< Yohana 3 >

1 Kulikuwa na kiongozi mmoja Myahudi, wa kikundi cha Mafarisayo, jina lake Nikodemo.
Now there was a man of the Pharisees named Nicodemus, a ruler of the Jewish people.
2 Siku moja alimwendea Yesu usiku, akamwambia, “Rabi, tunajua kwamba wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, maana hakuna mtu awezaye kufanya ishara unazozifanya Mungu asipokuwa pamoja naye.”
This man came to him at night, and said to him, "Rabbi, we know that you are a teacher come from God, for no one can do these signs that you do, unless God is with him."
3 Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa upya hataweza kuuona ufalme wa Mungu.”
Jesus answered him, "Truly, truly, I tell you, unless one is born again he cannot see the Kingdom of God."
4 Nikodemo akamwuliza, “Mtu mzima awezaje kuzaliwa tena? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake na kuzaliwa mara ya pili!”
Nicodemus said to him, "How can anyone be born when he is old? Can he enter a second time into his mother's womb, and be born?"
5 Yesu akamjibu, “Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.
Jesus answered, "Truly, truly, I tell you, unless one is born of water and Spirit he cannot enter into the Kingdom of God.
6 Mtu huzaliwa kimwili kwa baba na mama, lakini huzaliwa kiroho kwa Roho.
That which is born of the flesh is flesh. That which is born of the Spirit is spirit.
7 Usistaajabu kwamba nimekwambia kuwa ni lazima kuzaliwa upya.
Do not be surprised that I said to you, 'You must be born again.'
8 Upepo huvuma kuelekea upendako; waisikia sauti yake, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda. Ndivyo ilivyo kwa mtu aliyezaliwa kwa Roho.”
The wind blows where it wants to, and you hear its sound, but do not know where it comes from and where it is going. So is everyone who is born of the Spirit."
9 Nikodemo akamwuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
Nicodemus answered and said to him, "How can these things be?"
10 Yesu akamjibu, “Je, wewe ni mwalimu katika Israel na huyajui mambo haya?
Jesus answered him, "Are you the teacher of Israel, and do not understand these things?
11 Kweli nakwambia, sisi twasema tunayoyajua na kushuhudia tuliyoyaona, lakini ninyi hamkubali ujumbe wetu.
Truly, truly, I tell you, we speak that which we know, and testify of that which we have seen, but you do not accept our testimony.
12 Ikiwa nimewaambieni mambo ya kidunia nanyi hamniamini, mtawezaje kuamini nikiwaambieni mambo ya mbinguni?
If I told you earthly things and you do not believe, how will you believe if I tell you heavenly things?
13 Hakuna mtu aliyepata kwenda juu mbinguni isipokuwa Mwana wa Mtu ambaye ameshuka kutoka mbinguni.
And no one has ascended into heaven, but he who descended out of heaven, the Son of Man, who is in heaven.
14 “Kama vile Mose alivyomwinua juu nyoka wa shaba kule jangwani, naye Mwana wa Mtu atainuliwa juu vivyo hivyo,
And as Moses lifted up the serpent in the wilderness, even so must the Son of Man be lifted up,
15 ili kila anayemwamini awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
so that everyone who believes in him may have life without end. (aiōnios g166)
16 Maana Mungu aliupenda ulimwengu hivi hata akamtoa Mwana wake wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
For this is how God loved the world: he gave his only Son, so that everyone who believes in him will not perish but have life without end. (aiōnios g166)
17 Maana Mungu hakumtuma Mwanae ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali aukomboe ulimwengu.
For God did not send his Son into the world to judge the world, but that the world should be saved through him.
18 “Anayemwamini Mwana hahukumiwi; asiyemwamini amekwisha hukumiwa kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.
The one who believes in him is not judged, but the one who does not believe has been judged already, because he has not believed in the name of the only Son of God.
19 Na hukumu yenyewe ndiyo hii: Mwanga umekuja ulimwenguni lakini watu wakapenda giza kuliko mwanga, kwani matendo yao ni maovu.
This is the judgment, that the light has come into the world, and people loved the darkness rather than the light, because their works were evil.
20 Kila mtu atendaye maovu anauchukia mwanga, wala haji kwenye mwanga, maana hapendi matendo yake maovu yamulikwe.
For everyone who does evil hates the light, and does not come to the light, so that his works will not be exposed.
21 Lakini mwenye kuuzingatia ukweli huja kwenye mwanga, ili matendo yake yaonekane yametendwa kwa kumtii Mungu.”
But the one who does the truth comes to the light, that his works may be revealed, that they have been done in God."
22 Baada ya hayo, Yesu alifika mkoani Yudea pamoja na wanafunzi wake. Alikaa huko pamoja nao kwa muda, akibatiza watu.
After these things, Jesus came with his disciples into the land of Judea. He stayed there with them, and was baptizing.
23 Yohane pia alikuwa akibatiza watu huko Ainoni, karibu na Salemu, maana huko kulikuwa na maji mengi. Watu walimwendea, naye akawabatiza.
Now John also was baptizing in Aenon near Salim, because there was much water there. They came, and were baptized.
24 (Wakati huo Yohane alikuwa bado hajafungwa gerezani.)
For John was not yet thrown into prison.
25 Ubishi ulitokea kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohane na Myahudi mmoja kuhusu desturi za kutawadha.
Now a dispute arose between John's disciples with a Jew about purification.
26 Basi, wanafunzi hao wakamwendea Yohane na kumwambia, “Mwalimu, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ng'ambo ya Yordani na ambaye wewe ulimshuhudia, sasa naye anabatiza, na watu wote wanamwendea.”
And they came to John, and said to him, "Rabbi, he who was with you beyond the Jordan, to whom you have testified, look, he is baptizing, and everyone is coming to him."
27 Yohane akawaambia, “Mtu hawezi kuwa na kitu asipopewa na Mungu.
John answered, "No one can receive anything, unless it has been given to him from heaven.
28 Nanyi wenyewe mwaweza kushuhudia kuwa nilisema: Mimi siye Kristo, lakini nimetumwa ili nimtangulie!
You yourselves bear me witness that I said, 'I am not the Christ,' but, 'I have been sent before him.'
29 Bibiarusi ni wake bwanaarusi, lakini rafiki yake bwana arusi, anayesimama na kusikiliza, hufurahi sana anapomsikia bwana arusi akisema. Ndivyo furaha yangu ilivyokamilishwa.
He who has the bride is the bridegroom; but the friend of the bridegroom, who stands and hears him, rejoices greatly because of the bridegroom's voice. So this joy of mine is now complete.
30 Ni lazima yeye azidi kuwa maarufu, na mimi nipungue.
He must increase, but I must decrease.
31 “Anayekuja kutoka juu ni mkuu kuliko wote; atokaye duniani ni wa dunia, na huongea mambo ya kidunia. Lakini anayekuja kutoka mbinguni ni mkuu kuliko wote.
He who comes from above is above all. He who is from the earth belongs to the earth, and speaks of the earth. He who comes from heaven is above all.
32 Yeye husema yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna mtu anayekubali ujumbe wake.
What he has seen and heard, of that he testifies; and no one receives his witness.
33 Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.
He who has received his witness has set his seal to this, that God is true.
34 Yule aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, maana Mungu humjalia mtu huyo Roho wake bila kipimo.
For he whom God has sent speaks the words of God; for he does not give the Spirit by measure.
35 Baba anampenda Mwana na amemkabidhi vitu vyote.
The Father loves the Son, and has given all things into his hand.
36 Anayemwamini Mwana anao uzima wa milele; asiyemtii Mwana hatakuwa na uzima wa milele, bali ghadhabu ya Mungu hubaki juu yake.” (aiōnios g166)
Whoever believes in the Son has everlasting life, but whoever refuses to believe in the Son won't see life, but the wrath of God remains on him." (aiōnios g166)

< Yohana 3 >