< Yohana 4 >
1 Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
Accordingly when the Lord knew that the Pharisees had heard it said, "Jesus is making and baptizing more disciples than John,"
2 (Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
(though Jesus himself was not accustomed to baptize, but his disciples),
3 Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
he left Judea and returned to Galilee.
4 na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
Now he had to pass through Samaria;
5 Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
so he came to a city of Samaria called Sychar, near the piece of ground that Jacob gave to his son Joseph.
6 Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
Jacob’s Spring was there. So Jesus, tired out with his journey, was sitting thus by the spring.
7 Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.”
It was about noon, and a woman of Samaria came to draw water.
8 (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
Jesus said to her, "Give me a drink" (for his disciples were gone away into the city to buy food.)
9 Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
"How is it," answered the Samaritan woman, "that you who are a Jew ask a drink from me, a woman, and a Samaritan?" (For Jews have no dealings with Samaritans.)
10 Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai.”
"If you had known the free gift of God," Jesus answered, "and who it is that says to you, ‘Give me a drink,’ you would have asked of him, and he would have given you living water."
11 Huyo mama akasema, “Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
"Sir," said the woman, "you have nothing to draw with, and the well is deep; whence have you that living water?
12 Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki.”
Surely you are not greater than our Father Jacob, who gave us the well, and used to drink from it himself, and his sons, and his cattle, too?"
13 Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
"All who drink of this water," Jesus answered, "will thirst again;
14 Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele.” (aiōn , aiōnios )
but whoever once drinks of the water that I will give him, shall never thirst any more, but the water that I will give him shall become a living spring of water within him, welling up into eternal life." (aiōn , aiōnios )
15 Huyo mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji.”
"Sir!" exclaimed the woman, "give me this water, so that I may not be thirsty, nor come all this way to draw water."
16 Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa.”
Jesus said to her, "Go, call your husband, and then come here."
17 Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume.
"I have no husband," answered the woman. "You are right in saying ‘I have no husband,’"Jesus said to her,
18 Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”
"for you have had five husbands, and the man you now have is not your husband; in this you have spoken truly."
19 Huyo Mwanamke akamwambia, “Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
"I see, Sir, that you are a prophet," replied the woman.
20 Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu.”
"Our forefathers worshiped in this mountain, yet you Jews say that in Jerusalem is the place where one must worship."
21 Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
"Woman, believe me," said Jesus, "that the hour is coming when neither in this mountain nor in Jerusalem will you worship the Father.
22 Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
You are worshiping something you do not know. we know what we worship, for salvation comes from the Jews.
23 Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
But an hour is coming, and is now here, when the true worshipers will worship the Father in spirit and in truth. For the Father is seeking such as his worshipers.
24 Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake.”
God is spirit, and those who worship him must worship him in spirit and in truth."
25 Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.”
"I know," said the woman, "that Messiah is coming, who is called the Christ; when he has come he will tell us everything."
26 Yesu akamwambia, “Mimi ninayesema nawe, ndiye.”
Jesus said to her, "I who am now talking to you, am he."
27 Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
Just then his disciples came up, and were astonished that he was talking with a woman; yet not one of them asked him, "What do you want?" or "Why are you talking with her?"
28 Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
Then the woman left her water-jar, and went away into the city and began saying to the people.
29 “Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?”
"Come! see a man who has told me everything that I ever did. He can’t be the Christ, can he?"
30 Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
They left the city and set out to go to him.
31 Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, ule chakula.”
Meanwhile the disciples kept urging him.
32 Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.”
"Rabbi," they said, "eat something." But he answered, "I have food to eat of which you know nothing."
33 Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?”
So the disciples began to say to one another, "Can any one have brought him something to eat?"
34 Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
Jesus said to them. "My food is to do the will of Him who sent me, and to accomplish his work.
35 Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
Do you not say, ‘It wants yet four months, and then comes the harvest’? Look, I tell you! Lift up your eyes and behold the fields, that they are already white for harvest.
36 Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja. (aiōnios )
The reaper is already receiving wages and gathering a crop for eternal life, so that the sower and the reaper may rejoice together. (aiōnios )
37 Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
For in this respect the saying is true, ‘One sows, another reaps.’
38 Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao.”
I sent you to reap a crop on which you have not toiled. Others have toiled, and you have reaped the benefit of their toil."
39 Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.”
Many of the Samaritans of that city believed on him because of the word of the woman when she declared, "He told me everything that I ever did."
40 Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
So when the Samaritans arrived, they began asking him to remain with them; and he stayed there two days.
41 Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
Then many more believed because of what he said, himself; and they told the woman.
42 Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
"We no longer believe because of what you said. for we ourselves have heard him, and we know that this is certainly the Saviour of the world."
43 Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
After these two days Jesus went away from there into Galilee.
44 Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, “Nabii hapati heshima katika nchi yake.”
For Jesus himself testified that a prophet has no honor in his own country.
45 Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
When he reached Galilee, however, the Galileans welcomed him, for they had seen all that he did in Jerusalem at the feast; for they, too, had been at the feast.
46 Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
So he came back again to Cana of Galilee, where he made the water wine. Now there was one of the king’s officers whose son was lying ill at Capernaum.
47 Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
When he heard that Jesus had come from Judea into Galilee, he went to him, and begged him to come down and heal his son who was lying at the point of death.
48 Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!”
Then Jesus said to him, "Unless you all see signs and wonders, you will not believe."
49 Huyo ofisa akamwambia, “Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa.”
"Sir," said the king’s officer, "come down before my little boy dies."
50 Yesu akamwambia, “Nenda tu, mwanao yu mzima.” Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
Jesus answered. "Go your way. Your son lives." And the man believed the word which Jesus spoke to him, and started to go home.
51 Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
And when he was already on his way down, his slaves met him, saying that his boy was living.
52 Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, “Jana saa saba mchana, homa ilimwacha.”
So he asked them at what hour he had begun mend. They answered, "Yesterday, about one o’clock, the fever left him."
53 Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: “Mwanao yu mzima.” Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
Then the father realized that it had left him at the very hour when Jesus had said to him, "Your son lives," and he himself believed, and his whole household.
54 Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.
This is the second sign which Jesus performed, on returning from Judea to Galilee.