< Yohana 7 >

1 Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
Pegamaliki genago, Yesu agendayi ku Galilaya kwenuko. Aganili lepi kugenda pamulima wa Yudea ndava Vachilongosi va Vayawudi vaganayi kumkoma.
2 Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
Lukumbi lwa mselebuko wa Vayawudi wewukemelewa vindanda wavi papipi.
3 Basi ndugu zake wakamwambia, “Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
Hinu, valongo vaki vakamjovela mwene, “Uwuka penapa na uhambayi ku Yudea muni vevakulanda vagawonayi mahengu gaku geukugahenga.
4 Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu.”
Kawaka mundu mweihenga mambu cha mfiyu kuni mwene igana kumanyikana kwa vandu. Ndava wikita mambu ago, hinu jilangilasa kwa vandu va mulima woha.”
5 (Hata ndugu zake hawakumwamini!)
Hati valongo vaki mewawa vamsadika lepi.
6 Basi, Yesu akawaambia, “Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
Yesu akavajovela, “Lukumbi lwangu lwabwina lwakona kuhika, nambu kwa nyenye lukumbi lwoha lwabwina.
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
Vandu va mulima nakuhotola kuvahakalila nyenye, nambu ukunihakalila nene ndava nene nijova kuvya matendu gaki gahakau.
8 Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika.”
Nyenye mhamba kumselebuko. Nambu nene nakuhamba kumselebuko wenuwo, muni lukumbi lwangu lwabwina lwakona kuhika.”
9 Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
Peamalili kujova genago, mwene akasigalila ku Galilaya.
10 Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
Valongo vaki pevahambili kumselebuko wa vindanda, Yesu namwene akahamba, nambu lepi hotohoto ndi chamfiyu.
11 Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: “Yuko wapi?”
Vachilongosi va Vayawudi vamlondayi Yesu kumselebuko wenuwo, vakakota “Avi koki?”
12 Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “La! Anawapotosha watu.”
Pamsambi wa vandu kwavi na vandu vamahele vevajovai chinunu. Vangi pagati yavi vakajova, “Mundu mbwina.” Vangi vakajova, “Mwe! Akuvayaganisa vandu.”
13 Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
Nambu avi lepi mundu mweahotwili kujova malovi ga Yesu hotohoto, ndava ya kuvayogopa Vachilongosi va Vayawudi.
14 Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
Peyahikili pagati ya mselebuko, Yesu akahamba mu Nyumba ya Chapanga na kutumbula kuwula.
15 Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema “Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?”
Hinu, Vachilongosi va Vayawudi vakakangasa na kujova, “Mundu uyu agamanyili wuli goha aga changali mwene kuwuliwa na mundu?”
16 Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
Penapo Yesu akavayangula, “Mawuliwu genikugawula aga ganamwene lepi, nambu gaki yula mweanitumili.
17 Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
Mundu mweigana kuhenga gala geigana Chapanga, yati imanya ngati mawuliwu gangu gahumili kwa Chapanga amala nijova namwene.
18 Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
Mweijova ga mwene ndu, mwenuyu ilonda ukulu waki mwene, nambu yula mweilonda ukulu wa mweamtumili, ndi chakaka na mugati yaki kawaka uhakau.
19 Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
Wu, Musa avapelili lepi Malagizu? Nambu kawaka hati mmonga mweiyidakila Malagizu. Ndava kyani mulonda kunikoma?”
20 Hapo watu wakamjibu, “Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?”
Bahapo msambi wa vandu ukayangula, “Una mizuka veve! Yani mweigana kukukoma?”
21 Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
Yesu akavayangula, “Nikitili ulangisu umonga na nyenye uvakangisi.
22 Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
Musa avapeli malagizu ga kudumula jandu ndi wahumili lepi kwa Musa muni wahumili kwa vagogo. Hinu nyenye mukumdumula mundu jandu hati Ligono la Kupumulila.
23 Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
Yakavya mundu idumuliwa jandu Ligono la Kupumulila, ndi muni malagizu ga Musa ukoto kudenywa, hinu ndava kyani mukuniyomela ndava ya kumlamisa mundu mu Ligono la Kupumulila?
24 Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”
Mkotoka kumuhamula mundu kwa kumlola chakuvala ndu, nambu muhamula cheyiganikiwa.”
25 Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
Vandu vangi va pa Yelusalemu vajovili, “Wu, mundu mwenuyu lepi yula vachilongosi vilonda kumkoma?
26 Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
Mlola, ilongela hotohoto kawaka mundu mweakumjovela hati lilovi! Wu yihotoleka vachilongosi vamanyili chakaka, mwenuyu ndi Kilisitu?
27 Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!”
Nambu Kilisitu peibwela avi lepi mundu yati imanya ihumila koki. Nambu tete tikumanyi kwe ahumili mundu uyu!”
28 Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, “Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
Hinu, Yesu peavili mukuwula Munyumba ya Chapanga akajova kwa lwami, “Mwe! Mnimanyili, hati kwe nihumili mukukumanya? Nene nibweli lepi kwa uhotola wangu. Muni mwene mweanitumili nene ndi wa chakaka, na nyenye nakummanya,
29 Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”
nambu nene nimmanyili ndava nihumili kwaki, mwene ndi mweanitumili.”
30 Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
Hinu, vandu vakalonda kumkamula, nambu kawaka mundu mweatalambwili chiwoko kumpamisa ndava lukumbi lwaki lwavi lwakona kuhika.
31 Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, “Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?”
Vandu vamahele mu msambi wula vamsadiki, vakajova, “Peibwela Kilisitu Msangula, yati ihenga milangisu ya kukangasa yamahele neju kuliku yeihenga mundu uyu?”
32 Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
Vafalisayu vevayuwini vandu vijova ga pahi ndava ya Yesu. Hinu, vene pamonga na Vamteta vakulu va Chapanga vavatumili valonda va nyumba ya Chapanga vamkamulayi.
33 Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
Yesu akajova, “Nakona nivii pamonga na nyenye palukumbi luhupi, kangi nihamba kwa mwene mweanitumili.
34 Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika.”
Yati mukunilonda nambu nakuniwona, na penivya nene, nyenye nakuhotola kuhika.”
35 Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
Vachilongosi va Vayawudi vakajovesana vene kwa vene, “Mundu mwenuyu yati ihamba koki kwe nakuhotola kumkamula? Yati ihamba kumiji ya Vagiliki, kwevahamalili vandu vitu na kuvawula Vagiliki?
36 Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?”
Mwenuyu ijova kyani peijova, yati mukunilonda nambu nakuniwona na pala penivya nene nyenye nakuhotola kuhika?”
37 Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, “Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
Ligono la kumalakisa mselebuko wenuwo ndi lavi ligono likulu, Yesu akayima na kujova kwa lwami mundu mweavi na njota ndi abwela kwanene anywayi.
38 Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!”
Ngati chegijova Mayandiku Gamsopi, mweakunisadika nene, mifuleni ya manji yeyileta wumi yati yihelela mumtima waki.
39 (Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
Ajovili genago kumvala Mpungu Msopi kuvya vevakumsadika vala yati vakumpokela. Lukumbi lwenulo Mpungu Msopi avi akona kuhika, ndava Yesu avi akona kupewa ukulu na Chapanga.
40 Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”
Vandu vangi mu msambi wula pevayuwini malovi ago, vakajova, “Chakaka mundu uyu ndi yula mlota wa Chapanga!”
41 Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
Vangi vakajova, “mwenuyu ndi Kilisitu.” Nambu vangi vakajova, “Wu, yihotoleka Kilisitu kuhuma ku Galilaya?
42 Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!”
Wu, Mayandiku Gamsopi gijova wuli? Gijova Kilisitu yati ihumila mu lukolo lwa Daudi na ivelekewa ku Betelehemu, pamuji wa Daudi.”
43 Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
Hinu, mu msambi wula mpechenganu wahumalili ndava ya Yesu.
44 Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
Vandu vangi vaganayi kumkamula nambu avi lepi mundu mweatalambwili chiwoko chaki kumpamisa.
45 Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?”
Kangi valonda vala vakavahambila Vakulu va kuteta va Chapanga na Vafalisayu. Ndi vene vakavakota valonda, “Ndava kyani, mwangamleta Yesu?”
46 Walinzi wakawajibu, “Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!”
Valonda vala vakayangula, “Avi lepi mundu mweamali kujova vindu vyeajovili mundu uyu!”
47 Mafarisayo wakawauliza, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
Vafalisayu vakavakota, “Wu, na nyenye mkongiwi mewa?
48 Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
Wu, mumuwene hati mmonga wa chilongosi wa vandu, amala mmonga wa Vafalisayu mweakumsadika?
49 Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!”
Lepi, nambu msambi wenuwo vangamanya Malagizu ga Bambu geampeli Musa, vapeliwi likoto na Chapanga!”
50 Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
Mmonga wavi avi Nikodemu mweamuhambili Yesu magono ga mumbele. Hinu mwene akavajovela.
51 “Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?”
“Malagizu gitu gijova tikumuhamula lepi mundu changali kumuyuwanila na kumanya ahengili kyani?”
52 Nao wakamjibu, “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!”
Vene vakamyangula, “Wu, na veve mewa uhumili ku Galilaya? Hinu ukagasoma bwina Mayandiku Gamsopi wamwene yati wilola kuvya ku Galilaya katu nakuhuma mlota wa Chapanga!”
53 Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;
Penapo kila mmonga awuyili kunyumba yaki.

< Yohana 7 >