< Yohana 2 >
1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
Le troisième jour, il y avait un repas de noce à Cana en Galilée. La mère de Jésus s'y trouvait,
2 naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
et Jésus également avait été invité avec ses disciples.
3 Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!”
Le vin étant venu à manquer, la mère de Jésus dit à celui-ci: «Ils n'ont plus de vin.» —
4 Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.”
«Femme, lui répondit Jésus, qu'y a-t-il entre toi et moi? mon heure n'est pas encore venue.»
5 Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”
Sa mère dit à ceux qui servaient: «Faites ce qu'il vous dira.»
6 Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
Or, il y avait là six urnes de pierre disposées pour les ablutions qui sont en usage parmi les Juifs. Chacune d'elles contenait deux ou trois mesures.
7 Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu.
«Remplissez d'eau les urnes», dit Jésus aux serviteurs. Ils les remplirent jusqu'au bord.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.”
«Puisez-y maintenant, leur dit Jésus, et portez-en à l'ordonnateur du repas.» Ils lui en portèrent.
9 Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
Quand celui-ci eut goûté l'eau devenue vin, — n'en sachant point la provenance, comme la savaient les serviteurs qui avaient puisé l'eau, — il appelle l'époux
10 akamwambia, “Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!”
et lui dit: «Tout le monde offre d'abord le bon vin à ses convives et, quand ils sont en ébriété, il leur en donne de qualité inférieure; quant à toi, tu as réservé le bon vin jusqu'à maintenant.»
11 Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
Tel fut, à Cana en Galilée, le commencement des miracles faits par Jésus. Ainsi il manifesta sa gloire et ses disciples crurent en lui.
12 Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
Après cela, il descendit à Capharnaüm, avec sa mère, ses frères et ses disciples. Il n'y demeura que peu de jours.
13 Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
La Pâque des Juifs était proche et il monta à Jérusalem.
14 Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
Dans le Temple, il trouva les marchands de boeufs, de brebis, de colombes, les changeurs installés.
15 Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
Se faisant alors un fouet avec des cordes, il les chassa tous du Temple ainsi que les brebis et les boeufs; il répandit sur le sol la monnaie des changeurs et renversa leurs tables
16 Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, “Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!”
et, quant aux marchands de colombes, il leur dit: «Emportez tout cela et ne faites pas de la maison de mon Père une maison de trafic.»
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: “Upendo wangu kwa nyumba yako waniua.”
Ses disciples se souvinrent qu'il est écrit: «Le zèle de ta maison me dévore.»
18 Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, “Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?”
Cependant les Juifs s'adressèrent à lui; ils lui dirent: «Quel miracle nous montres-tu pour agir de la sorte?»
19 Yesu akawaambia, “Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu.”
Jésus leur répondit par ces paroles: «Renversez ce Temple et en trois jours je le relèverai!» —
20 Hapo Wayahudi wakasema, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?”
«Il a fallu, reprirent les Juifs, quarante-six ans pour bâtir ce Temple et toi tu le relèverais en trois jours!»
21 Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
Mais lui, il parlait du Temple de son corps;
22 Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
et lorsqu'il fut ressuscité d'entre les morts, ses disciples se souvinrent de ce langage, et ils crurent alors à l'Écriture et à la parole dite par Jésus.
23 Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
Pendant qu'il était à Jérusalem, à la fête de Pâque, un grand nombre, à la vue des miracles qu'il faisait, crurent en son nom.
24 Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
Mais lui, Jésus, ne se fiait pas à eux, parce qu'il les connaissait tous. Il n'avait pas besoin en effet que tel ou tel témoignage vînt le renseigner sur qui que ce soit;
25 Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
il savait par-lui-même ce qu'il y avait en chacun.