< Yohana 6 >
1 Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
Après cela, Jésus passa au-delà de la mer de Galilée, ou de Tibériade.
2 Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
Et une grande foule le suivait, parce qu'ils voyaient les miracles qu'il opérait sur les malades.
3 Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
Et Jésus monta sur la montagne, et là il s'assit avec ses disciples.
4 Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
Or, la Pâque, la fête des Juifs, était proche.
5 Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, “Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?”
Jésus donc ayant levé les yeux, et voyant une grande foule qui venait à lui, dit à Philippe: Où achèterons-nous des pains, afin que ces gens-ci aient à manger?
6 (Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
Or, il disait cela pour l'éprouver, car il savait ce qu'il devait faire.
7 Filipo akamjibu, “Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!”
Philippe lui répondit: Deux cents deniers de pain ne leur suffiraient pas pour que chacun en prît un peu.
8 Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
L'un de ses disciples, André, frère de Simon Pierre, lui dit:
9 “Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?”
Il y a ici un jeune garçon qui a cinq pains d'orge et deux poissons; mais qu'est-ce que cela pour tant de gens?
10 Yesu akasema, “Waketisheni watu.” Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
Cependant Jésus dit: Faites asseoir ces gens. Or il y avait beaucoup d'herbe dans ce lieu. Les hommes donc s'assirent, au nombre d'environ cinq mille.
11 Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
Et Jésus prit les pains, et ayant rendu grâces, il les distribua aux disciples, et les disciples à ceux qui étaient assis; et de même pour les poissons, autant qu'ils en voulurent.
12 Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee.”
Après qu'ils furent rassasiés, il dit à ses disciples: Ramassez les morceaux qui sont restés, afin que rien ne se perde.
13 Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
Ils les ramassèrent donc, et ils remplirent douze paniers des morceaux des cinq pains d'orge, qui étaient restés de trop à ceux qui en avaient mangé.
14 Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, “Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni.”
Et ces gens, voyant le miracle que Jésus avait fait, disaient: Celui-ci est véritablement le prophète qui devait venir au monde.
15 Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
C'est pourquoi Jésus connaissant qu'ils allaient venir l'enlever, pour le faire roi, se retira encore seul sur la montagne.
16 Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
Quand le soir fut venu, ses disciples descendirent à la mer,
17 wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
Et étant entrés dans la barque, ils voulaient aller au-delà de la mer à Capernaüm; il faisait déjà obscur, et Jésus n'était pas encore venu vers eux.
18 Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
Comme il soufflait un grand vent, la mer élevait ses vagues.
19 Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
Or, quand ils eurent ramé environ vingt-cinq ou trente stades, ils virent Jésus qui marchait sur la mer, et s'approchait de la barque, et ils eurent peur.
20 Yesu akawaambia, “Ni mimi, msiogope!”
Mais il leur dit: C'est moi, n'ayez point de peur.
21 Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
Ils le reçurent donc avec plaisir dans la barque et aussitôt la barque aborda au lieu où ils allaient.
22 Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
Le lendemain, la foule qui était demeurée de l'autre côté de la mer, vit qu'il n'y avait point eu là d'autre barque que celle dans laquelle ses disciples étaient entrés, et que Jésus n'y était point entré avec eux, mais que ses disciples s'en étaient allés seuls;
23 Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
(Cependant d'autres barques étaient arrivées de Tibériade, près du lieu où ils avaient mangé le pain, après que le Seigneur eut rendu grâces);
24 Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
Quand donc la foule vit que Jésus n'était point là, ni ses disciples, ils entrèrent dans les barques, et allèrent à Capernaüm, chercher Jésus.
25 Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, “Mwalimu, ulifika lini hapa?”
Et l'ayant trouvé de l'autre côté de la mer, ils lui dirent: Maître, quand es-tu arrivé ici?
26 Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
Jésus leur répondit et leur dit: En vérité, en vérité je vous le dis, vous me cherchez, non parce que vous avez vu des miracles, mais parce que vous avez mangé des pains, et que vous avez été rassasiés.
27 Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho.” (aiōnios )
Travaillez, non point pour la nourriture qui périt, mais pour celle qui demeure jusqu'à la vie éternelle, et que le Fils de l'homme vous donnera; car le Père, Dieu, l'a marqué de son sceau. (aiōnios )
28 Wao wakamwuliza, “Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?”
Ils lui dirent donc: Que ferons-nous pour travailler aux ouvres de Dieu?
29 Yesu akawajibu, “Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma.”
Jésus leur répondit: C'est ici l'ouvre de Dieu, que vous croyiez en celui qu'il a envoyé.
30 Hapo wakamwambia, “Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
Alors ils lui dirent: Quel miracle fais-tu donc, que nous le voyions et que nous croyions en toi? Quelle œuvre fais-tu?
31 Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni.”
Nos pères ont mangé la manne dans le désert, selon qu'il est écrit: Il leur a donné à manger le pain du ciel.
32 Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
Et Jésus leur dit: En vérité, en vérité je vous le dis, Moïse ne vous a point donné le pain du ciel; mais mon Père vous donne le vrai pain du ciel.
33 Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima.”
Car le pain de Dieu est celui qui est descendu du ciel, et qui donne la vie au monde.
34 Basi, wakamwambia, “Mheshimiwa, tupe daima mkate huo.”
Ils lui dirent: Seigneur, donne-nous toujours de ce pain-là.
35 Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
Et Jésus leur répondit: Je suis le pain de vie; celui qui vient à moi n'aura jamais faim, et celui qui croit en moi n'aura jamais soif.
36 Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
Mais je vous l'ai dit, vous m'avez vu, et vous ne croyez point.
37 Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
Tout ce que le Père me donne viendra à moi, et je ne mettrai point dehors celui qui vient à moi.
38 kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
Car je suis descendu du ciel, pour faire, non ma volonté, mais la volonté de celui qui m'a envoyé.
39 Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
Or c'est ici la volonté du Père qui m'a envoyé, que je ne perde aucun de ceux qu'il m'a donnés, mais que je les ressuscite au dernier jour.
40 Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho.” (aiōnios )
C'est ici la volonté de celui qui m'a envoyé, que quiconque contemple le Fils et croit en lui, ait la vie éternelle; et je le ressusciterai au dernier jour. (aiōnios )
41 Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: “Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
Les Juifs murmuraient donc contre lui parce qu'il disait: Je suis le pain descendu du ciel.
42 Wakasema, “Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?”
Et ils disaient: N'est-ce pas là Jésus, le fils de Joseph, dont nous connaissons le père et la mère? Comment donc dit-il: Je suis descendu du ciel?
43 Yesu akawaambia, “Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
Jésus répondit et leur dit: Ne murmurez point entre vous.
44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
Personne ne peut venir à moi, si le Père qui m'a envoyé ne l'attire; et je le ressusciterai au dernier jour.
45 Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
Il est écrit dans les prophètes: Ils seront tous enseignés de Dieu. Quiconque a écouté le Père et a été instruit par lui, vient à moi.
46 Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
Ce n'est pas que personne ait vu le Père, si ce n'est celui qui vient de Dieu; celui-là a vu le Père.
47 Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios )
En vérité, en vérité je vous le dis: Celui qui croit en moi a la vie éternelle. (aiōnios )
48 Mimi ni mkate wa uzima.
Je suis le pain de vie.
49 Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
Vos pères ont mangé la manne dans le désert, et ils sont morts.
50 Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
C'est ici le pain qui est descendu du ciel, afin que celui qui en mange ne meure point.
51 Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn )
Je suis le pain vivant, qui est descendu du ciel; si quelqu'un mange de ce pain, il vivra éternellement; et le pain que je donnerai, c'est ma chair. Je la donnerai pour la vie du monde. (aiōn )
52 Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
Les Juifs disputaient donc entre eux, disant: Comment cet homme peut-il donner sa chair à manger?
53 Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
Jésus leur dit: En vérité, en vérité je vous le dis: Si vous ne mangez la chair du Fils de l'homme, et si vous ne buvez son sang, vous n'aurez point la vie en vous-mêmes.
54 Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios )
Celui qui mange ma chair et qui boit mon sang, a la vie éternelle; et je le ressusciterai au dernier jour. (aiōnios )
55 Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
Car ma chair est véritablement une nourriture, et mon sang est véritablement un breuvage.
56 Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
Celui qui mange ma chair et qui boit mon sang, demeure en moi, et moi en lui.
57 Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
Comme le Père, qui est vivant, m'a envoyé, et que je vis par le Père; ainsi celui qui me mange vivra par moi.
58 Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn )
C'est ici le pain qui est descendu du ciel. Ce n'est pas comme vos pères qui ont mangé la manne, et ils sont morts; celui qui mangera ce pain vivra éternellement. (aiōn )
59 Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
Jésus dit ces choses, enseignant dans la synagogue à Capernaüm.
60 Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, “Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?”
Plusieurs de ses disciples l'ayant entendu, dirent: Cette parole est dure, qui peut l'écouter?
61 Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, “Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
Mais Jésus, sachant en lui-même que ses disciples murmuraient de cela, leur dit: Ceci vous scandalise-t-il?
62 Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
Que sera-ce donc si vous voyez le Fils de l'homme monter où il était auparavant?
63 Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
C'est l'esprit qui vivifie; la chair ne sert de rien. Les paroles que je vous dis sont esprit et vie.
64 Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini.” (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
Mais il y en a parmi vous qui ne croient point. Car Jésus savait dès le commencement qui étaient ceux qui ne croyaient pas, et qui était celui qui le trahirait.
65 Kisha akasema, “Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu.”
Et il disait: C'est à cause de cela que je vous ai dit, que personne ne peut venir à moi, si cela ne lui a été donné par mon Père.
66 Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
Dès lors plusieurs de ses disciples se retirèrent, et n'allaient plus avec lui.
67 Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, “Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?”
Jésus dit donc aux douze: Et vous, ne voulez-vous point aussi vous en aller?
68 Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele. (aiōnios )
Simon Pierre lui répondit: Seigneur, à qui irions-nous? Tu as les paroles de la vie éternelle; (aiōnios )
69 Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu.”
Et nous avons cru, et nous avons connu que tu es le Christ, le Fils du Dieu vivant.
70 Yesu akawaambia, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!”
Jésus leur répondit: Ne vous ai-je pas choisis, vous douze? et l'un de vous est un démon.
71 Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.
Or, il parlait de Judas l'Iscariote, fils de Simon; car celui-ci devait le trahir, lui, l'un des douze.