaleyale aliyofanya babu yenu.” Wao wakamwambia, “Sisi si watoto haramu! Tunaye baba mmoja tu, yaani Mungu.”
ye do the works of your father.' They said, therefore, to him, 'We of whoredom have not been born; one Father we have — God;'
42 Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda mimi, maana mimi nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
Jesus then said to them, 'If God were your father, ye were loving me, for I came forth from God, and am come; for neither have I come of myself, but He sent me;
43 Kwa nini hamwelewi hayo ninayosema? Ni kwa kuwa hamwezi kuusikiliza ujumbe wangu.
wherefore do ye not know my speech? because ye are not able to hear my word.
44 Ninyi ni watoto wa baba yenu Ibilisi na mnataka tu kutekeleza tamaa za baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo; hana msimamo katika ukweli, kwani ukweli haumo ndani yake. Kila asemapo uongo, husema kutokana na hali yake ya maumbile, maana yeye ni mwongo na baba wa uongo.
'Ye are of a father — the devil, and the desires of your father ye will to do; he was a man-slayer from the beginning, and in the truth he hath not stood, because there is no truth in him; when one may speak the falsehood, of his own he speaketh, because he is a liar — also his father.
45 Mimi nasema ukweli, na ndiyo maana ninyi hamniamini.
'And because I say the truth, ye do not believe me.
46 Nani kati yenu awezaye kuthibitisha kuwa mimi nina dhambi? Ikiwa basi nasema ukweli, kwa nini hamniamini?
Who of you doth convict me of sin? and if I speak truth, wherefore do ye not believe me?
47 Aliye wa Mungu husikiliza maneno ya Mungu. Lakini ninyi hamsikilizi kwa sababu ninyi si (watu wa) Mungu.”
he who is of God, the sayings of God he doth hear; because of this ye do not hear, because of God ye are not.'
48 Wayahudi wakamwambia, “Je, hatukusema kweli kwamba wewe ni Msamaria, na tena una pepo?”
The Jews, therefore, answered and said to him, 'Do we not say well, that thou art a Samaritan, and hast a demon?'
49 Yesu akajibu, “Mimi sina pepo; mimi namheshimu Baba yangu, lakini ninyi hamniheshimu.
Jesus answered, 'I have not a demon, but I honour my Father, and ye dishonour me;
50 Mimi sijitafutii utukufu wangu mwenyewe; yuko mmoja mwenye kuutafuta utukufu huo, naye ni hakimu.
and I do not seek my own glory; there is who is seeking and is judging;
51 Kweli nawaambieni, anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele.” (aiōn )
verily, verily, I say to you, If any one may keep my word, death he may not see — to the age.' (aiōn )
52 Basi, Wayahudi wakasema, “Sasa tunajua kweli kwamba wewe ni mwendawazimu! Abrahamu alikufa, na manabii pia walikufa, nawe wasema ati, Anayeuzingatia ujumbe wangu hatakufa milele! (aiōn )
The Jews, therefore, said to him, 'Now we have known that thou hast a demon; Abraham did die, and the prophets, and thou dost say, If any one may keep my word, he shall not taste of death — to the age! (aiōn )
53 Je, unajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa? Hata na manabii walikufa. Wewe unajifanya kuwa nani?”
Art thou greater than our father Abraham, who died? and the prophets died; whom dost thou make thyself?'
54 Yesu akawajibu, “Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu. Baba yangu ambaye ninyi mwasema ni Baba yenu, ndiye anayenitukuza.
Jesus answered, 'If I glorify myself, my glory is nothing; it is my Father who is glorifying me, of whom ye say that He is your God;
55 Ninyi hamjapata kumjua, lakini mimi namjua. Na, nikisema simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi. Mimi namjua na ninashika neno lake.
and ye have not known Him, and I have known Him, and if I say that I have not known Him, I shall be like you — speaking falsely; but I have known Him, and His word I keep;
56 Abrahamu, baba yenu, alishangilia aione siku yangu; naye aliiona, akafurahi.”
Abraham, your father, was glad that he might see my day; and he saw, and did rejoice.'
57 Basi, Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza miaka hamsini bado, nawe umemwona Abrahamu?”
The Jews, therefore, said unto him, 'Thou art not yet fifty years old, and Abraham hast thou seen?'
58 Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, kabla Abrahamu hajazaliwa, mimi niko.”
Jesus said to them, 'Verily, verily, I say to you, Before Abraham's coming — I am;'
59 Hapo wakaokota mawe ili wamtupie, lakini Yesu akajificha, akatoka Hekaluni.
they took up, therefore, stones that they may cast at him, but Jesus hid himself, and went forth out of the temple, going through the midst of them, and so passed by.