< Yohana 7 >

1 Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
After these things, Jesus was walking in Galilee, for he would not walk in Judea, because the Jewish leaders sought to kill him.
2 Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
Now the Jewish festival, the Feast of Tabernacles, was near.
3 Basi ndugu zake wakamwambia, “Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
So his brothers said to him, "Depart from here, and go into Judea, that your disciples also may see your works that you are doing.
4 Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu.”
For no one does anything in secret when he himself seeks to be known openly. If you do these things, show yourself to the world."
5 (Hata ndugu zake hawakumwamini!)
For even his brothers did not believe in him.
6 Basi, Yesu akawaambia, “Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
Jesus therefore said to them, "My time has not yet come, but your time is always ready.
7 Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
The world cannot hate you, but it hates me, because I testify about it, that its works are evil.
8 Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika.”
You go up to the feast. I am not yet going up to this feast, because my time is not yet fulfilled."
9 Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
After he had said this, he stayed in Galilee.
10 Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
But when his brothers had gone up to the feast, then he also went up, not publicly, but as it were in secret.
11 Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: “Yuko wapi?”
The Jewish leaders therefore sought him at the feast, and said, "Where is he?"
12 Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “La! Anawapotosha watu.”
There was much murmuring among the crowds concerning him. Some said, "He is a good man." But others said, "Not so, but he leads the crowd astray."
13 Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
Yet no one spoke openly of him for fear of the Jewish leaders.
14 Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
But when it was now the midst of the feast, Jesus went up into the temple and taught.
15 Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema “Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?”
Then the Jewish leaders were astonished, saying, "How does this man know such writings, having never been educated?"
16 Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
Jesus therefore answered them, "My teaching is not mine, but his who sent me.
17 Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
If anyone desires to do his will, he will know about the teaching, whether it is from God, or if I am speaking from myself.
18 Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
He who speaks from himself seeks his own glory, but he who seeks the glory of him who sent him is true, and no unrighteousness is in him.
19 Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?”
Did not Moses give you the Law, and yet none of you keeps the Law? Why do you seek to kill me?"
20 Hapo watu wakamjibu, “Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?”
The crowd answered, "You have a demon. Who seeks to kill you?"
21 Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
Jesus answered them, "I did one work, and you are all amazed.
22 Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
Moses has given you circumcision (not that it is of Moses, but of the fathers), and on the Sabbath you circumcise a boy.
23 Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
If a boy receives circumcision on the Sabbath, that the Law of Moses may not be broken, are you angry with me, because I made a man completely healthy on the Sabbath?
24 Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”
Do not judge according to appearance, but judge righteous judgment."
25 Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
Therefore some of them of Jerusalem said, "Is not this he whom they seek to kill?
26 Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
Look, he speaks openly, and they say nothing to him. Can it be that the rulers indeed know that this is the Christ?
27 Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!”
However we know where this man comes from, but when the Christ comes, no one will know where he comes from."
28 Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, “Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
Jesus therefore called out in the temple, teaching and saying, "You both know me, and know where I am from. I have not come of myself, but he who sent me is true, whom you do not know.
29 Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”
I know him, because I am from him, and he sent me."
30 Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
They sought therefore to take him; but no one laid a hand on him, because his hour had not yet come.
31 Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, “Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?”
But many in the crowd believed in him. They said, "When the Christ comes, he won't do more signs than those which this man has done, will he?"
32 Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
The Pharisees heard the crowd murmuring these things concerning him, and the chief priests and the Pharisees sent officers to arrest him.
33 Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
Then Jesus said, "I will be with you a little while longer, then I go to him who sent me.
34 Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika.”
You will seek me, but won't find; and where I am, you cannot come."
35 Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
The Jewish leaders therefore said among themselves, "Where will this man go that we won't find him? Will he go to the Diaspora among the Greeks, and teach the Greeks?
36 Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?”
What is this word that he said, 'You will seek me, but won't find; and where I am, you cannot come'?"
37 Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, “Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
Now on the last and greatest day of the feast, Jesus stood and said in a loud voice, "If anyone is thirsty, let him come to me and drink.
38 Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!”
He who believes in me, as the Scripture has said, from within him will flow rivers of living water."
39 (Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
But he said this about the Spirit, which those believing in him were to receive. For the Spirit was not yet given, because Jesus was not yet glorified.
40 Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!”
Some of the crowd therefore, when they heard these words, said, "This is truly the Prophet."
41 Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
Others said, "This is the Christ." But some said, "What, does the Christ come out of Galilee?
42 Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!”
Hasn't the Scripture said that the Christ comes of the offspring of David, and from Bethlehem, the village where David was?"
43 Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
So there arose a division in the crowd because of him.
44 Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
Some of them would have arrested him, but no one laid hands on him.
45 Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?”
The officers therefore came to the chief priests and Pharisees, and they said to them, "Why did you not bring him?"
46 Walinzi wakawajibu, “Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!”
The officers answered, "No man ever spoke like this man."
47 Mafarisayo wakawauliza, “Je, nanyi pia mmedanganyika?
The Pharisees therefore answered them, "You are not also led astray, are you?
48 Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
Have any of the rulers believed in him, or of the Pharisees?
49 Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!”
But this crowd that does not know the Law is accursed."
50 Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
Nicodemus (he who came to him before, being one of them) said to them,
51 “Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?”
"Does our Law judge a man, unless it first hears from him personally and knows what he does?"
52 Nao wakamjibu, “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!”
They answered him, "Are you also from Galilee? Search, and see that no prophet comes from Galilee."
53 Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;
Then everyone went to his own house,

< Yohana 7 >