< Yohana 2 >

1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
Et die tertia nuptiae factae sunt in Cana Galilaeae, et erat mater Iesu ibi.
2 naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
Vocatus est autem et Iesus, et discipuli eius ad nuptias.
3 Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!”
Et deficiente vino, dicit mater Iesu ad eum: Vinum non habent.
4 Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.”
Et dicit ei Iesus: Quid mihi, et tibi est, mulier? nondum venit hora mea.
5 Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”
Dicit mater eius ministris: Quodcumque dixerit vobis, facite.
6 Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
Erant autem ibi lapideae hydriae sex positae secundum purificationem Iudaeorum, capientes singulae metretas binas vel ternas.
7 Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu.
Dicit eis Iesus: Implete hydrias aqua. Et impleverunt eas usque ad summum.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.”
Et dicit eis Iesus: Haurite nunc, et ferte architriclino. Et tulerunt.
9 Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
Ut autem gustavit architriclinus aquam vinum factam, et non sciebat unde esset, ministri autem sciebant, qui hauserant aquam: vocat sponsum architriclinus,
10 akamwambia, “Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!”
et dicit ei: Omnis homo primum bonum vinum ponit: et cum inebriati fuerint, tunc id, quod deterius est. Tu autem servasti bonum vinum usque adhuc.
11 Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
Hoc fecit initium signorum Iesus in Cana Galilaeae: et manifestavit gloriam suam, et crediderunt in eum discipuli eius.
12 Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
Post haec descendit Capharnaum ipse, et mater eius, et fratres eius, et discipuli eius: et ibi manserunt non multis diebus.
13 Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
Et prope erat Pascha Iudaeorum, et ascendit Iesus Ierosolymam:
14 Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
et invenit in templo vendentes boves, et oves, et columbas, et numularios sedentes.
15 Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
Et cum fecisset quasi flagellum de funiculis, omnes eiecit de templo, oves quoque, et boves, et numulariorum effudit aes, et mensas subvertit.
16 Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, “Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!”
Et his, qui columbas vendebant, dixit: Auferte ista hinc, et nolite facere domum patris mei, domum negotiationis.
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: “Upendo wangu kwa nyumba yako waniua.”
Recordati sunt vero discipuli eius quia scriptum est: Zelus domus tuae comedit me.
18 Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, “Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?”
Responderunt ergo Iudaei, et dixerunt ei: Quod signum ostendis nobis quia haec facis?
19 Yesu akawaambia, “Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu.”
Respondit Iesus, et dixit eis: Solvite templum hoc, et in tribus diebus excitabo illud.
20 Hapo Wayahudi wakasema, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?”
Dixerunt ergo Iudaei: Quadraginta et sex annis aedificatum est templum hoc, et tu in tribus diebus excitabis illud?
21 Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
Ille autem dicebat de templo corporis sui.
22 Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
Cum ergo resurrexisset a mortuis, recordati sunt discipuli eius, quia hoc dicebat, et crediderunt scripturae, et sermoni, quem dixit Iesus.
23 Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
Cum autem esset Ierosolymis in pascha in die festo, multi crediderunt in nomine eius, videntes signa eius, quae faciebat.
24 Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
Ipse autem Iesus non credebat semetipsum eis, eo quod ipse nosset omnes,
25 Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
et quia opus ei non erat ut quis testimonium perhiberet de homine: ipse enim sciebat quid esset in homine.

< Yohana 2 >