< Yohana 6 >
1 Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
After these things, Jesus went away to the other side of the Sea of Galilee, also called the Sea of Tiberias.
2 Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
A great crowd was following him because they saw the signs that he was doing on those who were sick.
3 Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
Jesus went up the mountain and there he sat down with his disciples.
4 Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
(Now the Passover, the Jewish festival, was near.)
5 Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, “Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?”
When Jesus looked up and saw a great crowd coming to him, he said to Philip, “Where are we going to buy bread so that these may eat?”
6 (Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
(But Jesus said this to test Philip, for he himself knew what he was going to do.)
7 Filipo akamjibu, “Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!”
Philip answered him, “Two hundred denarii worth of bread would not be sufficient for each one to have even a little.”
8 Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
One of the disciples, Andrew, the brother of Simon Peter, said to Jesus,
9 “Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?”
“There is a boy here who has five bread loaves of barley and two fish, but what are these among so many?”
10 Yesu akasema, “Waketisheni watu.” Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
Jesus said, “Make the people sit down.” (Now there was a lot of grass in the place.) So the men sat down, about five thousand in number.
11 Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
Then Jesus took the loaves and after giving thanks, he gave it to those who were sitting. He did the same with the fish, as much as they wanted.
12 Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee.”
When the people were filled, he said to his disciples, “Gather up the broken pieces which remain, so that nothing will be lost.”
13 Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
So they gathered them up and filled twelve baskets with broken pieces from the five barley loaves left over by those who had eaten.
14 Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, “Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni.”
Then, when the people saw this sign that he did, they said, “This truly is the prophet who is to come into the world.”
15 Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
When Jesus realized that they were about to come and seize him by force to make him king, he withdrew again up the mountain by himself.
16 Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
When it became evening, his disciples went down to the sea.
17 wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
They got into a boat, and were going over the sea to Capernaum. It was dark by this time, and Jesus had not yet come to them.
18 Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
A strong wind was blowing, and the sea was getting rough.
19 Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
When they had rowed about twenty-five or thirty stadia, they saw Jesus walking on the sea and coming near the boat, and they were afraid.
20 Yesu akawaambia, “Ni mimi, msiogope!”
But he said to them, “It is I! Do not be afraid.”
21 Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
Then they were willing to receive him into the boat, and immediately the boat reached the land where they were going.
22 Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
The next day, the crowd that had been standing on the other side of the sea saw that there was no other boat there except the one, and that Jesus had not entered it with his disciples but that his disciples had gone away alone.
23 Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
However, there were some boats that came from Tiberias close to the place where they had eaten the bread loaves after the Lord had given thanks.
24 Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
When the crowd discovered that neither Jesus nor his disciples were there, they themselves got into the boats and went to Capernaum seeking Jesus.
25 Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, “Mwalimu, ulifika lini hapa?”
After they found him on the other side of the sea, they said to him, “Rabbi, when did you come here?”
26 Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
Jesus replied to them, saying, “Truly, truly, you seek me, not because you saw signs, but because you ate some of the bread loaves and were filled.
27 Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho.” (aiōnios )
Do not work for the food that perishes, but work for the food that endures to eternal life which the Son of Man will give you, for God the Father has set his seal on him.” (aiōnios )
28 Wao wakamwuliza, “Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?”
Then they said to him, “What must we do, so that we may do the works of God?”
29 Yesu akawajibu, “Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma.”
Jesus replied and said to them, “This is the work of God: That you believe in the one whom he has sent.”
30 Hapo wakamwambia, “Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
So they said to him, “What sign then will you do, so that we may see and believe you? What will you do?
31 Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni.”
Our fathers ate the manna in the wilderness, as it is written, 'He gave them bread from heaven to eat.'”
32 Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
Then Jesus replied to them, “Truly, truly, it was not Moses who gave you the bread out of heaven, but it is my Father who is giving you the true bread from heaven.
33 Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima.”
For the bread of God is that which comes down from heaven and gives life to the world.”
34 Basi, wakamwambia, “Mheshimiwa, tupe daima mkate huo.”
So they said to him, “Sir, give us this bread always.”
35 Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
Jesus said to them, “I am the bread of life; he who comes to me will not be hungry, and he who believes in me will never be thirsty.
36 Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
But I told you that indeed you have seen me, and you do not believe.
37 Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
Everyone whom the Father gives me will come to me, and he who comes to me I will certainly not throw out.
38 kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
For I have come down from heaven, not to do my own will, but the will of him who sent me.
39 Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
This is the will of him who sent me, that I would lose not one of all those whom he has given me, but will raise them up on the last day.
40 Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho.” (aiōnios )
For this is the will of my Father, that everyone who sees the Son and believes in him would have eternal life and I will raise him up on the last day.” (aiōnios )
41 Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: “Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
Then the Jews grumbled about him because he had said, “I am the bread that has come down from heaven.”
42 Wakasema, “Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?”
They said, “Is not this Jesus son of Joseph, whose father and mother we know? How then does he now say, 'I have come down from heaven'?”
43 Yesu akawaambia, “Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
Jesus replied and said to them, “Stop grumbling among yourselves.
44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
No one can come to me unless the Father who sent me draws him, and I will raise him up on the last day.
45 Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
It is written in the prophets, 'Everyone will be taught by God.' Everyone who has heard and learned from the Father comes to me.
46 Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
Not that anyone has seen the Father, except he who is from God—he has seen the Father.
47 Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios )
Truly, truly, he who believes has eternal life. (aiōnios )
48 Mimi ni mkate wa uzima.
I am the bread of life.
49 Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
Your fathers ate the manna in the wilderness, and they died.
50 Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
This is the bread which comes down from heaven, so that a person may eat some of it and not die.
51 Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn )
I am the living bread that came down from heaven. If anyone eats some of this bread, he will live forever. The bread that I will give is my flesh for the life of the world.” (aiōn )
52 Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
The Jews became angry among themselves and began to argue, saying, “How can this man give us his flesh to eat?”
53 Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
Then Jesus said to them, “Truly, truly, unless you eat the flesh of the Son of Man and drink his blood, you will not have life in yourselves.
54 Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios )
Whoever eats my flesh and drinks my blood has everlasting life, and I will raise him up at the last day. (aiōnios )
55 Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
For my flesh is true food, and my blood is true drink.
56 Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
He who eats my flesh and drinks my blood remains in me, and I in him.
57 Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
As the living Father sent me, and as I live because of the Father, so he who eats me, he will also live because of me.
58 Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn )
This is the bread that has come down from heaven, not as the fathers ate and died. He who eats this bread will live forever.” (aiōn )
59 Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
But Jesus said these things in the synagogue while he was teaching in Capernaum.
60 Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, “Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?”
Then many of his disciples who heard this said, “This is a difficult teaching; who can accept it?”
61 Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, “Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
Jesus, because he knew in himself that his disciples were grumbling at this, said to them, “Does this offend you?
62 Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
Then what if you should see the Son of Man going up to where he was before?
63 Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
It is the Spirit who makes alive; the flesh profits nothing. The words that I have spoken to you are spirit, and they are life.
64 Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini.” (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
Yet there are some of you who do not believe.” For Jesus knew from the beginning who were the ones that would not believe and who it was who would betray him.
65 Kisha akasema, “Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu.”
He said, “It is because of this that I said to you that no one can come to me unless it is granted to him by the Father.”
66 Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
Because of this, many of his disciples went away and no longer walked with him.
67 Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, “Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?”
Then Jesus said to the twelve, “You do not want to go away also, do you?”
68 Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele. (aiōnios )
Simon Peter answered him, “Lord, to whom shall we go? You have words of eternal life, (aiōnios )
69 Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu.”
and we have believed and come to know that you are the Holy One of God.”
70 Yesu akawaambia, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!”
Jesus said to them, “Did not I choose you, the twelve, and one of you is a devil?”
71 Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.
Now he spoke of Judas son of Simon Iscariot, for it was he, one of the twelve, who would betray Jesus.