< Yohana 2 >
1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
And on the third day after, there was a marriage at Cana of Galilee: and the mother of Jesus was there.
2 naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
And Jesus and his disciples were invited to the wedding.
3 Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!”
And the wine falling short, the mother of Jesus saith unto Him, They have no wine.
4 Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.”
Jesus saith unto her, Woman, what have I to do with thee? my time is not yet come.
5 Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.”
His mother saith to the servants, Whatsoever he ordereth you to do, do it.
6 Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
And there were six stone waterpots, placed according to the custom of purifying among the Jews, containing each about two or three firkins.
7 Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu.
Jesus saith unto them, Fill the water-pots with water: and they filled them up to the brim.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.”
And he saith unto them, Draw out now, and carry it to the master of the feast. And they carried it to him.
9 Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
And when the manager of the feast had tasted the water which was made wine, and knew not whence it was, (but the servants, that drew the water, knew, ) he called the bride-groom,
10 akamwambia, “Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!”
and saith unto him, Every man sets out good wine at first, and when they have drank plentifully, then that which is worse; but thou hast keep the good wine till now.
11 Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
This beginning of his miracles Jesus wrought at Cana of Galilee, and made manifest his glory: and his disciples believed on Him.
12 Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
After this He went down to Capernaum, He and his mother, and his brethren, and his disciples: but they staid there not many days.
13 Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
For the passover of the Jews was near, and Jesus went up to Jerusalem. And He found in the temple those that sold oxen,
14 Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
and sheep, and doves, and the money changers sitting:
15 Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
and having made a whip of small cords He drove them all, out of the temple; with the sheep and the oxen: and He poured out the changers money, and threw down the tables.
16 Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, “Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!”
And said to them that sold doves, Take away these things from hence, and make not my Father's house an house of traffick.
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: “Upendo wangu kwa nyumba yako waniua.”
And his disciples remembered that it is written, The zeal of thine house hath eaten me up.
18 Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, “Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?”
The Jews therefore answered and said unto Him, What sign dost thou shew us, seeing thou dost these things?
19 Yesu akawaambia, “Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu.”
Jesus answered and said unto them, Destroy this temple, and in three days I will raise it up again: then said the Jews,
20 Hapo Wayahudi wakasema, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?”
Forty and six years has this temple been in building, and wilt thou raise it up in three days? but He spake of the temple of his body.
21 Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
Therefore when he was risen from the dead,
22 Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
his disciples remembered, that He had said this to them: and they believed the scripture, and the word which Jesus had said.
23 Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
And when he was in Jerusalem at the passover on the feast-day, many believed in his name, seeing his miracles, which He wrought.
24 Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
But Jesus did not trust Himself to them;
25 Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
for He knew all men, and He had no need that any should testify concerning man; for He knew what was in man.